< Genesis 5 >
1 This is the book of the generation of Adam. In the day that God created man, he made him to the likeness of God.
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 He created them male and female; and blessed them: and called their name Adam, in the day when they were created.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 And Adam lived a hundred and thirty years, and begot a son to his own image and likeness, and called his name Seth.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 And the days of Adam, after he begot Seth, were eight hundred years: and he begot sons and daughters.
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 And all the time that Adam lived came to nine hundred and thirty years, and he died.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 Seth also lived a hundred and five years, and begot Enos.
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 And Seth lived after he begot Enos, eight hundred and seven years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 And all the days of Seth were nine hundred and twelve years, and he died.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 And Enos lived ninety years, and begot Cainan.
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 After whose birth he lived eight hundred and fifteen years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 And all the days of Enos were nine hundred and five years, and he died.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 And Cainan lived seventy years, and begot Malaleel.
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 And Cainan lived after he begot Malaleel, eight hundred and forty years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 And all the days of Cainan were nine hundred and ten years, and he died.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 And Malaleel lived sixty-five years, and begot Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 And Malaleel lived after he begot Jared, eight hundred and thirty years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 And all the days of Malaleel were eight hundred and ninety-five years, and he died.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 And Jared lived a hundred and sixty-two years, and begot Henoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 And Jared lived after he begot Henoch, eight hundred years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 And all the days of Jared were nine hundred and sixty-two years, and he died.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 And Henoch lived sixty-five years, and begot Mathusala.
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 And Henoch walked with God: and lived after he begot Mathusala, three hundred years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 And all the days of Henoch were three hundred and sixty-five years.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 And he walked with God, and was seen no more: because God took him.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 And Mathusala lived a hundred and eighty-seven years, and begot Lamech.
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 And Mathusala lived after he begot Lamech, seven hundred and eighty-two years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 And all the days of Mathusala were nine hundred and sixty-nine years, and he died.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 And Lamech lived a hundred and eighty-two years, and begot a son.
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 And he called his name Noe, saying: This same shall comfort us from the works and labours of our hands on the earth, which the Lord hath cursed.
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 And Lamech lived after he begot Noe, five hundred and ninety-five years, and begot sons and daughters.
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 And all the days of Lamech came to seven hundred and seventy-seven years, and he died.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 And Noe, when he was five hundred years old, begot Sem, Cham, and Japheth.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.