< Job 38 >
1 Then the Lord answered Job out of a whirlwind, and said:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 Who is this that wrappeth up sentences in unskillful words?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Gird up thy loins like a man: I will ask thee, and answer thou me.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Where wast thou when I laid up the foundations of the earth? tell me if thou hast understanding.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Who hath laid the measures thereof, if thou knowest? or who hath stretched the line upon it?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 Upon what are its bases grounded? or who laid the corner stone thereof,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 When the morning stars praised me together, and all the sons of God made a joyful melody?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Who shut up the sea with doors, when it broke forth as issuing out of the womb:
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 When I made a cloud the garment thereof, and wrapped it in a mist as in swaddling bands?
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 I set my bounds around it, and made it bars and doors:
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 And I said: Hitherto thou shalt come, and shalt go no further, and here thou shalt break thy swelling waves.
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Didst thou since thy birth command the morning, and shew the dawning of the day its place?
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 And didst thou hold the extremities of the earth shaking them, and hast thou shaken the ungodly out of it?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 The seal shall be restored as clay, and shall stand as a garment:
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 From the wicked their light shall be taken away, and the high arm shall be broken.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Hast thou entered into the depths of the sea, and walked in the lowest parts of the deep?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Have the gates of death been opened to thee, and hast thou seen the darksome doors?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 Hast thou considered the breadth of the earth? tell me, if thou knowest all things?
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Where is the way where light dwelleth, and where is the place of darkness:
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 That thou mayst bring every thing to its own bounds, and understand the paths of the house thereof.
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Didst thou know then that thou shouldst be born? and didst thou know the number of thy days?
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Hast thou entered into the storehouses of the snow, or has thou beheld the treasures of the hail:
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 Which I have prepared for the time of the enemy, against the day of battle and war?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 By what way is the light spread, and heat divided upon the earth?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Who gave a course to violent showers, or a way for noisy thunder:
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 That it should rain on the earth without man in the wilderness, where no mortal dwelleth:
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 That it should fill the desert and desolate land, and should bring forth green grass?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Who is the father of rain? or who begot the drops of dew?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 Out of whose womb came the ice; and the frost from heaven who hath gendered it?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 The waters are hardened like a stone, and the surface of the deep is congealed.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Shalt thou be able to join together the shining stars the Pleiades, or canst thou stop the turning about of Arcturus?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Canst thou bring forth the day star in its time, and make the evening star to rise upon the children of the earth?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Dost thou know the order of heaven, and canst thou set down the reason thereof on the earth?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Canst thou lift up thy voice to the clouds, that an abundance of waters may cover thee?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Canst thou send lightnings, and will they go, and will they return and say to thee: Here we are?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Who hath put wisdom in the heart of man? or who gave the cock understanding?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Who can declare the order of the heavens, or who can make the harmony of heaven to sleep?
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 When was the dust poured on the earth, and the clods fastened together?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Wilt thou take the prey for the lioness, and satisfy the appetite of her whelps,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 When they couch in the dens and lie in wait in holes?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Who provideth food for the raven, when her young ones cry to God, wandering about, because they have no meat?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?