< Job 37 >

1 At this my heart trembleth, and is moved out of its place.
Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
2 Hear ye attentively the terror of his voice, and the sound that cometh out of his mouth.
Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
3 He beholdeth under all the heavens, and his light is upon the ends of the earth.
Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
4 After it a noise shall roar, he shall thunder with the voice of his majesty, and shall not be found out, when his voice shall be heard.
Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
5 God shall thunder wonderfully with his voice, he that doth great and unsearchable things.
Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
6 He commandeth the snow to go down upon the earth, and the winter rain, and the shower of his strength.
Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
7 He sealeth up the hand of all men, that every one may know his works.
Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
8 Then the beast shall go into his covert, and shall abide in his den.
Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
9 Out of the inner parts shall a tempest come, and cold out of the north.
Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
10 When God bloweth there cometh frost, and again the waters are poured out abundantly.
Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
11 Corn desireth clouds, and the clouds spread their light:
Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
12 Which go round about, whithersoever the will of him that governeth them shall lead them, to whatsoever he shall command them upon the face of the whole earth:
Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
13 Whether in one tribe, or in his own land, or in what place soever of his mercy he shall command them to be found.
Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
14 Hearken to these things, Job: Stand, and consider the wondrous works of God.
Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
15 Dost thou know when God commanded the rains, to shew his light of his clouds?
Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
16 Knowest thou the great paths of the clouds, and the perfect knowledges?
Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
17 Are not thy garments hot, when the south wind blows upon the earth?
Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
18 Thou perhaps hast made the heavens with him, which are most strong, as if they were of molten brass.
Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
19 Shew us what we may say to him: for we are wrapped up in darkness.
Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
20 Who shall tell him the things I speak? even if a man shall speak, he shall be swallowed up.
Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
21 But now they see not the light: the air on a sudden shall be thickened into clouds, and the wind shall pass and drive them away.
Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
22 Cold cometh out of the north, and to God praise with fear.
Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
23 We cannot find him worthily: he is great in strength, and in judgment, and in justice, and he is ineffable.
Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
24 Therefore men shall fear him, and all that seem to themselves to be wise, shall not dare to behold him.
Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”

< Job 37 >