< 2 Kings 11 >
1 And Athalia the mother of Ochozias seeing that her son was dead, arose, and slew all the royal seed.
Basi Athalia, mama yake na Ahazia, alipoona kwamba mtoto wake amekufa, aliinuka na kuwaua watoto wote wa kifalme.
2 But Josaba the daughter of king Joram, sister of Ochozias, took Joas the son of Ochozias, and stole him from among the king’s sons that were slain, out of the bedchamber with his nurse: and hid him from the face of Athalia, so that he was not slain.
Lakini Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu na dada wa Ahazia, akamchukua Yoashi mwana wa Ahazia, na kumficha mbali mwa miongoni mwa watoto wa mfalme waliokuwa wameuawa, wakati wote pamoja na mlezi wake; akawaweka kwenye chumba cha kulala. Wakamficha kutoka Athalia kwa hiyo hakuuawa.
3 And he was with her six years hid in the house of the Lord. And Athalia reigned over the land.
Alikuwa pamoja na Yehosheba, wamejificha kwenye nyumba ya Yahwe, kwa mda wa miaka sita, wakati Athalia alipotawala juu ya nchi.
4 And in the seventh year Joiada seat, and taking the centurions and the soldiers, brought them in to him into the temple of the Lord, and made a covenant with them: and taking an oath of them in the house of the Lord, shewed them the king’s son:
Katika mwaka wa saba, Yehoyada alituma ujumbe na kuleta maamiri jeshi mamia wa Wakari na wa walinzi, na kuwaleta kwake mwenyewe, ndani ya nyumba ya Yahwe. Akafanya agano pamoja nao, na kuwaapisha kiapo katika nyumba ya Yahwe. Kisha akawaonyesha mtoto wa mfalme.
5 And he commanded them, saying: This is the thing that you must do:
Akawaamuru, akisema, “Hivi ndivyo mnavyotakiwa kufanya. Theluthi yenu mtakaokuja kwenye Sabato mtakuwa mkiiangalia nyumba ya mfalme,
6 Let a third part of you go in on the sabbath, and keep the watch of the king’s house. And let a third part be at the gate of Sur: and let a third part be at the gate behind the dwelling of the shieldbearers: and you shall keep the watch of the house of Messa.
na theluthi mtakuwa langoni mwa Suri, na theluthi langoni nyuma ya walinzi.”
7 But let two parts of you, all that go forth on the sabbath, keep the watch of the house of the Lord about the king.
Makundi mengine mawili ambayo hayatumikii Sabato, Mtayalinda juu ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya mfalme.
8 And you shall compass him round about, having weapons in your hands: and if any man shall enter the precinct of the temple, let him be slain: and you shall be with the king coming in and going out.
Ni lazima mumzunguke mfalme, kila mmoja na silaha zake kwenye mkono wake. Yeyote aingiaye ndani ya safu, auwawe. Lazima mkae pamoja na mfalme kila atokapo na kila aingiapo.
9 And the centurions did according to all things that Joiada the priest had commanded them: and taking every one their men, that went in on the sabbath, with them that went out on the sabbath, came to Joiada the priest.
Hivyo mamia ya maamri jeshi wakatii kila kitu Yehoyada kuhani alichokiamuru. Kila mmoja akachukua watu wake, wale ambao walitakiwa kuja kutumika siku ya hiyo Sabato, na wale ambao wataacha kuitumika kwenye hiyo Sabato; ndipo wakaja kwa Yehoyada kuhani.
10 And he gave them the spears, and the arms of king David, which were in the house of the Lord.
Kisha Yehoyada yule kuhani akawapa mikuki na ngao mamia wa maamri jeshi ambayo ilikuwa mali ya mfalme Daudi ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe.
11 And they stood having every one their weapons in their hands, from the right side of the temple, unto the left side of the altar, and of the temple, about the king.
