< 2 Thessalonians 2 >

1 And we beseech you, brethren, by the coming of our Lord Jesus Christ, and of our gathering together unto him:
Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi,
2 That you be not easily moved from your sense, nor be terrified, neither by spirit, nor by word, nor by epistle, as sent from us, as if the day of the Lord were at hand.
msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.
3 Let no man deceive you by any means, for unless there come a revolt first, and the man of sin be revealed, the son of perdition,
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
4 Who opposeth, and is lifted up above all that is called God, or that is worshipped, so that he sitteth in the temple of God, shewing himself as if he were God.
Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
5 Remember you not, that when I was yet with you, I told you these things?
Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya?
6 And now you know what withholdeth, that he may be revealed in his time.
Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia.
7 For the mystery of iniquity already worketh; only that he who now holdeth, do hold, until he be taken out of the way.
Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.
8 And then that wicked one shall be revealed whom the Lord Jesus shall kill with the spirit of his mouth; and shall destroy with the brightness of his coming, him,
Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake.
9 Whose coming is according to the working of Satan, in all power, and signs, and lying wonders,
Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo,
10 And in all seduction of iniquity to them that perish; because they receive not the love of the truth, that they might be saved.
na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.
11 Therefore God shall send them the operation of error, to believe lying:
Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo,
12 That all may be judged who have not believed the truth, but have consented to iniquity.
na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.
13 But we ought to give thanks to God always for you, brethren, beloved of God, for that God hath chosen you firstfruits unto salvation, in sanctification of the spirit, and faith of the truth:
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.
14 Whereunto also he hath called you by our gospel, unto the purchasing of the glory of our Lord Jesus Christ.
Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo.
15 Therefore, brethren, stand fast; and hold the traditions which you have learned, whether by word, or by our epistle.
Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.
16 Now our Lord Jesus Christ himself, and God and our Father, who hath loved us, and hath given us everlasting consolation, and good hope in grace, (aiōnios g166)
Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
17 Exhort your hearts, and confirm you in every good work and word.
awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.

< 2 Thessalonians 2 >