< Numbers 2 >
1 And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying:
Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
2 All the children of Israel shall camp by their troops, ensigns, and standards, and the houses of their kindreds, round about the tabernacle of the covenant.
“Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
3 On the east Juda shall pitch his tents by the bands of his army: and the prince of his sons shall be Nahasson the son of Aminadab.
Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
4 And the whole sum of the fighting men of his stock, were seventy-four thousand six hundred.
Kundi lake lina watu 74,600.
5 Next unto him they of the tribe of Issachar encamped, whose prince was Nathanael, the son of Suar.
Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
6 And the whole number of his fighting men were fifty-four thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 54,400.
7 In the tribe of Zabulon the prince was Eliab the son of Helon.
Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
8 And all the army of fighting men of his stock, were fifty-seven thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 57,400.
9 All that were numbered in the camp of Juda, were a hundred and eighty-six thousand four hundred: and they by their troops shall march first.
Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
10 In the camp of the sons of Ruben, on the south side, the prince shall be Elisur the son of Sedeur:
Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
11 And the whole army of his fighting men, that were numbered, were forty-six thousand five hundred.
Kundi lake lina watu 46,500.
12 Beside him camped they of the tribe of Simeon: whose prince was Salamiel the son of Surisaddai.
Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
13 And the whole army of his fighting men, that were numbered, were fifty-nine thousand three hundred.
Kundi lake lina watu 59,300.
14 In the tribe of Gad the prince was Eliasaph the son of Duel.
Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
15 And the whole army of his fighting men that were numbered, were forty-five thousand six hundred and fifty.
Kundi lake lina watu 45,650.
16 All that were reckoned up in the camp of Ruben, were a hundred and fifty-one thousand four hundred and fifty, by their troops: they shall march in the second place.
Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
17 And the tabernacle of the testimony shall be carried by the officers of the Levites and their troops. As it shall be set up, so shall it be taken down. Every one shall march according to their places, and ranks.
Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
18 On the west side shall be the camp of the sons of Ephraim, whose prince was Elisama, the son of Ammiud.
Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
19 The whole army of his fighting men, that were numbered, were forty thousand five hundred.
Kundi lake lina watu 40,500.
20 And with them the tribe of the sons of Manasses, whose prince was Gamaliel the son of Phadassur.
Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
21 And the whole army of his fighting men, that were numbered, were thirty-two thousand two hundred.
Kundi lake lina watu 32,200.
22 In the tribe of the sons of Benjamin the prince was Abidan the son of Gedeon.
Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
23 And the whole army of his fighting men, that were reckoned up, were thirty-five thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 35,400.
24 All that were numbered in the camp of Ephraim, were a hundred and eight thousand one hundred by their troops: they shall march in the third place.
Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
25 On the north side camped the sons of Dan: whose prince was Ahiezar the son of Ammisaddai.
Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26 The whole army of his fighting men, that were numbered, were sixty-two thousand seven hundred.
Kundi lake lina watu 62,700.
27 Beside him they of the tribe of Aser pitched their tents: whose prince was Phegiel the son of Ochran.
Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
28 The whole army of his fighting men, that were numbered, were forty-one thousand five hundred.
Kundi lake lina watu 41,500.
29 Of the tribe of the sons of Nephtali the prince was Ahira the son of Enan.
Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
30 The whole army of his fighting men, were fifty-three thousand four hundred.
Kundi lake lina watu 53,400.
31 All that were numbered in the camp of Dan, were a hundred and fifty-seven thousand six hundred: and they shall march last.
Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
32 This is the number of the children of Israel, of their army divided according to the houses of their kindreds and their troops, six hundred and three thousand five hundred and fifty.
Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
33 And the Levites were not numbered among the children of Israel: for so the Lord had commanded Moses.
Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
34 And the children of Israel did according to all things that the Lord had commanded. They camped by their troops, and marched by the families and houses of their fathers.
Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.