< Deuteronomy 29 >
1 These are the words of the covenant which the Lord commanded Moses to make with the children of Israel in the land of Moab: beside that covenant which he made with them in Horeb.
Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
2 And Moses called all Israel, and said to them: You have seen all the things that the Lord did before you in the land of Egypt to Pharao, and to all his servants, and to his whole land.
Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
3 The great temptations, which thy eyes have seen, those mighty signs and wonders,
mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
4 And the Lord hath not given you a heart to understand, and eyes to see, and ears that may hear, unto this present day.
Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
5 He hath brought you forty years through the desert: your garments are not worn out, neither are the shoes of your feet consumed with age.
Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
6 You have not eaten bread, nor have you drunk wine or strong drink: that you might know that I am the Lord your God.
Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
7 And you came to this place: sand Sehon king of Hesebon, and Og king of Basan, came out against us to fight. And we slew them.
Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
8 And took their land, and delivered it for a possession to Ruben and Gad, and the half tribe of Manasses.
Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
9 Keep therefore the words of this covenant, and fulfill them: that you may understand all that you do.
Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
10 You all stand this day before the Lord your God, your princes, and tribes, and ancients, and doctors, all the people of Israel,
Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
11 Your children and your wives, and the stranger that abideth with thee in the camp, besides the hewers of wood, and them that bring water:
watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
12 That thou mayst pass in the covenant of the Lord thy God, and in the oath which this day the Lord thy God maketh with thee.
Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
13 That he may raise thee up a people to himself, and he may be thy God as he hath spoken to thee, and as he swore to thy fathers Abraham, Isaac, and Jacob.
ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
14 Neither with you only do I make this covenant, and confirm these oaths,
Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
15 But with all that are present and that are absent.
pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
16 For you know how we dwelt in the land of Egypt, and how we have passed through the midst of nations, and passing through them,
Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
17 You have seen their abominations and filth, that is to say, their idols, wood and stone, silver and gold, which they worshipped.
Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
18 Lest perhaps there should be among you a man or a woman, a family or a tribe, whose heart is turned away this day from the Lord our God, to go and serve the gods of those nations: and there should be among you a root bringing forth gall and bitterness.
Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
19 And when he shall hear the words of this oath, he should bless himself in his heart saying: I shall have peace, and will walk on in the naughtiness of my heart: and the drunken may consume the thirsty,
Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
20 And the Lord should not forgive him: but his wrath and jealousy against that man should be exceedingly enkindled at that time, and all the curses that are written in this volume should light upon him: and the Lord should blot out his name from under heaven,
Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
21 And utterly destroy him out of all the tribes of Israel, according to the curses that are contained in the book of this law and covenant:
Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
22 And the following generation shall say, and the children that shall be born hereafter, and the strangers that shall come from afar, seeing the plagues of that land and the evils wherewith the Lord hath afflicted it,
Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
23 Burning it with brimstone, and the heat of salt, so that it cannot be sown any more, nor any green thing grow therein, after the example of the destruction of Sodom and Gomorrha, Adama and Seboim, which the Lord destroyed in his wrath and indignation:
na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
24 And all the nations shall say: Why hath the Lord done thus to this land? what meaneth this exceeding great heat of his wrath?
watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
25 And they shall answer: Because they forsook the covenant of the Lord, which he made with their fathers, when he brought them out of the land of Egypt:
Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
26 And they have served strange gods, and adored them, whom they knew not, and for whom they had not been assigned:
na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
27 Therefore the wrath of the Lord was kindled against this land, to bring upon it all the curses that are written in this volume:
Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
28 And he hath cast them out of their land, in anger and in wrath, and in very great indignation, and hath thrown them into a strange land, as it is seen this day.
Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
29 Secret things to the Lord our God: things that are manifest, to us and to our children for ever, that we may do all the words of this law.
Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.