< Genesis 11 >

1 And the earth was of one tongue, and of the same speech.
Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
2 And when they removed from the east, they found a plain in the land of Sennaar, and dwelt in it.
Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
3 And each one said to his neighbour: Come, let us make brick, and bake them with fire. And they had brick instead of stones, and slime instead of mortar.
Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
4 And they said: Come, let us make a city and a tower, the top whereof may reach to heaven: and let us make our name famous before we be scattered abroad into all lands.
Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
5 And the Lord came down to see the city and the tower, which the children of Adam were building.
Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
6 And he said: Behold, it is one people, and all have one tongue: and they have begun to do this, neither will they leave off from their designs, till they accomplish them in deed.
Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
7 Come ye, therefore, let us go down, and there confound their tongue, that they may not understand one another’s speech.
Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
8 And so the Lord scattered them from that place into all lands, and they ceased to build the city.
Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
9 And therefore the name thereof was called Babel, because there the language of the whole earth was confounded: and from thence the Lord scattered them abroad upon the face of all countries.
Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
10 These are the generations of Sem: Sem was a hundred years old when he begot Arphaxad, two years after the flood.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
11 And Sem lived after he begot Arphaxad, five hundred years, and begot sons and daughters.
Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
12 And Arphaxad lived thirty-five years, and begot Sale.
Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
13 And Arphaxad lived after he begot Sale, three hundred and three years; and begot sons and daughters.
Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
14 Sale also lived thirty years, and begot Heber.
Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 And Sale lived after he begot Heber, four hundred and three years; and begot sons and daughters.
Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
16 And Heber lived thirty-four years, and begot Phaleg.
Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 And Heber lived after he begot Phaleg, four hundred and thirty years: and begot sons and daughters.
Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
18 Phaleg also lived thirty years, and begot Reu.
Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 And Phaleg lived after he begot Reu, two hundred and nine years, and begot sons and daughters.
Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
20 And Reu lived thirty-two years, and begot Sarug.
Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
21 And Reu lived after he begot Sarug, two hundred and seven years, and begot sons and daughters.
Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
22 And Sarug lived thirty years, and begot Nachor.
Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 And Sarug lived after he begot Nachor, two hundred years: and begot sons and daughters.
Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
24 And Nachor lived nine and twenty years, and begot Thare.
Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 And Nachor lived after he begot Thare, a hundred and nineteen years: and begot sons and daughters.
Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
26 And Thare lived seventy years, and begot Abram, and Nachor, and Aran.
Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
27 And these are the generations of Thare: Thare begot Abram, Nachor, and Aran. And Aran begot Lot.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
28 And Aran died before Thare his father, in the land of his nativity in Ur of the Chaldees.
Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
29 And Abram and Nachor married wives: the name of Abram’s wife was Sarai: and the name of Nachor’s wife, Melcha, the daughter of Aran, father of Melcha, and father of Jescha.
Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
30 And Sarai was barren, and had no children.
Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
31 And Thare took Abram, his son, and Lot the son of Aran, his son’s son, and Sarai his daughter in law, the wife of Abram his son, and brought them out of Ur of the Chaldees, to go into the land of Chanaan: and they came as far as Haran, and dwelt there.
Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
32 And the days of Thare were two hundred and five years, and he died in Haran.
Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.

< Genesis 11 >