< Ezekiel 14 >

1 And some of the ancients of Israel came to me, and sat before me.
Baadhi ya viongozi wa Israeli wakaja kwangu na kuketi mbele yangu.
2 And the word of the Lord came to me, saying:
Ndipo neno la Yahwe likanijia, likisema,
3 Son of man, these men have placed their uncleannesses in their hearts, and have set up before their face the stumblingblock of their iniquity: and shall I answer when they inquire of me?
“Mwanadamu, hawa watu wamchukua sanamu zao kwenye mioyo yao na kuweka pingamizi la uovu wao mbele ya nyuso zao wenyewe. Je naweza kuulizwa yote na wao?
4 Therefore speak to them, and say to them: Thus saith the Lord God: Man, man of the house of Israel that shall place his uncleannesses in his heart, and set up the stumblingblock of his iniquity before his face, and shall come to the prophet inquiring of me by him: I the Lord will answer him according to the multitude of his uncleannesses:
Kwa hiyo watangazie hivi na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kila mtu wa nyumba ya Israeli achukuaye sanamu moyoni mwake, au awekeye pingamizi la uovu mbele ya uso wake, na kisha yule ajaye kwa nabii-Mimi, Yahwe, nitamjibu kulingana na sanamu zake.
5 That the house of Israel may be caught in their own heart, with which they have departed from me through all their idols.
Nitafanya hivi ili kwamba niweze kuirudisha nyumba ya Israeli katika mioyo yao ambayo ilikuwa mbali nami kwa ajili ya sanamu zao.'
6 Therefore say to the house of Israel: Thus saith the Lord God: Be converted, and depart from your idols, and turn away your faces from all your abominations.
Kwa hiyo sema kwa nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tubuni na rudini kutoka kwenye sanamu zenu! Rudisheni nyuma nyuso zenu kutoka kwenye kachukizo yenu yote.
7 For every man of the house of Israel, and every stranger among the proselytes in Israel, if he separate himself from me, and place his idols in his heart, and set the stumblingblock of his iniquity before his face, and come to the prophet to inquire of me by him: I the Lord will answer him by myself.
Kwa kuwa kila mmoja kutoka kwenye nyumba ya Israeli na kila mmoja wa wageni wanaoishi katika Israeli ajitengaye nami, achukuaye sanamu zake kwenye moyo wake na kuweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake mwenyewe, na kisha yule ajaye kwa nabii kunitafuta-mimi, Yahwe, nitamjibu mimi mwenyewe.
8 And I will set my face against that man, and will make him an example, and a proverb, and will cut him off from the midst of my people: and you shall know that I am the Lord.
Hivyo nitauweka uso wangu juu ya huyo mtu na kumfanya ishara na mithali, kwa kuwa nitamkata kutoka kati ya watu wangu, na mtajua kuwa mimi ni Yahwe.
9 And when the prophet shall err, and speak a word: I the Lord have deceived that prophet: and I will stretch forth my hand upon him, and will cut him off from the midst of my people Israel.
Kama nabii atadanganywa na kuongea ujumbe, kisha Mimi Yahwe, nitamdanganya huyo nabii; Nitanyoosha mkono wangu na kumwangamizaku toka kati watu wangu Israeli.
10 And they shall bear their iniquity: according to the iniquity of him that inquireth, so shall the iniquity of the prophet be.
Watabeba uovu wao wenyewe; uwovu wa nabii utakua uleule kama uovu wa yule aulizaye kutoka kwake.
11 That the house of Israel may go no more astray from me, nor be polluted with all their transgressions: but may be my people, and I may be their God, saith the Lord of hosts.
Kwa sababu hiyo basi, nyumba ya Israeli haitaenda mbali kutoka kunifuata mimi wala kujinajisi wenyewe kupitia dhambi zao zote. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao-hivi ndivyo Yahwe asemavyo.”'
