< Job 30 >
1 But now the younger in time scorn me, whose fathers I would not have set with the dogs of my flock:
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 The strength of whose hands was to me as nothing, and they were thought unworthy of life itself.
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Barren with want and hunger, who gnawed in the wilderness, disfigured with calamity and misery.
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 And they ate grass, and barks of trees, and the root of junipers was their food.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Who snatched up these things out of the valleys, and when they had found any of them, they ran to them with a cry.
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 They dwelt in the desert places of torrents, and in caves of earth, or upon the gravel.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 They pleased themselves among these kind of things, and counted it delightful to be under the briers.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 The children of foolish and base men, and not appearing at all upon the earth.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Now I am turned into their song, and am become their byword.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 They abhor me, and flee far from me, and are not afraid to spit in my face.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 For he hath opened his quiver, and hath afflicted me, and hath put a bridle into my mouth.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 At the right hand of my rising, my calamities forthwith arose: they have overthrown my feet, and have overwhelmed me with their paths as with waves.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 They have destroyed my ways, they have lain in wait against me, and they have prevailed, and there was none to help.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 They have rushed in upon me, as when a wall is broken, and a gate opened, and have rolled themselves down to my miseries.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 I am brought to nothing: as a wind thou hast taken away my desire: and my prosperity hath passed away like a cloud.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 And now my soul fadeth within myself, and the days of affliction possess me.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 In the night my bone is pierced with sorrows: and they that feed upon me, do not sleep.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 With the multitude of them my garment is consumed, and they have girded me about, as with the collar of my coat.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 I am compared to dirt, and am likened to embers and ashes.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 I cry to thee, and thou hearest me not: I stand up, and thou dost not regard me.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Thou art changed to be cruel toward me, and in the hardness of thy hand thou art against me.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Thou hast lifted me up, and set me as it were upon the wind, and thou hast mightily dashed me.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 I know that thou wilt deliver me to death, where a house is appointed for every one that liveth.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 But yet thou stretchest not forth thy hand to their consumption: and if they shall fall down thou wilt save.
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 I wept heretofore for him that was afflicted, and my soul had compassion on the poor.
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 I expected good things, and evils are come upon me: I waited for light, and darkness broke out.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 My inner parts have boiled without any rest, the days of affliction have prevented me.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 I went mourning without indignation; I rose up, and cried in the crowd.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 I was the brother of dragons, and companion of ostriches.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 My skin is become black upon me, and my bones are dried up with heat.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 My harp is turned to mourning, and my organ into the voice of those that weep.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.