< 1 Samuel 14 >
1 Now it came to pass one day that Jonathan the son of Saul said to the young man that bore his armour: Come, and let us go over to the garrison of the Philistines, which is on the other side of yonder place. But he told not this to his father.
Siku moja Yonathani mwana wa Sauli akamwambia kijana mbeba silaha wake, akasema, “Njoo, tuwavukie Wafilisti kwenye doria upande ule mwingine.” Lakini hakumwambia baba yake.
2 And Saul abode in the uttermost part of Gabaa under the pomegranate tree, which was in Magron: and the people with him were about six hundred men.
Sauli alikuwa akikaa kwenye viunga vya Gibea chini ya mkomamanga huko Migroni. Alikuwa pamoja na watu kama 600,
3 And Achias the son of Achitob brother to Ichabod the son of Phinees, the son of Heli the priest of the Lord in Silo, wore the ephod. And the people knew not whither Jonathan was gone.
miongoni mwao alikuwepo Ahiya, ambaye alikuwa amevaa kisibau. Alikuwa mwana wa Ikabodi, nduguye Ahitubu mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa Bwana huko Shilo. Hakuna yeyote aliyekuwa na habari kwamba Yonathani alikuwa ameondoka.
4 Now there were between the ascents, by which Jonathan sought to go over to the garrison of the Philistines, rocks standing up on both sides, and steep cliffs like teeth on the one side, and on the other, the name of the one was Boses, and the name of the other was Sene:
Kila upande wa njia ambayo Yonathani alikusudia kupita ili kuvuka kufikia doria ya Wafilisti kulikuwepo na jabali; moja lilikuwa linaitwa Bosesi, na jingine Sene.
5 One rock stood out towards the north over against Machmas, and the other to the south over against Gabaa.
Jabali moja lilisimama kaskazini kuelekea Mikmashi na jingine upande wa kusini kuelekea Geba.
6 And Jonathan said to the young man that bore his armour: Come, let us go over to the garrison of these uncircumcised, it may be the Lord will do for us, because it is easy for the Lord to save either by many, or by few.
Yonathani akamwambia kijana wake mbeba silaha, “Njoo, tuvukie doria ya wale jamaa wasiotahiriwa. Huenda Bwana atatenda kwa ajili yetu. Hakuna chochote kitakachoweza kumzuia Bwana kuokoa, kwamba ni kwa wingi au kwa uchache.”
7 And his armourbearer said to him: Do all that pleaseth thy mind: go whither thou wilt, and I will be with thee wheresoever thou hast a mind.
Mbeba silaha wake akamwambia, “Fanya yale yote uliyo nayo katika moyo wako. Songa mbele; moyo wangu na roho yangu viko pamoja nawe.”
8 And Jonathan said: Behold we will go over to these men. And when we shall be seen by them,
Yonathani akasema, “Basi njoo; tutavuka kuwaelekea hao watu na kuacha watuone.
9 If they shall speak thus to us: Stay till we come to you: let us stand still in our place, and not go up to them.
Kama wakituambia, ‘Subirini hapo mpaka tuje kwenu,’ tutakaa pale tulipo na hatutakwea kwao.
10 But if they shall say: Come up to us: let us go up, because the Lord hath delivered them into our hands, this shall be a sign unto us.
Lakini kama watasema, ‘Pandeni mje kwetu,’ tutakwea, kwa sababu hiyo itakuwa ishara yetu kwamba Bwana amewatia mikononi mwetu.”
11 So both of them discovered themselves to the garrison of the Philistines: and the Philistines said: Behold the Hebrews come forth out of the holes wherein they were hid.
Basi wote wawili wakajionyesha kwa doria ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Tazama! Waebrania wanatambaa toka mashimoni walimokuwa wamejificha.”
12 And the men of the garrison spoke to Jonathan, and to his armourbearer, and said: Come up to us, and we will shew you a thing. And Jonathan said to his armourbearer: Let us go up, follow me: for the Lord hath delivered them into the hands of Israel.
Watu wa kwenye doria wakawapigia kelele Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njooni, pandeni kwetu nasi tutawakomesha.” Basi Yonathani akamwambia mbeba silaha wake, “Panda nyuma yangu; Bwana amewatia mikononi mwa Israeli.”
13 And Jonathan went up creeping on his hands and feet, and his armourbearer after him. And some fell before Jonathan, others his armourbearer slew as he followed him.
