< Job 23 >
1 Then Job answered, and said:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Now also my words are in bitterness, and the hand of my scourge is more grievous than my mourning.
“Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
3 Who will grant me that I might know and find him, and come even to his throne?
Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
4 I would set judgment before him, and would fill my mouth with complaints.
Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
5 That I might know the words that he would answer me, and understand what he would say to me.
Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
6 I would not that he should contend with me with much strength, nor overwhelm me with the weight of his greatness.
Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
7 Let him propose equity against me, and let my judgment come to victory.
Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
8 But if I go to the east, he appeareth not; if to the west, I shall not understand him.
Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
9 If to the left hand, what shall I do? I shall not take hold on him: if I turn myself to the right hand, I shall not see him.
Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
10 But he knoweth my way, and has tried me as gold that passeth through the fire:
Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
11 My foot hath followed his steps, I have kept his way, and have not declined from it.
Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
12 I have not departed from the commandments of his lips, and the words of his mouth I have hid in my bosom.
Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
13 For he is alone, and no man can turn away his thought: and whatsoever is soul hath desired, that hath he done.
Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
14 And when he shall have fulfilled his will in me, many other like things are also at hand with him.
Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
15 And therefore I am troubled at his presence, and when I consider him I am made pensive with fear.
Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
16 God hath softened my heart, and the Almighty hath troubled me.
Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
17 For I have not perished because of the darkness that hangs over me, neither hath the mist covered my face.
Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.