< Jeremiah 44 >
1 The word that came to Jeremias, concerning all the Jews that dwelt in the land of Egypt, dwelling in Magdal, and in Taphnis, and in Memphis, and in the land of Phatures, saying:
Hili lilikuwa neno ambalo lilikuja kwa Yeremia kuhusu Wayahudi wote walioishi katika nchi ya Misri, wale wanaoishi Migdoli, Tahpanhesi, Memphis, na katika nchi ya Patrosi.
2 Thus saith the Lord of hosts the God of Israel: You have seen all this evil that I have brought upon Jerusalem, and upon all the cities of Juda: and behold they are desolate this day, and there is not an inhabitant in them:
“Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi: Wewe mwenyewe umeyaona maafa yote niliyoleta juu ya Yerusalemu na miji yote ya Yuda. Ona, ni ukiwa leo. Hakuna yeyote anaishi mwao.
3 Because of the wickedness which they have committed, to provoke me to wrath, and to go and offer sacrifice, and worship other gods, which neither they, nor you, nor your fathers knew.
Hii ni kwa sababu ya mambo maovu waliyofanya kunikosea mimi kwa kwenda kuchoma ubani na kuabudu miungu mengine. Hawa walikuwa miungu ambao wala wao wenyewe, wala ninyi, wala mababu zenu walijua.
4 And I sent to you all my servants the prophets, rising early, and sending, and saying: Do not commit this abominable thing, which I hate.
Basi nirudie kuwatuma watumwa wangu wote manabii kwao. Niliwatuma wao kusema, 'Acha kufanya vitu hivi machukizo ambayo nachukia.
5 But they heard not, nor inclined their ear to turn from their evil ways, and not to sacrifice to strange gods.
Lakini hawakunisikiliza. Walikataa kuwa makini au kuyaacha maovu kwa kuchoma ubani kwa miungu mingine.
6 Wherefore my indignation and my fury was poured forth, and was kindled in the cities of Juda, and in the streets of Jerusalem: and they are turned to desolation and waste, as at this day.
Basi hasira yangu na gadhabu yangu zilimwanga na kuwasha moto kwenye miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu. Basi waliharibiwa na kuteketezwa, kama katika siku ya leo.”
7 And now thus saith the Lord of hosts the God of Israel: Why do you commit this great evil against your own souls, that there should die of you man and woman, child and suckling out of the midst of Juda, and no remnant should be left you:
Basi sasa Yahwe, Mungu wa majeshi na Mungu wa Israel, asema hivi, “Kwanini unafanya maovu makubwa dhidi yenu? Kwanini mnasababisha ninyi wenyewe kujitenga kutoka miongoni mwa Yuda - wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao? Hakuna mabaki yenu yatabaki.
8 In that you provoke me to wrath with the works of your hands, by sacrificing to other gods in the land of Egypt, into which you are come to dwell there: and that you should perish, and be a curse, and a reproach to all the nations of the earth?
Kwa maovu yenu mmenikosea pamoja na matendo ya mikono yenu, kwa kuchoma ubani kwa miungu mingine kwenye nchi ya Misri, ambapo mmekwenda kuishi. Mmeenda huko ili kwamba mtaangamizwa, ili kwamba mtalaaniwa na mashutumu miongoni mwa mataifa yote ya duniani.
9 Have you forgotten the evils of your fathers, and the evils of the kings of Juda, and the evils of their wives, and your evils, and the evils of your wives, that they have done in the land of Juda, and in the streets of Jerusalem?
Mmesahau maovu yaliyofanywa na mababu zenu na maouvu yaliyofanywa na wafalme wa Yuda na wake zao? Mmesahau uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu?
10 They are not cleansed even to this day: neither have they feared, nor walked in the law of the Lord, nor in my commandments, which I set before you and your fathers.
Kwa siku hii, hawajanyenyekea bado. Hawashimu sheria yangu au maagizo niliyoweka mbele yao na mababu zao, wala hawatembei nazo.”
11 Therefore thus saith the Lord of hosts the God of Israel: Behold I will set my face upon you for evil: and I will destroy all Juda.
Kwa hiyo sasa Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, “Ona, Nimekaribia kuweka uso wangu dhidi yenu kuleta maafa kwenu na kuiharibu Yuda yote.
12 And I will take the remnant of Juda that have set their faces to go into the land of Egypt, and to dwell there: and they shall be all consumed in the land of Egypt: they shall fall by the sword, and by the famine: and they shall be consumed from the least even to the greatest, by the sword, and by the famine shall they die: and they shall be for an execration, and for a wonder, and for a curse, and for a reproach.
