< Isaiah 13 >

1 The burden of Babylon, which Isaias the son of Amos saw.
Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:
2 Upon the dark mountain lift ye up a banner, exalt the voice, lift up the hand, and let the rulers go into the gates.
Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu, wapazieni sauti, wapungieni mkono waingie katika malango ya wenye heshima.
3 I have commanded my sanctified ones, and have called my strong ones in my wrath, them that rejoice in my glory.
Nimewaamuru watakatifu wangu; nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu: wale wanaoshangilia ushindi wangu.
4 The noise of a multitude in the mountains, as it were of many people, the noise of the sound of kings, of nations gathered together: the Lord of hosts hath given charge to the troops of war.
Sikilizeni kelele juu ya milima, kama ile ya umati mkubwa wa watu! Sikilizeni, makelele katikati ya falme, kama mataifa yanayokusanyika pamoja! Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya jeshi kwa ajili ya vita.
5 To them that come from a country afar off, from the end of heaven: tile Lord and the instruments of his wrath, to destroy the whole land.
Wanakuja kutoka nchi za mbali sana, kutoka miisho ya mbingu, Bwana na silaha za ghadhabu yake, kuangamiza nchi yote.
6 Howl ye, for the day of the Lord is near: it shall come as a destruction from the Lord.
Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu, itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.
7 Therefore shall all hands be faint, and every heart of man shall melt,
Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
8 And shall be broken. Gripings and pains shall take hold of them, they shall be in pain as a woman in labour. Every one shall be amazed at his neighbour, their countenances shall be as faces burnt.
Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.
9 Behold, the day of the Lord shall come, a cruel day, and full of indignation, and of wrath, and fury, to lay the land desolate, and to destroy the sinners thereof out of it.
Tazameni, siku ya Bwana inakuja, siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali, kuifanya nchi kuwa ukiwa na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.
10 For the stars of heaven, and their brightness shall not display their light: the sun shall be darkened in his rising, and the moon shall not shine with her light.
Nyota za mbinguni na makundi ya nyota havitatoa mwanga wake. Jua linalochomoza litatiwa giza na mwezi hautatoa nuru yake.
11 And I will visit the evils of the world, and against the wicked for their iniquity: and I will make the pride of infidels to cease, and will bring down the arrogancy of the mighty.
Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake, waovu kwa ajili ya dhambi zao. Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi, na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.
12 A man shall be more precious than gold, yea a man than the finest of gold.
Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi, watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.
13 For this I will trouble the heaven: and the earth shall be moved out of her place, for the indignation of the Lord of hosts, and for the day of his tierce wrath.
Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke, nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika siku ya hasira yake iwakayo.
14 And they shall be as a doe fleeing away, and as a sheep: and there shall be none to gather them together: every man shall turn to his own people, and every one shall flee to his own land.
Kama swala awindwaye, kama kondoo wasio na mchungaji, kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.
15 Every one that shall be found, shall be slain: and every one that shall come to their aid, shall fall by the sword.
Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo, wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.
16 Their infants shall be dashed in pieces before their eyes: their houses shall be pillaged, and their wives shall be ravished.
Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande mbele ya macho yao; nyumba zao zitatekwa na wake zao watatendwa jeuri.
17 Behold I will stir up the Medes against them, who shall not seek silver, nor desire gold:
Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao, ambao hawajali fedha wala hawafurahii dhahabu.
18 But with their arrows they shall kill the children, and shall have no pity upon the sucklings of the womb, and their eye shall not spare their sons.
Mishale yao itawaangusha vijana, hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga wala hawataangalia watoto kwa huruma.
19 And that Babylon, glorious among kingdoms, the famous pride of the Chaldeans, shall be even as the Lord destroyed Sodom and Gomorrha.
Babeli, johari ya falme, utukufu wa kiburi cha Wababeli, itaangushwa na Mungu kama Sodoma na Gomora.
20 It shall no more be inhabited for ever, and it shall not be founded unto generation and generation: neither shall the Arabian pitch his tents there, nor shall shepherds rest there.
Hautakaliwa na watu kamwe wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko, hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.
21 But wild beasts shall rest there, and their houses shall be filled with serpents, and ostriches shall dwell there, and the hairy ones shall dance there:
Lakini viumbe wa jangwani watalala huko, mbweha watajaza nyumba zake, bundi wataishi humo nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.
22 And owls shall answer one another there, in the houses thereof, and sirens in the temples of pleasure.
Fisi watalia ndani ya ngome zake, mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari. Wakati wake umewadia, na siku zake hazitaongezwa.

< Isaiah 13 >