Basi walinzi wakasimama, kila mtu na silaha kwenye mkono wake, kutoka upande wa kuume wa hekalu, kwenda upande wa kushoto, karibu na madhabahu ya hekelu, wakimzunguka mfalme.
12 And he brought forth the king’s son, and put the diadem upon him, and the testimony: and they made him king, and anointed him: and clapping their hands. they said, God save the king.
Kisha Yehoyada akamleta nje mtoto wa mfalme Yoashi, na kumvalisha taji la kifalme, na kumpatia mikataba ya agano. Kisha wakamfanya mfalme na kummiminia mafuta. Wakapiga makofi wakisema, “Mfalme na aishi!”
13 And Athalia heard the noise of the people running: and going in to the people into the temple of the Lord,
Wakati Athalia aliposikia sauti za walinzi na za watu, alikuja kwa wale watu kwenye nyumba ya Yahwe.
14 She saw the king standing upon a tribunal, as the manner was, and the singers, and the trumpets near him, and all the people of the land rejoicing, and sounding the trumpets: and she rent her garments, and cried: A conspiracy, a conspiracy.
Akatazama, na, kisha, yule mfalme alikuwa amesimama kwenye nguzo, kama ilivyokuwa desturi, na manahodha na wapiga mabaragumu walikuwa karibu na mfalme. Watu wote wa nchi hiyo walikuwa wakifurahi na kupiga matarumbeta. Kisha Athalia akachana mavazi yake kwa hasira na kupiga kelele, “Uhaini! Uhaini!”
15 But Joiada commended the centurions that were over the army, and said to them: Have her forth without the precinct of the temple, and whosoever shall follow her, let him be slain with the sword. For the priest had said: Let her not be slain in the temple of the Lord.
Ndipo Yehoyada yule kuhani akawaagiza maamri jeshi wa mamia ambao waliokuwa juu ya jeshi, akisema, “Mtoeni kwenye safu.” Atakayemfuata, muueni kwa upanga.” Kwa kuwa kuhani alisema, “Msimwache auawe kwenye nyumba ya Yahwe.”
16 And they laid hands on her: and thrust her out by the way by which the horses go in, by the palace, and she was slain there.
Hivyo wakamtwaa kadiri walivyokuwa wakiikaribia hiyo sehemu iliyokuwa na farasi wakaingia chini, na akauawa huko.
17 And Joiada made a covenant between the Lord, and the king, and the people, that they should be the people of the Lord, and between the king and the people.
Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yahwe na mfalme na watu, ambao wangekuwa watu wa Yahwe, na pia kati ya mfalme na watu.
18 And all the people of the land went into the temple of Baal, and broke down his altars, and his images they broke in pieces thoroughly: they slew also Mathan the priest of Baal before the altar. And the priest set guards in the house of the Lord.
Basi watu wote wa nchi wakaenda kwenye nyumba ya Baali na kuingusha chini. Wakaangusha madhabahu ya Baali na sanamu zake wakazivunja vipande vipande, na kumuua Matani, mfalme wa Baali, mbele ya haya madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawachagua walinzi juu ya hekalu la Yahwe.
19 And he took the centurions, and the bands of the Cerethi and the Phelethi, and all the people of the land, and they brought the king from the house of the Lord: and they came by the way of the gate of the shieldbearers into the palace. and he sat on the throne of the kings.
Yehoyada akawachukua maamiri jeshi wa mamia, Wakari, walinzi, na watu wote wa nchi, na kwa pamoja wakamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe na wakaenda kwenye nyumba ya mfalme, wakaingia kwa njia ya lango la walinzi. Yoashi akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi cha mfalme.
20 And all the people of the land rejoiced, and the city was quiet: but Athalia was slain with the sword in the king’s house.
Hivyo watu wote wa nchi wakamsifu, na nchi ilikuwa kimya baada ya Athalia kuuawa kwa upanga kwenye nyumba ya mfalme.
21 Now Joas was seven years old, when he began to reign.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba tangu alipoanza kutawala.