< Ezekiel 27 >

1 And the word of the Lord came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Thou therefore, O son of man, take up a lamentation for Tyre:
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
3 And say to Tyre that dwelleth at the entry of the sea, being the mart of the people for many islands: Thus saith the Lord God: O Tyre, thou hast said: I am of perfect beauty,
Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
4 And situate in the heart of the sea. Thy neighbours, that built thee, have perfected thy beauty:
Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
5 With fir trees of Sanir they have built thee with all sea planks: they have taken cedars from Libanus to make thee masts.
Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
6 They have cut thy oars out of the oaks of Basan: and they have made thee benches of Indian ivory and cabins with things brought from the islands of Italy.
Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
7 Fine broidered linen from Egypt was woven for thy sail, to be spread on thy mast: blue and purple from the islands of Elisa, were made thy covering.
Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
8 The inhabitants of Sidon, and the Arabians were thy rowers: thy wise men, O Tyre, were thy pilots.
Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
9 The ancients of Gebal, and the wise men thereof furnished mariners for the service of thy various furniture: all the ships of the sea, and their mariners were thy factors.
Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
10 The Persians, and Lydians, and the Libyans were thy soldiers in thy army: they hung up the buckler and the helmet in thee for thy ornament.
“‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
11 The men of Arad were with thy army upon thy walls round about: the Pygmeans also that were in thy towers, hung up their quivers on thy walls round about: they perfected thy beauty.
Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
12 The Carthaginians thy merchants supplied thy fairs with a multitude of all kinds of riches, with silver, iron, tin, and lead.
“‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
13 Greece, Thubal, and Mosoch, they were thy merchants: they brought to thy people slaves and vessels of brass.
“‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
14 From the house of Thogorma they brought horses, and horsemen, and mules to thy market.
“‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
15 The men of Dedan were thy merchants: many islands were the traffic of thy hand, they exchanged for thy price teeth of ivory and ebony.
“‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
16 The Syrian was thy merchant: by reason of the multitude of thy works, they set forth precious stones, and purple, and broidered works, and fine linen, and silk, and chodchod in thy market.
“‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
17 Juda and the land of Israel, they were thy merchants with the best corn: they set forth balm, and honey, and oil, and rosin in thy fairs.
“‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
18 The men of Damascus were thy merchants in the multitude of thy works, in the multitude of divers riches, in rich wine, in wool of the best colour.
“‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
19 Dan, and Greece, and Mosel have set forth in thy marts wrought iron: stacte, and calamus were in thy market.
“‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
20 The men of Dedan were thy merchants in tapestry for seats.
“‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
21 Arabia, and all the princes of Cedar, they were the merchants of thy hand: thy merchants came to thee with lambs, and rants, and kids.
“‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 The sellers of Saba, and Reema, they were thy merchants: with all the best spices, and precious stones, and gold, which they set forth in thy market.
“‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
23 Haran, and Chene, and Eden were thy merchants; Saba, Assur, and Chelmad sold to thee.
“‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
24 They were thy merchants in divers manners, with bales of blue cloth, and of embroidered work, and of precious riches, which were wrapped up and bound with cords: they had cedars also in thy merchandise.
Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
25 The ships of the sea, were thy chief in thy merchandise: and thou wast replenished, and glorified exceedingly in the heart of the sea.
“‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
26 Thy rowers have brought thee into great waters: the south wind hath broken thee in the heart of the sea.
Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
27 Thy riches, and thy treasures, and thy manifold furniture, thy mariners, and thy pilots, who kept thy goods, and were chief over thy people: thy men of war also, that were in thee, with all thy multitude that is in the midst of thee: shall fall in the heart of the sea in the day of thy ruin.
Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
28 Thy fleets shall be troubled at the sound of the cry of thy pilots.
Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
29 And all that handled the oar shall come down from their ships: the mariners, and all the pilots of the sea shall stand upon the land:
Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
30 And they shall mourn over thee with a loud voice, and shall cry bitterly: and they shall cast up dust upon their heads, and shall be sprinkled with ashes.
Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
31 And they shall shave themselves bald for thee, and shall be girded with haircloth: and they shall weep for thee with bitterness of soul, with most bitter weeping.
Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
32 And they shall take up a mournful song for thee, and snail lament thee: What city is like Tyre, which is become silent in the midst of the sea?
Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
33 Which by thy merchandise that went from thee by sea didst fill many people: which by the multitude of thy riches, and of thy people didst enrich the kings of the earth.
Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
34 Now thou art destroyed by the sea, thy riches are in the bottom of the waters, and all the multitude that was in the midst of thee is fallen.
Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
35 All the inhabitants of the islands are astonished at thee: and all their kings being struck with the storm have changed their countenance.
Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
36 The merchants of people have hissed at thee: thou art brought to nothing, and thou shalt never be any more.
Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”

< Ezekiel 27 >