Yonathani akapanda juu, akitumia mikono yake na miguu, pamoja na mbeba silaha wake papo hapo nyuma yake. Wafilisti wakaanguka mbele ya Yonathani, naye mbeba silaha wake akamfuata akiwaua nyuma yake.
14 And the first slaughter which Jonathan and his armourbearer made, was of about twenty men, within half an acre of land, which a yoke of oxen is wont to plough in a day.
Katika hilo shambulio la kwanza, Yonathani na mbeba silaha wake waliua kama watu ishirini kwenye eneo kama la nusu eka.
15 And there was a miracle in the camp, through the fields: yea and all the people of their garrison, who had gone out to plunder, were amazed, and the earth trembled: and it happened as a miracle from God.
Kisha fadhaa ikawapata jeshi lote, wale waliokuwa kambini na shambani, wale waliokuwa katika doria na makundi ya washambuliaji, nayo nchi ilitetemeka. Ilikuwa ni hofu ya ghafula iliyotumwa na Mungu.
16 And the watchmen of Saul, who were in Gabaa of Benjamin looked, and behold a multitude overthrown, and fleeing this way and that.
Wapelelezi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona jeshi likitokomea pande zote.
17 And Saul said to the people that were with him: Look, and see who is gone from us. And when they had sought, it was found that Jonathan and his armourbearer were not there.
Ndipo Sauli akawaambia watu wale waliokuwa pamoja naye, “Kagueni jeshi mkaone ni nani ameondoka katikati yetu.” Walipokagua, akawa ni Yonathani na mbeba silaha wake ambao hawakuwepo.
18 And Saul said to Achias: Bring the ark of the Lord. (For the ark of God was there that day with the children of Israel.)
Sauli akamwambia Ahiya, “Leta Sanduku la Mungu.” (Wakati huo lilikuwa kwa Waisraeli.)
19 And while Saul spoke to the priest, there arose a great uproar in the camp of the Philistines: and it increased by degrees, and was heard more clearly. And Saul said to the priest: Draw in thy hand.
Wakati Sauli alipokuwa akisema na kuhani, makelele katika kambi ya Wafilisti yakaongezeka zaidi na zaidi. Hivyo Sauli akamwambia kuhani, “Rudisha mkono wako.”
20 Then Saul and all the people that were with him, shouted together, and they came to the place of the fight: and behold every man’s sword was turned upon his neighbour, and there was a very great slaughter.
Kisha Sauli na watu wake wote wakakusanyika na kwenda vitani. Wakawakuta Wafilisti wakiwa wamechanganyikiwa kabisa, wakitiana panga kila mmoja na wenzake.
21 Moreover the Hebrews that had been with the Philistines yesterday and the day before, and went up with them into the camp, returned to be with the Israelites, who were with Saul and Jonathan.
Wale Waebrania ambao walishakuwa pamoja na Wafilisti, na waliokuwa wamepanda pamoja nao katika kambi zao, wakaenda upande wa Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 And all the Israelites that had hid themselves in mount Ephraim, hearing that the Philistines fled, joined themselves with their countrymen in the fight. And there were with Saul about ten thousand men.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika nchi ya milima ya Efraimu waliposikia kuwa Wafilisti wamekimbia, wakajiunga vitani na kuwafuata kwa bidii.
23 And the Lord saved Israel that day. And the fight went on as far as Bethaven.
Hivyo Bwana akawaokoa Waisraeli siku ile, navyo vita vilienea hadi kupita Beth-Aveni.
24 And the men of Israel were joined together that day; and Saul adjured the people, saying: Cursed be the man that shall eat food till evening, till I be revenged of my enemies. So none of the people tasted any food:
Basi watu wa Israeli walikuwa katika dhiki siku ile, kwa sababu Sauli alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, akisema, “Alaaniwe mtu yeyote ambaye atakula chakula kabla ya jioni, kabla sijalipiza kisasi juu ya adui zangu!” Kwa hiyo hakuna mtu yeyote katika jeshi aliyeonja chakula.
25 And all the common people came into a forest, in which there was honey upon the ground.
Jeshi lote liliingia mwituni, na huko kulikuwepo na asali ardhini.
26 And when the people came into the forest, behold the honey dropped, but no man put his hand to his mouth. For the people feared the oath.
Walipoingia mwituni, wakaona asali ikitiririka, hata hivyo hakuna mtu yeyote aliyetia mkono wake kinywani, kwa sababu waliogopa kiapo.
