< Job 31 >

1 I made a covenant with my eyes, that I would not so much as think upon a virgin.
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 For what part should God from above have in me, and what inheritance the Almighty from on high?
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 Is not destruction to the wicked, and aversion to them that work iniquity?
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 Doth not he consider my ways, and number all my steps?
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 If I have walked in vanity, and my foot hath made haste to deceit:
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 Let him weigh me in a just balance, and let God know my simplicity.
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 If my step hath turned out of the way, and if my heart hath followed my eyes, and if a spot hath cleaved to my hands:
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 Then let me sow and let another eat: and let my offspring be rooted out.
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 If my heart hath been deceived upon a woman, and if I have laid wait at my friend’s door:
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 Let my wife be the harlot of another, and let other men lie with her.
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 For this is a heinous crime, and a most grievous iniquity.
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 It is a fire that devoureth even to destruction, and rooteth up all things that spring.
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 If I have despised to abide judgment with my manservant, or my maidservant, when they had any controversy against me:
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 For what shall I do when God shall rise to judge? and when he shall examine, what shall I answer him?
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 Did not he that made me in the womb make him also: and did not one and the same form me in the womb?
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 If I have denied to the poor what they desired, and have made the eyes of the widow wait:
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 If I have eaten my morsel alone, and the fatherless hath not eaten thereof:
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 (For from my infancy mercy grew up with me: and it came out with me from my mother’s womb: )
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 If I have despised him that was perishing for want of clothing, and the poor man that had no covering:
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 If his sides have not blessed me, and if he were not warmed with the fleece of my sheep:
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 If I have lifted up my hand against the fatherless, even when I saw myself superior in the gate:
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 Let my shoulder fall from its joint, and let my arm with its bones be broken.
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 For I have always feared God as waves swelling over me, and his weight I was not able to bear.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 If I have thought gold my strength, and have said to fine gold: My confidence:
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 If I have rejoiced over my great riches, and because my hand had gotten much.
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 If I beheld the sun when it shined, and the moon going in brightness:
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 And my heart in secret hath rejoiced, and I have kissed my hand with my mouth:
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 Which is a very great iniquity, and a denial against the most high God.
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 If I have been glad at the downfall of him that hated me, and have rejoiced that evil had found him.
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 For I have not given my mouth to sin, by wishing a curse to his soul.
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 If the men of my tabernacle have not said: Who will give us of his flesh that we may be filled?
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 The stranger did not stay without, my door was open to the traveller.
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 If as a man I have hid my sin, and have concealed my iniquity in my bosom.
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 If I have been afraid at a very great multitude, and the contempt of kinsmen hath terrified me: and I have not rather held my peace, and not gone out of the door.
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 Who would grant me a hearer, that the Almighty may hear my desire; and that he himself that judgeth would write a book,
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 That I may carry it on my shoulder, and put it about me as a crown?
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 At every step of mine I would pronounce it, and offer it as to a prince.
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 If my land cry against me, and with it the furrows thereof mourn:
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 If I have eaten the fruits thereof without money, and have afflicted the soul of the tillers thereof:
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 Let thistles grow up to me instead of wheat, and thorns instead of barley.
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.

< Job 31 >