Kwa kuwa nitachukua mabaki wa Yuda ambaye ameanza safari kwenda nchi ya Misri kuishi huko. Nitafanya hivi ili kwamba wataangamia wote katika nchi ya Misri. Wataanguka kwa upanga na njaa. Kutoka wadogo kwa wakubwa wataangamia kwa upanga na njaa. Watakufa na watakuwa sababu ya kuaapa, kulaani, mashutumu, na kitu kibaya.
13 And I will visit them that dwell in the land of Egypt, as I have visited Jerusalem by the sword, and by famine, and by pestilence.
Kwa kuwa nitawaadhibu watu wakazi wa nchi ya Misri kama nilivyoadhibu Yerusalem kwa upanga, njaa, na pigo.
14 And there shall be none that shall escape, and remain of the remnant of the Jews that are gone to sojourn in the land of Egypt: and that shall return into the land of Juda, to which they have a desire to return to dwell there: there shall none return but they that shall flee.
Hakuna mkimbizi au mwathirika wa mabaki ya Yuda ambaye wataenda kuishi huko kwenye nchi ya Misri watarudi kwenye nchi ya Yuda, hata kama wanataka kurudi na kuishi huko. Hakuna kati yao atarudi, ijapokuwa wachache ambayo watatoroka kutoka huko.”
15 Then all the men that knew that their wives sacrificed to other gods: and all the women of whom there stood by a great multitude, and all the people of them that dwelt in the land of Egypt in Phatures, answered Jeremias, saying:
Kisha watu wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakichoma ubani kwa miungu mingine, na wanawake wote waliokuwa katika kusanyiko kuu, na watu wote ambao walikuwa wakiishi kwenye nchi ya Misri katika Pathrosi walimjibu Yeremia.
16 As for the word which thou hast spoken to us in the name of the Lord, we will not hearken to thee:
Walisema, “Kuhusu neno ambalo mmetuambia sisi kwa jina la Yahwe: Hatutakusikiliza.
17 But we will certainly do every word that shall proceed out of our own mouth, to sacrifice to the queen of heaven, and to pour out drink offerings to her, as we and our fathers have done, our kings, and our princes in the cities of Juda, and in the streets of Jerusalem: and we were filled with bread, and it was well with us, and we saw no evil.
Kwa hakika tutafanya mambo yote ambayo tulisema tungefanya: kuchoma ubani kwa malkia wa Mbingu na kumwaga kinywaji cha sadaka kwake kama sisi, mababu zetu, wafalme wetu, na viongozi wetu walivyofanya kwenye miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu. Kisha tutajazwa pamoja na chakula na tutafanikiwa, pasipo kupata maafa yoyote.
18 But since we left off to offer sacrifice to the queen of heaven, and to pour out drink offerings to her, we have wanted all things, and have been consumed by the sword, and by famine.
Wakati tunajiepusha kutofanya mambo haya, si kutoa sadaka ya ubani kwa Malkia wa Mbinguni na si kumwanga kinywaji cha sadaka kwake, tulikuwa wote tunaumwa umaskini na tulikuwa tunakufa kwa upanga na njaa.”
19 And if we offer sacrifice to the queen of heaven, and pour out drink offerings to her: did we make cakes to worship her, to pour out drink offerings to her, without our husbands?
Wanawake walisema, “Wakati tulipokuwa tunatengeneza ubani wa sadaka mbele ya Malkia wa Mbinguni na kumwaga kinywaji cha sadaka kwake, tulifanya hivi vitu pasipo waume wetu kujua.”
20 And Jeremias spoke to all the people, to the men, and to the women, and to all the people which had given him that answer, saying:
Kisha Yeremia alisema kwa watu wote - kwa wanaume na wanawake, na watu wote waliomjibu yeye - alihubiri na kusema,
21 Was it not the sacrifice that you offered in the cities of Juda, and in the streets of Jerusalem, you and Sour fathers, your kings, and your princes, and the people of the land, which the Lord hath remembered, and hath it not entered into his heart?
“Je Yahwe hakukumbuka ubani ambao mliuchoma kwenye miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalem - wewe na mababu zenu, wafalme wenu na viongozi, na watu wa nchi? Kwa kuwa Yahwe anakumbuka hili kwenye akili; inakuja kwenye mawazo yake.