12 And the word of the Lord came to me, saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
13 Son of man, when a land shall sin against me, so as to transgress grievously, I will stretch forth my hand upon it, and will break the staff of the bread thereof: and I will send famine upon it, and will destroy man and beast out of it.
“Mwanadamu, wakati nchi itakapo asi dhidi yangu kwa kufanya dhambi ili kwamba ninyooshe mkono wangu dhidi yake na kuvunja tegemea la mkate wake, na kuleta njaa juu yake na kukata mnyama kutoka kwenye nchi;
14 And if these three men, Noe, Daniel, and Job, shall be in it: they shall deliver their own souls by their justice, saith the Lord of hosts.
kisha hata kama hawa watu watatu-Nuhu, Danieli, na Ayubu-walikuwa katikati ya nchi, wangeweza kuokoa maisha yao wenyewe kwa haki-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 And if I shall bring mischievous beasts also upon the land to waste it, and it be desolate, so that there is none that can pass because of the beasts:
Kama nikileta wanyama waovu kwenye nchi na kuwafanya wasizae hivyo basi itakuwa hakuna mtu asiweze kupita kwa sababu ya hao wanyama,
16 If these three men shall be in it, as I live, saith the Lord, they shall deliver neither sons nor daughters: but they only shall be delivered, and the land shall be made desolate.
kisha hata kama watu hawa hawa watatu ndani yake-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuwaokoa hata watoto wao wala binti; isipokuwa maisha yao yataokoka, lakini nchi itakuwa ukiwa.
17 Or if I bring the sword upon that land, and say to the sword: Pass through the land: and I destroy man and beast out of it:
Au nikileta upanga juu ya hiyo nchi na kusema, 'Upanga, nenda kwenye nchi na wakate wote mtu na mnyama kutoka huo',
18 And these three men be in the midst thereof: as I live, saith the Lord God, they shall deliver neither sons nor daughters, but they themselves alone shall be delivered.
kisha hata kama hawa watu watatu watakuwa katikatai ya nchi-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuwaokoa japo watoto wao wala binti; ila tu maisha yao wenyewe yangeokolewa.
19 Or if I also send the pestilence upon that land, and pour out my indignation upon it in blood, to cut off from it man and beast:
Au kama nikipeleka tauni juu ya nchi na kumwaga dhahabu yangu juu yake kwa damu, ili kuwakata mtu na mnyama,
20 And Noe, and Daniel, and Job be in the midst thereof: as I live, saith the Lord God, they shall deliver neither son nor daughter: but they shall only deliver their own souls by their justice.
kisha hata kama Nuhu, Danieli, na Ayubu wangekuwa kwenye hiyo nchi-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuokoa hata watoto wao au binti; maisha yao pekee yangeokoka kwa haki.
21 For thus saith the Lord: Although I shall send in upon Jerusalem my four grievous judgments, the sword, and the famine, and the mischievous beasts, and the pestilence, to destroy out of it man and beast,
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: hakika nitafanya mambo makali sana kwa kuleta adhabu zangu nne-njaa, upanga, wanyama wa porini, na tauni-juu ya Yerusalemu kuwakata wote mtu na mnyama kutoka kwake.
22 Yet there shall be left in it some that shall be saved, who shall bring away their sons and daughters: behold they shall come among you, and you shall see their way, and their doings: and you shall be comforted concerning the evil that I have brought upon Jerusalem, in all things that I have brought upon it.
Kisha, tazama! mabaki yatasalia kwake, watakaokoka wataenda pamoja na wana na binti. Tazama! Watawatokea, na mtaona njia zao na matendo yao yakiwafariji kuhusu adhabu niliyoipeleka Yerusalemu, na kuhusu kila kitu kingine ambacho nilichopeleka juu ya nchi.
23 And they shall comfort you, when you shall see their ways, and their doings: and you shall know that I have not done without cause all that I have done in it, saith the Lord God.
Waliokoka watawafariji ninyi mtakapoona njia zao na matendo yao, hivyo mtayajua haya mambo niliyoyafanya juu yake, kwamba sijayafanya bure! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 14 >