< John 8 >

1 And Jesus went unto mount Olivet.
Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
2 And early in the morning he came again into the temple, and all the people came to him, and sitting down he taught them.
Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
3 And the scribes and the Pharisees bring unto him a woman taken in adultery: and they set her in the midst,
Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
4 And said to him: Master, this woman was even now taken in adultery.
Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
5 Now Moses in the law commanded us to stone such a one. But what sayest thou?
Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
6 And this they said tempting him, that they might accuse him. But Jesus bowing himself down, wrote with his finger on the ground.
Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
7 When therefore they continued asking him, he lifted up himself, and said to them: He that is without sin among you, let him first cast a stone at her.
Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
8 And again stooping down, he wrote on the ground.
Akainama tena na kuandika ardhini.
9 But they hearing this, went out one by one, beginning at the eldest. And Jesus alone remained, and the woman standing in the midst.
Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
10 Then Jesus lifting up himself, said to her: Woman, where are they that accused thee? Hath no man condemned thee?
Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
11 Who said: No man, Lord. And Jesus said: Neither will I condemn thee. Go, and now sin no more.
Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
12 Again therefore, Jesus spoke to them, saying: I am the light of the world: he that followeth me, walketh not in darkness, but shall have the light of life.
Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 The Pharisees therefore said to him: Thou givest testimony of thyself: thy testimony is not true.
Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
14 Jesus answered, and said to them: Although I give testimony of myself, my testimony is true: for I know whence I came, and whither I go: but you know not whence I come, or whither I go.
Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 You judge according to the flesh: I judge not any man.
Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
16 And if I do judge, my judgment is true: because I am not alone, but I and the Father that sent me.
Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
17 And in your law it is written, that the testimony of two men is true.
Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
18 I am one that give testimony of myself: and the Father that sent me giveth testimony of me.
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
19 They said therefore to him: Where is thy Father? Jesus answered: Neither me do you know, nor my Father: if you did know me, perhaps you would know my Father also.
Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
20 These words Jesus spoke in the treasury, teaching in the temple: and no man laid hands on him, because his hour was not yet come.
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
21 Again therefore Jesus said to them: I go, and you shall seek me, and you shall die in your sin. Whither I go, you cannot come.
Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
22 The Jews therefore said: Will he kill himself, because he said: Whither I go, you cannot come?
Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
23 And he said to them: You are from beneath, I am from above. You are of this world, I am not of this world.
Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 Therefore I said to you, that you shall die in your sins. For if you believe not that I am he, you shall die in your sin.
Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
25 They said therefore to him: Who art thou? Jesus said to them: The beginning, who also speak unto you.
Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
26 Many things I have to speak and to judge of you. But he that sent me, is true: and the things I have heard of him, these same I speak in the world.
Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 And they understood not, that he called God his Father.
Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
28 Jesus therefore said to them: When you shall have lifted up the Son of man, then shall you know, that I am he, and that I do nothing of myself, but as the Father hath taught me, these things I speak:
Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
29 And he that sent me, is with me, and he hath not left me alone: for I do always the things that please him.
Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
30 When he spoke these things, many believed in him.
Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
31 Then Jesus said to those Jews, who believed him: If you continue in my word, you shall be my disciples indeed.
Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
32 And you shall know the truth, and the truth shall make you free.
Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
33 They answered him: We are the seed of Abraham, and we have never been slaves to any man: how sayest thou: you shall be free?
Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
34 Jesus answered them: Amen, amen I say unto you: that whosoever committeth sin, is the servant of sin.
Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 Now the servant abideth not in the house for ever; but the son abideth for ever. (aiōn g165)
Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn g165)
36 If therefore the son shall make you free, you shall be free indeed.
Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
37 I know that you are the children of Abraham: but you seek to kill me, because my word hath no place in you.
Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
38 I speak that which I have seen with my Father: and you do the things that you have seen with your father.
Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
39 They answered, and said to him: Abraham is our father. Jesus saith to them: If you be the children of Abraham, do the works of Abraham.
Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
40 But now you seek to kill me, a man who have spoken the truth to you, which I have heard of God. This Abraham did not.
Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
41 You do the works of your father. They said therefore to him: We are not born of fornication: we have one Father, even God.
Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
42 Jesus therefore said to them: If God were your Father, you would indeed love me. For from God I proceeded, and came; for I came not of myself, but he sent me:
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 Why do you not know my speech? Because you cannot hear my word.
Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
44 You are of your father the devil, and the desires of your father you will do. He was a murderer from the beginning, and he stood not in the truth; because truth is not in him. When he speaketh a lie, he speaketh of his own: for he is a liar, and the father thereof.
Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
45 But if I say the truth, you believe me not.
Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
46 Which of you shall convince me of sin? If I say the truth to you, why do you not believe me?
Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
47 He that is of God, heareth the words of God. Therefore you hear them not, because you are not of God.
Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
48 The Jews therefore answered, and said to him: Do not we say well that thou art a Samaritan, and hast a devil?
Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
49 Jesus answered: I have not a devil: but I honour my Father, and you have dishonoured me.
Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
50 But I seek not my own glory: there is one that seeketh and judgeth.
Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
51 Amen, amen I say to you: If any man keep my word, he shall not see death for ever. (aiōn g165)
Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn g165)
52 The Jews therefore said: Now we know that thou hast a devil. Abraham is dead, and the prophets; and thou sayest: If any man keep my word, he shall not taste death for ever. (aiōn g165)
Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn g165)
53 Art thou greater than our father Abraham, who is dead? and the prophets are dead. Whom dost thou make thyself?
Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Jesus answered: If I glorify myself, my glory is nothing. It is my Father that glorifieth me, of whom you say that he is your God.
Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
55 And you have not known him, but I know him. And if I shall say that I know him not, I shall be like to you, a liar. But I do know him, and do keep his word.
Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
56 Abraham your father rejoiced that he might see my day: he saw it, and was glad.
Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
57 The Jews therefore said to him: Thou art not yet fifty years old, and hast thou seen Abraham?
Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
58 Jesus said to them: Amen, amen I say to you, before Abraham was made, I am.
Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
59 They took up stones therefore to cast at him. But Jesus hid himself, and went out of the temple.
Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.

< John 8 >