22 So that the Lord could no longer bear, because of the evil of your doings, and because of the abominations which you have committed: therefore your land is become a desolation, and an astonishment, and a curse, without an inhabitant, as at this day.
Basi hawakuweza tena kuvumilia kwa sababu ya matendo yenu maovu, kwa sababu machukizo ambayo mlifanya. Basi nchi yenu imekuwa ukiwa, kutisha, na laana basi hapakuwa na mkazi tena kwa siku hii.
23 Because you have sacrificed to idols, and have sinned against the Lord: and have not obeyed the voice of the Lord, and have not walked in his law, and in his commandments, and in his testimonies: therefore are these evils come upon you, as at this day.
Kwa sababu mlichoma ubani na kufanya dhambi dhidi ya Yahwe, na kwa sababu msingesikiliza sauti yake, sheria yake, amri zake, au maagizo ya agano lake, maafa haya dhidi yenu yemetokea kama kwa siku hii. “
24 And Jeremias said to all the people, and to all the women: Hear ye the word of the Lord, all Juda, you that dwell in the land of Egypt:
Kisha Yeremia alisema kwa watu wote na wanawake wote, “Sikia neno la Yahwe, Yuda yote ambao wamo katika nchi ya Misri.
25 Thus saith the Lord of hosts the God of Israel, saying: You and your wives have spoken with your mouth, and fulfilled with your hands, saying: Let us perform our vows which we have made, to offer sacrifice to the queen of heaven, and to pour out drink offerings to her: you have fulfilled your vows, and have performed them indeed.
Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israel, asema hivi, Wewe na wake zako wote mmesema kwa vinywa vyenu na kubeba kwa mikono yenu kile mlichosema, “Hakika tutabeba viapo ambavyo tulifanya kumwabudu Malkia wa Mbinguni, kwanga kinywaji cha sadaka kwake.” Sasa timiza viapo vyenu, vibebe.”
26 Therefore hear ye the word of the Lord, all Juda, you that dwell in the land of Egypt: Behold I have sworn by my great name, saith the Lord: that my name shall no more be named in the mouth of any man of Juda, in the land of Egypt, saying: The Lord God liveth.
Basi, sikiliza neno la Yahwe, Yuda yote ambao mnaishi katika nchi ya Misri, 'Ona, Nimeapa kwa jina langu kuu-asema Yahwe. Jina langu halitaitwa kwa vinywa vya wanaume wowote wa Yuda kwenye nchi ya Misri, wewe ambaye sasa unasema, “Kama Bwana Yahwe aishivyo.”
27 Behold I will watch over them for evil, and not for good: and all the men of Juda that are in the land of Egypt, shall be consumed, by the sword, and by famine, till there be an end of them.
Ona, Ninakutazama juu yako kwa ajili ya maafa na si kwa uzuri. Kila mtu wa Yuda katika nchi ya Misri ataangamia kwa upanga na njaa mpaka wote wameishia.
28 And a few men that shall flee from the sword, shall return out of the land of Egypt into the land of Juda: and all the remnant of Juda that are gone into the land of Egypt to dwell there, shall know whose word shall stand, mine, or theirs.
Kisha waathirika wa upanga watarudi kutoka nchi ya Misri kwa nchi ya Yuda, peke idadi ndogo yao. Basi mabaki yote ya Yuda walioenda kwenye nchi ya Misri kuishi huko watajua ambao neno litakuwa kweli: yangu au yao.
29 And this shall be a sign to you, saith the Lord, that I will punish you in this place: that you may know that my words shall be accomplished indeed against you for evil.
Hii itakuwa ishara kwa ajili yako - hili ni tamko la Yahwe - kwamba ninaweka dhidi yenu katika eneo hili, ili kwamba mtajua kwamba maneno yangu hakika yatawavamia pamoja na maafa.
30 Thus saith the Lord: Behold I will deliver Pharao Ephree king of Egypt into the hand of his enemies, and into the hand of them that seek his life: as I delivered Sedecias king of Juda into the hand of Nabuchodonosor the king of Babylon his enemy, and that sought his life.
Yahwe asema hivi, 'Tazama, ninakaribia kumtoa Farao Hofra mfalme wa Misri kwenye mkono wa adui zake na kwenye mkono wa wale wanaotafuta kumuua. Itakuwa sawa kama wakati nilimpa Sedekia mfalme wa Yuda kwenye mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, adui wake aliyetafuta maisha yake.