< Job 37 >
1 At this my heart trembleth, and is moved out of its place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Hear ye attentively the terror of his voice, and the sound that cometh out of his mouth.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He beholdeth under all the heavens, and his light is upon the ends of the earth.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 After it a noise shall roar, he shall thunder with the voice of his majesty, and shall not be found out, when his voice shall be heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God shall thunder wonderfully with his voice, he that doth great and unsearchable things.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 He commandeth the snow to go down upon the earth, and the winter rain, and the shower of his strength.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 He sealeth up the hand of all men, that every one may know his works.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Then the beast shall go into his covert, and shall abide in his den.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Out of the inner parts shall a tempest come, and cold out of the north.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 When God bloweth there cometh frost, and again the waters are poured out abundantly.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Corn desireth clouds, and the clouds spread their light:
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Which go round about, whithersoever the will of him that governeth them shall lead them, to whatsoever he shall command them upon the face of the whole earth:
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Whether in one tribe, or in his own land, or in what place soever of his mercy he shall command them to be found.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Hearken to these things, Job: Stand, and consider the wondrous works of God.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Dost thou know when God commanded the rains, to shew his light of his clouds?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Knowest thou the great paths of the clouds, and the perfect knowledges?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Are not thy garments hot, when the south wind blows upon the earth?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Thou perhaps hast made the heavens with him, which are most strong, as if they were of molten brass.
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Shew us what we may say to him: for we are wrapped up in darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Who shall tell him the things I speak? even if a man shall speak, he shall be swallowed up.
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 But now they see not the light: the air on a sudden shall be thickened into clouds, and the wind shall pass and drive them away.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Cold cometh out of the north, and to God praise with fear.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 We cannot find him worthily: he is great in strength, and in judgment, and in justice, and he is ineffable.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Therefore men shall fear him, and all that seem to themselves to be wise, shall not dare to behold him.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”