< Daniel 9 >

1 In the first year of Darius the son of Assuerus of the seed of the Medes, who reigned over the kingdom of the Chaldeans:
Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,
2 The first year of his reign, I Daniel understood by books the number of the years, concerning which the word of the Lord came to Jeremias the prophet, that seventy years should be accomplished of the desolation of Jerusalem.
katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.
3 And I set my face to the Lord my God, to pray and make supplication with fasting, and sackcloth, and ashes.
Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.
4 And I prayed to the Lord my God, and I made my confession, and said: I beseech thee, O Lord God, great and terrible, who keepest the covenant, and mercy to them that love thee, and keep thy commandments.
Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu: “Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,
5 We have sinned, we have committed iniquity, we have done wickedly, and have revolted: and we have gone aside from thy commandments, and thy judgments.
tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.
6 We have not hearkened to thy servants the prophets, that have spoken in thy name to our kings, to our princes, to our fathers, and to all the people of the land.
Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.
7 To thee, O Lord, justice: but to us confusion of face, as at this day to the men of Juda, and to the inhabitants of Jerusalem, and to all Israel to them that are near, and to them that are far off in all the countries whither thou hast driven them, for their iniquities by which they have sinned against thee.
“Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.
8 O Lord, to us belongeth confusion of face, to our princes, and to our fathers that have sinned.
Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
9 But to thee, the Lord our God, mercy and forgiveness, for we have departed from thee:
Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake.
10 And we have not hearkened to the voice of the Lord our God, to walk in his law, which he set before us by his servants the prophets.
Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.
11 And all Israel have transgressed thy law, and have turned away from hearing thy voice, and the malediction, and the curse, which is written in the book of Moses the servant of God, is fallen upon us, because we have sinned against him.
Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii. “Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
12 And he hath confirmed his words which he spoke against us, and against our princes that judged us, that he would bring in upon us a great evil, such as never was under all the heaven, according to that which hath been done in Jerusalem.
Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu.
13 As it is written in the law of Moses, all this evil is come upon us: and we entreated not thy face, O Lord our God, that we might turn from our iniquities, and think on thy truth.
Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.
14 And the Lord hath watched upon the evil, and hath brought it upon us: the Lord our God is just in all his works which he hath done: for we have not hearkened to his voice.
Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.
15 And now, O Lord our God, who hast brought forth thy people out of the land of Egypt with a strong hand, and hast made thee a name as at this day: we have sinned, we have committed iniquity,
“Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.
16 O Lord, against all thy justice: let thy wrath and thy indignation be turned away, I beseech thee, from thy city Jerusalem, and from thy holy mountain. For by reason of our sins, and the iniquities of our fathers, Jerusalem, and thy people are a reproach to all that are round about us.
Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.
17 Now therefore, O our God, hear the supplication of thy servant, and his prayers: and shew thy face upon thy sanctuary which is desolate, for thy own sake.
“Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu.
18 Incline, O my God, thy ear, and hear: open thy eyes, and see our desolation, and the city upon which thy name is called: for it is not for our justifications that we present our prayers before thy face, but for the multitude of thy tender mercies.
Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.
19 O Lord, hear: O Lord, be appeased: hearken and do: delay not for thy own sake, O my God: because thy name is invocated upon thy city, and upon thy people.
Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”
20 Now while I was yet speaking, and praying, and confessing my sins, and the sins of my people of Israel, and presenting my supplications in the sight of my God, for the holy mountain of my God:
Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,
21 As I was yet speaking in prayer, behold the man Gabriel, whom I had seen in the vision at the beginning, flying swiftly touched me at the time of the evening sacrifice.
wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.
22 And he instructed me, and spoke to me, and said: O Daniel, I am now come forth to teach thee, and that thou mightest understand.
Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.
23 From the beginning of thy prayers the word came forth: and I am come to shew it to thee, because thou art a man of desires: therefore do thou mark the word, and understand the vision.
Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:
24 Seventy weeks are shortened upon thy people, and upon thy holy city, that transgression may be finished, and sin may have an end, and iniquity may be abolished; and everlasting justice may be brought; and vision and prophecy may be fulfilled; and the saint of saints may be anointed.
“Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.
25 Know thou therefore, and take notice: that from the going forth of the word, to build up Jerusalem again, unto Christ the prince, there shall be seven weeks, and sixty-two weeks: and the street shall be built again, and the walls in straitness of times.
“Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.
26 And after sixty-two weeks Christ shall be slain: and the people that shall deny him shall not be his. And a people with their leader that shall come, shall destroy the city and the sanctuary: and the end thereof shall be waste, and after the end of the war the appointed desolation.
Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.
27 And he shall confirm the covenant with many, in one week: and in the half of the week the victim and the sacrifice shall fall: and there shall be in the temple the abomination of desolation: and the desolation shall continue even to the consummation, and to the end.
Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”

< Daniel 9 >