< Hebrews 3 >

1 Wherefore, holy brethren, partakers of the heavenly vocation, consider the apostle and high priest of our confession, Jesus:
Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa wito wa mbinguni, mumfikiri Yesu, Mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
2 Who is faithful to him that made him, as was also Moses in all his house.
Alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua, kama Musa alivyokuwa mwaminifu pia katika nyumba yote ya Mungu.
3 For this man was counted worthy of greater glory than Moses, by so much as he that hath built the house, hath greater honour than the house.
Kwa kuwa Yesu amehesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko aliyokuwa nayo Musa, kwa sababu yule anayejenga nyumba anahesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
4 For every house is built by some man: but he that created all things, is God.
Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule anayejenga kila kitu ni Mungu.
5 And Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were to be said:
Hakika Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi katika nyumba yote ya Mungu, akitoa ushuhuda kuhusu mambo yatakayosemwa wakati ujao.
6 But Christ as the Son in his own house: which house are we, if we hold fast the confidence and glory of hope unto the end.
Lakini Kristo ni Mwana katika usimamizi wa nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tutashikilia haraka katika kujiamini na fahari ya kujiamini.
7 Wherefore, as the Holy Ghost saith: Today if you shall hear his voice,
Kwa hiyo, ni kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, kama utasikia sauti yake,
8 Harden not your hearts, as in the provocation; in the day of temptation in the desert,
Usiufanye moyo wako kuwa mgumu kama Waisraeli walivyofanya katika uasi, katika wakati wa kujaribiwa nyikani.
9 Where your fathers tempted me, proved and saw my works,
Huu ulikuwa wakati ambao baba zenu waliniasi kwa kunijaribu, na wakati, kwa miaka arobaini, waliona matendo yangu.
10 Forty years: for which cause I was offended with this generation, and I said: They always err in heart. And they have not known my ways,
Kwa hiyo sikufurahishwa na kizazi hicho. Nilisema, 'Wanapotea kila mara katika mioyo yao, na hawajui njia zangu.
11 As I have sworn in my wrath: If they shall enter into my rest.
Ni kama vile nilivyoapa katika hasira yangu: hawataiingia raha yangu.”
12 Take heed, brethren, lest perhaps there be in any of you an evil heart of unbelief, to depart from the living God.
Muwe waangalifu, ndugu, ili kwamba usije ukawepo moyo mwovu wa kutokuamini kwa mmoja wenu, moyo ambao utakwenda mbali na Mungu aliye hai.
13 But exhort one another every day, whilst it is called today, that none of you be hardened through the deceitfulness of sin.
Badala yake, mhamasishane kila siku kila mmoja na mwenzie, ili kila iitwapo leo mtamani, ili kwamba mmoja kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
14 For we are made partakers of Christ: yet so, if we hold the beginning of his substance firm unto the end.
Kwa maana tumekuwa washiriki wa Kristo ikiwa tutashikamana na uthabiti wetu kwa nguvu katika yeye kutoka mwanzo hadi mwisho.
15 While it is said, Today if you shall hear his voice, harden not your hearts, as in that provocation.
Kuhusu hili imekwisha kusemwa, “Leo kama mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu, kama Waisraeli walivyofanya wakati wa uasi.”
16 For some who heard did provoke: but not all that came out of Egypt by Moses.
Ni akina nani hao waliomsikia Mungu na kuasi? Hawakuwa wale wote ambao Musa alikuwa amewaongoza kutoka Misri?
17 And with whom was he offended forty years? Was it not with them that sinned, whose carcasses were overthrown in the desert?
Na kina nani ambao Mungu aliwakasirikia kwa miaka arobaini? Siyo pamoja na wale waliotenda dhambi, ambao miili yao iliyokufa ililala jangwani?
18 And to whom did he swear, that they should not enter into his rest: but to them that were incredulous?
Ni akina nani aliowaapia Mungu kwamba hawataingia katika raha yake, kama siyo wale ambao hawakumtii yeye?
19 And we see that they could not enter in, because of unbelief.
Tunaona kwamba hawakuweza kuingia katika raha yake kwa sababu ya kutokuamini.

< Hebrews 3 >