< Jeremiah 1 >

1 The words of Jeremias the son of Helcias, of the priests that were in Anathoth, in the land of Benjamin.
Hili ndilo neno la Yeremia mwana wa Hilikia; yeye alikuwa mmoja wa makuhani kule Anatothi katika nchi ya Benjamini.
2 The word of the Lord which came to him in the days of Josias the son of Amon king of Juda, in the thirteenth year of his reign.
Neno la BWANA lilimjia katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wake.
3 And which came to him in the days of Joakim the son of Josias king of Juda, unto the end of the eleventh year of Sedecias the son of Josias king of Juda, even unto the carrying away of Jerusalem captive, in the fifth month.
Lakini pia lilimjia katika wakati wa Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka mwezi wa tano wa mwaka wa kumi na moja wa Zedekia mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, wakati watu wa Yerusalemu walipochukuliwa kuwa watumwa.
4 And the word of the Lord came to me, saying:
Neno la BWANA lilinijia, likisema,
5 Before I formed thee in the bowels of thy mother, I knew thee: and before thou camest forth out of the womb, I sanctified thee, and made thee a prophet unto the nations.
“kabla sijakuumba tumboni, Nilikuchagua; kabla hujazailiwa toka tumboni Nilikutenga; Nilikufanya kuwa nabii kwa mataifa.”
6 And I said: Ah, ah, ah, Lord God: behold, I cannot speak, for I am a child.
“Ahaa, BWANA!” Nilisema, “mimi sijui kusema, kwa kuwa mimi ni mtoto.”
7 And the Lord said to me: Say not: I am a child: for thou shalt go to all that I shall send thee: and whatsoever I shall command thee, thou shalt speak.
Lakini BWANA akaniambia, “Usiseme, 'mimi ni mtoto.' Utaenda kila mahali ninapokutuma, na utasema kila kitu ninachokuamuru!
8 Be not afraid at their presence: for I am with thee to deliver thee, saith the Lord.
Usiwaogpe hao, kwa kuwa Mimi niko pamoja na wewe kukuokoa- asema BWANA.”
9 And the Lord put forth his hand, and touched my mouth: and the Lord said to me: Behold I have given my words in thy mouth:
Kisha BWANA akanyosh mkono wake, akagusa kinywa changu, na akaniambia, “Nimeweka maneno yangu kinywani mwako.
10 Lo, I have set thee this day over the nations, and over the kingdoms, to root up, and pull down, and to waste, and to destroy, and to build, and to plant.
Nimekuchagua leo juu ya mataifa na juu ya mataifa, ili kung'oa na kuvunja, kuharibu na kutupa, kujenga na kupanda.”
11 And the word of the Lord came to me, saying: What seest thou, Jeremias? And I said: I see a rod watching.
Neno la BWANA lilinijia, likisema, “Yeremia, unaona nini?” Nikasema, “Ninaona tawi la mlozi.”
12 And the Lord said to me: Thou hast seen well: for I will watch over my word to perform it.
BWANA akaniambia, “umeona vyema, kwa kuwa ninaliangalia neno langu ili nilitimize.”
13 And the word of the Lord came to me a second time, saying: What seest thou? I see a boiling caldron, and the face thereof from the face of the north.
Neno la BWANA likaniji mara ya pili likisema, “Unaona nini? “Nikasema, “Ninaona chungu kikichemuka, ambacho mdomo wake unaelekea toka upande wa kaskazini,”
14 And the Lord said to me: from the north shall an evil break forth upon all the inhabitants of the land.
BWANA akaniambia, “Janga litatokea kaskazini juu ya wote wanaoishi katika nchi hii.
15 For behold I will call together all the families of the kingdoms of the north: saith the Lord: and they shall come, and shall set every one his throne in the entrance of the gates of Jerusalem, and upon all the walls thereof round about, and upon all the cities of Juda,
Kwa kuwa ninayaita makabila yote ya falme za kaskazini, asema BWANA. Yatakuja, na kila mmoja atasimika enzi yake katika malango ya Yerusalemu, dhidi ya kuta zote zinazoizunguka, na dhidi ya miji ya Yuda.
16 And I will pronounce my judgements against them, touching all their wickedness, who have forsaken me, and have sacrificed to strange gods, and have adored the work of their own hands.
Nitatamka hukumu dhidi yao juu ya uovu wao wa kuniacha, kwa kufukiza uvumba kwa miungu mingine, na kwa kuabudu kile walichotengeneza kwa mikono yao.
17 Thou therefore gird up thy loins, and arise, and speak to them all that I command thee. Be not afraid at their presence: for I will make thee not to fear their countenance.
Jiandae! Simama ukawaambie kila kitu ninachokuamuru. Usifdhaike mbele zao nisije nikakufadhaisha wewe mbele zao!
18 For behold I have made thee this day a fortified city, and a pillar of iron, and a wall of brass, over all the land, to the kings of Juda, to the princes thereof, and to the priests, and to the people of the land.
Tazama! Leo nimekufanya kuwa mji ulio na ngome, kuwa ngome ya chuma, na ukata wa shaba dhidi ya nchi yote - dhidi ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wote wa nchi.
19 And they shall fight against thee, and shall not prevail: for I am with thee, saith the Lord, to deliver thee.
Watapigana na wewe, lakinai hawatakushinda, kwa kuwa nitakuwa pamoja na wewe ili kukuokoa- asema BWANA.”

< Jeremiah 1 >