27 But Jonathan had not heard when his father adjured the people: and he put forth the end of the rod, which he had in his hand, and dipt it in a honeycomb: and he carried his hand to his mouth, and his eyes were enlightened.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kuwa baba yake alikuwa amewafunga watu kwa kiapo, hivyo akainyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya katika sega la asali. Akainua mkono wake na kuutia kinywani mwake, nayo macho yake yakawa maangavu.
28 And one of the people answering, said: Thy father hath bound the people with an oath, saying: Cursed be the man that shall eat any food this day. (And the people were faint.)
Kisha mmoja wa askari wake akamwambia, “Baba yako alilifunga jeshi kwa kiapo kikali, akisema, ‘Alaaniwe mtu yeyote alaye chakula leo!’ Ndiyo sababu watu wanalegea.”
29 And Jonathan said: My father hath troubled the land: you have seen yourselves that my eyes are enlightened, because I tasted a little of this honey:
Yonathani akasema, “Baba yangu ameitaabisha nchi. Ona jinsi nilivyopata nguvu mpya nilipoonja asali hii kidogo.
30 How much more if the people had eaten of the prey of their enemies, which they found? had there not been made a greater slaughter among the Philistines?
Ingekuwa bora zaidi mara ngapi kama watu wangalikula leo baadhi ya nyara walizoteka kutoka kwa adui zao. Je, mauaji ya Wafilisti yasingekuwa makubwa zaidi?”
31 So they smote that day the Philistines from Machmas to Ailon. And the people were wearied exceedingly.
Siku ile baada ya Waisraeli kuwaua Wafilisti kutoka Mikmashi mpaka Aiyaloni, walikuwa wamechoka.
32 And falling upon the spoils, they took sheep, and oxen, and calves, and slew them on the ground: and the people ate them with the blood.
Watu wakarukia zile nyara, wakichukua kondoo, ngʼombe na ndama, wakawachinja hapo juu ya nchi na kuwala, pamoja na damu.
33 And they told Saul that the people had sinned against the Lord, eating with the blood. And he said: You have transgressed: roll here to me now a great stone.
Kisha mtu mmoja akamwambia Sauli, “Tazama, watu wanatenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama yenye damu.” Akasema, “Mmevunja uaminifu. Livingirisheni jiwe kubwa hapa mara moja.”
34 And Saul said: Disperse yourselves among the people, and tell them to bring me every man his ox and his ram, and slay them upon this stone, and eat, and you shall not sin against the Lord in eating with the blood. So all the people brought every man his ox with him till the night: and slew them there.
Kisha Sauli akasema, “Nendeni miongoni mwa watu, mwaambie, ‘Kila mmoja wenu aniletee ngʼombe wake na kondoo, mwachinjie hapa na mle. Msitende dhambi dhidi ya Bwana kwa kula nyama ikiwa na damu ndani yake.’” Hivyo kila mmoja akaleta ngʼombe wake jioni ile na kumchinja hapo.
35 And Saul built an altar to the Lord and he then first began to build an altar to the Lord.
Ndipo Sauli akamjengea Bwana madhabahu, na ndiyo ilivyokuwa mara yake ya kwanza kujenga madhabahu.
36 And Saul said: Let us fall upon the Philistines by night, and destroy them till the morning light, and let us not leave a man of them. And the people said: Do all that seemeth good in thy eyes. And the priest said: Let us draw near hither unto God.
Sauli akasema, “Tuteremke tufuatie Wafilisti usiku na kuwateka nyara mpaka mapambazuko, nasi tusiache hata mmoja wao hai.” Wakajibu, “Fanya lolote lile uonalo jema zaidi kwako.” Lakini kuhani akasema, “Tuulize kwa Mungu mahali hapa.”
37 And Saul consulted the Lord: Shall I pursue after the Philistines? wilt thou deliver them into the hands of Israel? And he answered him not that day.
Basi Sauli akamuuliza Mungu, akisema, “Je, niteremke kuwafuatia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwa Israeli?” Lakini Mungu hakumjibu siku ile.
38 And Saul said: Bring hither all the corners of the people: and know, and see by whom this sin hath happened today.
Kwa hiyo Sauli akasema, “Njooni hapa, ninyi nyote ambao ni viongozi wa jeshi, na tutafute ni dhambi gani imefanywa leo.
39 As the Lord liveth who is the saviour of Israel, if it was done by Jonathan my son, he shall surely die. In this none of the people gainsaid him.
Kwa hakika kama Bwana aiokoaye Israeli aishivyo, hata kama itakuwa juu ya mwana wangu Yonathani, ni lazima afe.” Lakini hakuna mtu yeyote aliyesema neno.
