< Exodus 24 >

1 And he said to Moses: Come up to the Lord, thou, and Aaron, Nadab, and Abiu, and seventy of the ancients of Israel, and you shall adore afar off.
Kisha Mungu akamwambia Mose, “Njooni huku juu kwa Bwana, wewe na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli. Mniabudu kwa mbali,
2 And Moses alone shall come up to the Lord, but they shall not come nigh; neither shall the people come up with him.
lakini Mose peke yake ndiye atakayemkaribia Bwana; wengine wasije karibu. Nao watu wasije wakapanda pamoja naye.”
3 So Moses came and told the people all the words of the Lord, and all the judgments: and all the people answered with one voice: We will do all the words of the Lord, which he hath spoken.
Mose alipokwenda na kuwaambia watu maneno yote na sheria zote za Bwana, wakaitikia kwa sauti moja, “Kila kitu alichosema Bwana tutakifanya.”
4 And Moses wrote all the words of the Lord: and rising in the morning he built an altar at the foot of the mount, and twelve titles according to the twelve tribes of Israel.
Ndipo Mose akaandika kila kitu Bwana alichokuwa amesema. Akaamka kesho yake asubuhi na mapema na kujenga madhabahu chini ya mlima na kusimamisha nguzo kumi na mbili za mawe kuwakilisha makabila kumi na mawili ya Israeli.
5 And he sent young men of the children of Israel, and they offered holocausts, and sacrificed pacific victims of calves to the Lord.
Kisha akawatuma vijana wanaume wa Kiisraeli, nao wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu za mafahali wachanga kuwa sadaka za amani kwa Bwana.
6 Then Moses took half of the blood, and put it into bowls: and the rest he poured upon the altar.
Mose akachukua nusu ya damu ya wale wanyama na kuiweka kwenye mabakuli na nusu nyingine akainyunyiza juu ya madhabahu.
7 And taking the book of the covenant, he read it in the hearing of the people: and they said: All things that the Lord hath spoken we will do, we will be obedient.
Kisha akachukua kile Kitabu cha Agano na kuwasomea watu. Nao wakajibu, “Tutafanya kila kitu alichosema Bwana, nasi tutatii.”
8 And he took the blood and sprinkled it upon the people, and he said: This is the blood of the covenant which the Lord hath made with you concerning all these words.
Ndipo Mose akachukua ile damu, akawanyunyizia wale watu, akasema, “Hii ni damu ya agano ambalo Bwana amelifanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.”
9 Then Moses and Aaron, Nadab and Abiu, and seventy of the ancients of Israel went up:
Mose na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli wakapanda mlimani,
10 And they saw the God of Israel: and under his feet as it were a work of sapphire stone, and as the heaven, when clear.
nao wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa na kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, iliyo safi kama anga angavu.
11 Neither did he lay his hand upon those of the children of Israel, that retired afar off, and they saw God, and they did eat and drink.
Lakini Mungu hakuinua mkono wake dhidi ya hawa viongozi wa Waisraeli; walimwona Mungu, nao wakala na kunywa.
12 And the Lord said to Moses: Come up to me into the mount, and be there: and I will give thee tables of stone, and the law, and the commandments which I have written: that thou mayst teach them.
Bwana akamwambia Mose, “Panda uje kwangu huku mlimani na ukae hapa, nami nitakupa vibao vya mawe, vyenye sheria na amri ambazo nimeziandika ziwe mwongozo wao.”
13 Moses rose up, and his minister Josue: and Moses going up into the mount of God,
Basi Mose akaondoka na Yoshua mtumishi wake, naye Mose akapanda juu kwenye mlima wa Mungu.
14 Said to the ancients: Wait ye here till we return to you. You have Aaron and Hur with you: if any question shall arise, you shall refer it to them.
Mose akawaambia wazee wa Israeli, “Tungojeni hapa mpaka tutakapowarudia. Aroni na Huri wako pamoja nanyi, na kila aliye na neno aweza kuwaendea wao.”
15 And when Moses was gone up, a cloud covered the mount.
Mose alipopanda juu mlimani, wingu liliufunika huo mlima,
16 And the glory of the Lord dwelt upon Sinai, covering it with a cloud six days: and the seventh day he called him out of the midst of the cloud.
nao utukufu wa Bwana ukatua juu ya Mlima Sinai. Kwa muda wa siku sita wingu lilifunika mlima, na siku ya saba Bwana akamwita Mose kutoka katikati ya lile wingu.
17 And the sight of the glory of the Lord was like a burning fire upon the top of the mount, in the eyes of the children of Israel.
Kwa Waisraeli utukufu wa Bwana ulionekana kama moto uteketezao juu ya mlima.
18 And Moses, entering into the midst of the cloud, went up into the mountain: and he was there forty days, and forty nights.
Kisha Mose akaingia ndani ya lile wingu alivyokuwa akipanda mlimani. Naye akakaa huko mlimani kwa muda wa siku arobaini, usiku na mchana.

< Exodus 24 >