< Leviticus 3 >

1 And if his oblation be a sacrifice of peace offerings, and he will offer of the herd, whether male or female, he shall offer them without blemish before the Lord.
“‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
2 And he shall lay his hand upon the head of his victim, which shall be slain in the entry of the tabernacle of the testimony, and the sons of Aaron the priests shall pour the blood round about upon the altar.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 And they shall offer of the sacrifice of peace offerings, for an oblation to the Lord, the fat that covereth the entrails, and all the fat that is within.
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
4 The two kidneys with the fat wherewith the flanks are covered, and the caul of the liver with the two little kidneys.
figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
5 And they shall burn them upon the altar, for a holocaust, putting fire under the wood: for an oblation of most sweet savour to the Lord.
Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
6 But if his oblation and the sacrifice of peace offering be of the flock, whether he offer male or female, they shall be without blemish.
“‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
7 If he offer a lamb before the Lord,
Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
8 He shall put his hand upon the head of his victim: and it shall be slain in the entry of the tabernacle of the testimony: and the sons of Aaron shall pour the blood thereof round about upon the altar.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
9 And they shall offer of the victim of peace offerings a sacrifice to the Lord: the fat and the whole rump,
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
10 With the kidneys, and the fat that covereth the belly and all the vitals and both the little kidneys, with the fat that is about the flanks, and the caul of the liver with the little kidneys.
figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
11 And the priest shall burn them upon the altar, for the food of the fire, and of the oblation of the Lord.
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
12 If his offering be a goat, and he offer it to the Lord,
“‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
13 He shall put his hand upon the head thereof: and shall immolate it in the entry of the tabernacle of the testimony. And the sons of Aaron shall pour the blood thereof round about upon the altar.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
14 And they shall take of it for the food of the Lord’s fire, the fat that covereth the belly, and that covereth all the vital parts:
Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
15 The two little kidneys with the caul that is upon them which is by the flanks, and the fat of the liver with the little kidneys:
figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
16 And the priest shall burn them upon the altar, for the food of the fire, and of a most sweet savour. All the fat shall be the Lord’s.
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
17 By a perpetual law for your generations, and in all your habitations: neither blood nor fat shall you eat at all.
“‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”

< Leviticus 3 >