40 And he said to all Israel: Be you on one side, and I with Jonathan my son will be on the other side. And the people answered Saul: Do what seemeth good in thy eyes.
Kisha Sauli akawaambia Waisraeli wote, “Ninyi simameni huko; mimi na mwanangu Yonathani tutasimama hapa.” Watu wakajibu, “Fanya lile unaloona jema zaidi kwako.”
41 And Saul said to the Lord: O Lord God of Israel, give a sign, by which we may know, what the meaning is, that thou answerest not thy servant today. If this iniquity be in me, or in my son Jonathan, give a proof: or if this iniquity be in thy people, give holiness. And Jonathan and Saul were taken, and the people escaped.
Kisha Sauli akamwomba Bwana, Mungu wa Israeli, akisema, “Nipe jibu lililo sawa.” Yonathani na Sauli wakatolewa kwa kura, nao watu wakawa salama.
42 And Saul said: Cast lots between me, and Jonathan my son. And Jonathan was taken.
Sauli akasema, “Pigeni kura kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kura ikamwangukia Yonathani.
43 And Saul said to Jonathan: Tell me what thou hast done. And Jonathan told him, and said: I did but taste a little honey with the end of the rod, which was in my hand, and behold I must die.
Basi Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie ni nini ulichokifanya.” Hivyo Yonathani akamwambia, “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo yangu. Je, sasa ni lazima nife?”
44 And Saul said: May God do so and so to me, and add still more: for dying thou shalt die, O Jonathan.
Sauli akasema, “Mungu na anishughulikie kwa ukali zaidi kama wewe Yonathani hutakufa.”
45 And the people said to Saul: Shall Jonathan then die, who hath wrought this great salvation in Israel? This must not be. As the Lord liveth, there shall not one hair of his head fall to the ground, for he hath wrought with God this day. So the people delivered Jonathan, that he should not die.
Lakini watu wakamwambia Sauli, “Je, Yonathani atakufa, yeye ambaye ameleta wokovu huu mkubwa Israeli? Hasha! Hakika kama Bwana aishivyo, hakuna hata unywele wa kichwa chake utakaoanguka juu ya ardhi, kwa kuwa alifanya jambo hili leo kwa msaada wa Mungu.” Basi watu wakamwokoa Yonathani, wala hakuuawa.
46 And Saul went back, and did not pursue after the Philistines: and the Philistines went to their own places.
Kisha Sauli akaacha kuwafuata Wafilisti, nao wakajiondoa na kurudi katika nchi yao.
47 And Saul having his kingdom established over Israel, fought against all his enemies round about, against Moab, and against the children of Ammon, and Edom, and the kings of Soba, and the Philistines; and whithersoever he turned himself, he overcame.
Baada ya Sauli kujitwalia utawala katika Israeli, alipigana dhidi ya adui zake kila upande: Moabu, Waamoni, Edomu, wafalme wa Soba, na Wafilisti. Popote alipogeukia, aliwashinda.
48 And gathering together an army, he defeated Amalec, and delivered Israel from the hand of them that spoiled them.
Akapigana kishujaa na kuwashinda Waamaleki, akiikomboa Israeli kutoka mikono ya wale waliokuwa wamewateka nyara.
49 And the sons of Saul, were Jonathan, and Jessui, and Melchisua: and the names of his two daughters, the name of the firstborn was Merob, and the name of the younger Michol.
Wana wa Sauli walikuwa Yonathani, Ishvi na Malki-Shua. Jina la binti yake mkubwa lilikuwa Merabu, naye mdogo aliitwa Mikali.
50 And the name of Saul’s wife, was Achinoam the daughter of Achimaas; and the name of the captain of his army was Abner, the son of Ner, the cousin german of Saul.
Jina la mkewe Sauli aliitwa Ahinoamu binti wa Ahimaasi. Jina la jemadari wa jeshi la Sauli aliitwa Abneri mwana wa Neri, naye Neri alikuwa babaye mdogo Sauli.
51 For Cis was the father of Saul, and Ner the father of Abner, was son of Abiel.
Babaye Sauli yaani, Kishi na Neri baba yake Abneri walikuwa wana wa Abieli.
52 And there was a great war against the Philistines all the days of Saul. For whomsoever Saul saw to be a valiant man, and fit for war, he took him to himself.
Siku zote za utawala wa Sauli zilikuwa za vita vikali dhidi ya Wafilisti, na wakati wowote Sauli alimwona mtu mwenye nguvu au shujaa, alimchukua kwa utumishi wake.