< Ezekiel 13 >
1 And the word of the Lord came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Son of man, prophesy thou against the prophets of Israel that prophesy: and thou shalt say to them that prophesy out of their own heart: Hear ye the word of the Lord:
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Bwana!
3 Thus saith the Lord God: Woe to the foolish prophets that follow their own spirit, and see nothing.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
4 Thy prophets, O Israel, were like foxes in the deserts.
Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
5 You have not gone up to face the enemy, nor have you set up a wall for the house of Israel, to stand in battle in the day of the Lord.
Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kwamba isimame imara kwenye vita katika siku ya Bwana.
6 They see vain things, and they foretell lies, saying: The Lord saith: whereas the Lord hath not sent them: and they have persisted to confirm what they have said.
Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Bwana amesema,” wakati Bwana hakuwatuma, bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
7 Have you not seen a vain vision and spoken a lying divination: and you say: The Lord saith: whereas I have not spoken.
Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu hapo msemapo, “Bwana asema,” lakini Mimi sijasema?
8 Therefore thus saith the Lord God: Because you have spoken vain things, and have seen lies: therefore behold I come against you, saith the Lord God.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ya uongo wa maneno yenu na kwa madanganyo ya maono yenu, Mimi ni kinyume na ninyi, asema Bwana Mwenyezi.
9 And my hand shall be upon the prophets that see vain things, and that divine lies: they shall not be in the council of my people, nor shall they be written in the writing of the house of Israel, neither shall they enter into the land of Israel, and you shall know that I am the Lord God.
Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuandikwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.
10 Because they have deceived my people, saying: Peace, and there is no peace: and the people built up a wall, and they daubed it with dirt without straw.
“‘Kwa sababu ni kweli wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani,” wakati ambapo hakuna amani, pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
11 Say to them that daub without tempering, that it shall fall: for there shall be an overflowing shower, and I will cause great hailstones to fall violently from above, and a stormy wind to throw it down.
kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
12 Behold, when the wall is fallen: shall it not be said to you: Where is the daubing wherewith you have daubed it?
Wakati ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
13 Therefore thus saith the Lord God: Lo, I will cause a stormy wind to break forth in my indignation, and there shall be an overflowing shower in my anger: and great hailstones in my wrath to consume.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, pia katika hasira yangu mvua ya mawe na mvua ya mafuriko itanyesha ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
14 And I will break down the wall that you have daubed with untempered mortar: and I will make it even with the ground, and the foundation thereof shall be laid bare: and it shall fall, and shall be consumed in the midst thereof: and you shall know that I am the Lord.
Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uachwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
15 And I will accomplish my wrath upon the wall, and upon them that daub it without tempering the mortar, and I will say to you: The wall is no more, and they that daub it are no more.
Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
16 Even the prophets of Israel that prophesy to Jerusalem, and that see visions of peace for her: and there is no peace, saith the Lord God.
wale manabii wa Israeli waliotabiri juu ya Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati kulipokuwa hakuna amani, asema Bwana Mwenyezi.”’
17 And thou, son of man, set thy face against the daughters of thy people that prophesy out of their own heart: and do thou prophesy against them,
“Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
18 And say: Thus saith the Lord God: Woe to them that sew cushions under every elbow: and make pillows for the heads of persons of every age to catch souls: and when they caught the souls of my people, they gave life to their souls.
na useme, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
19 And they violated me among my people, for a handful of barley, and a piece of bread, to kill souls which should not die, and to save souls alive which should not live, telling lies to my people that believe lies.
Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwaambia uongo watu wangu, wale ambao husikiliza uongo, mmewaua wale watu ambao wasingekufa na kuwaacha hai wale ambao wasingeishi.
20 Therefore thus saith the Lord God: Behold I declare against your cushions, wherewith you catch flying souls: and I will tear them off from your arms: and I will let go the souls that you catch, the souls that should fly.
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi ambazo kwa hizo mnawatega watu kama ndege, nami nitazirarua kutoka mikononi mwenu, nitawaweka huru watu wale mliowatega kama ndege.
21 And I will tear your pillows, and will deliver my people out of your hand, neither shall they be any more in your hands to be a prey: and you shall know that I am the Lord.
Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
22 Because with lies you have made the heart of the just to mourn, whom I have not made sorrowful: and have strengthened the hands of the wicked, that he should not return from his evil way, and live.
Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
23 Therefore you shall not see vain things, nor divine divinations any more, and I will deliver my people out of your hand: and you shall know that I am the Lord.
kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’”