< 1 Samuel 31 >
1 And the Philistines fought against Israel, and the men of Israel fled from before the Philistines, and fell down slain in mount Gelboe.
Basi Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli. Waisraeli wakakimbia mbele ya Wafilisti na wakaanguka chini wakafa katika mlima wa Gilboa.
2 And the Philistines fell upon Saul, and upon his sons, and they slew Jonathan, and Abinadab and Melchisua the sons of Saul.
Wafilisti wakamwandama Sauli na wanawe kwa karibu. Wakawaua wanawe Yonathani, Abinadabu, and Malkishua.
3 And the whole weight of the battle was turned upon Saul: and the archers overtook him, and he was grievously wounded by the archers.
Vita vikamwelemea Sauli, na wapiga upinde wakampata. Akapata maumivu makali kwa sababu yao.
4 Then Saul said to his armourbearer: Draw thy sword, and kill me: lest these uncircumcised come, and slay me, and mock at me. And his armourbearer would not: for he was struck with exceeding great fear. Then Saul took his sword, and fell upon it.
Kisha Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Chomoa upanga wako unichome nao. Vinginevyo, hawa wasiotahiriwa watakuja na kuninyanyasa.” Lakini mbeba silaha wake hakukubali, kwa kuwa aliogopa sana. Hivyo Sauli alichukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
5 And when his armourbearer saw this, to wit, that Saul was dead, he also fell upon his sword and died with him.
Yule mbeba silaha akaona kwamba Sauli amekufa, yeye naye vivyo hivyo akauangukia upanga wake akafa pamoja naye.
6 So Saul died, and his three sons, and his armourbearer, and all his men that same day together.
Kwa hiyo Sauli alikufa, wanawe watatu, na mbeba silaha wake - watu hawa wote walikufa pamoja siku iyo hiyo.
7 And the men of Israel, that were beyond the valley, and beyond the Jordan, seeing that the Israelites were fled, and that Saul was dead, and his sons, forsook their cities, and fled: and the Philistines came, and dwelt there.
Watu wa Israeli waliokuwa upande mwingine wa bonde, na hao waliokuwa ng'ambo ya Yordani, walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliiacha miji yao na kukimbia, nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
8 And on the morrow the Philistines came to strip the slain, and they found Saul and his three sons lying in mount Gelboe.
IKawa katika siku iliyofuata, Wafilisti wakafika kuchukua nyara za waliokufa, ndipo wakamuona Sauli na wanawe watatu wameanguka juu ya mlima wa Gilboa.
9 And they cut off Saul’s head, and stripped him of his armour, and sent into the land of the Philistines round about, to publish it in the temples of their idols, and among their people.
Nao wakakata kichwa chake na kuondoa silaha zake, na wakawatuma wajumbe kwenda pande zote katika nchi ya Wafilisti kutangaza habari hizo katika mahekalu yao ya sanamu na kwa watu.
10 And they put his armour in the temple of Astaroth, but his body they hung on the wall of Bethsan.
Wakaziweka silaha zake katika hekalu la Ashtorethi, nao wakakitundika kiwiliwili chake kwenye ukuta wa mji wa Bethi Shani.
11 Now when the inhabitants of Jabes Galaad had heard all that the Philistines had done to Saul,
Na wenyeji wa Yabeshi Gileadi waliposikia kile Wafilisti walichomfanyia Sauli,
12 All the most valiant men arose, and walked all the night, and took the body of Saul, and the bodies of his sons, from the wall of Bethsan: and they came to Jabes Galaad, and burnt them there:
wapiganaji wote wakainuka na kwenda usiku wote na wakauondoa mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka ukuta wa Bethi Shani. Nao wakaenda Yabeshi na wakaichoma moto hiyo miili huko.
13 And they took their bones and buried them in the wood of Jabes: and fasted seven days.
Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, na wakafunga siku saba.