< 1 Kings 12 >

1 And Roboam went to Sichem: for thither were all Israel come together to make him king.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 But Jeroboam the son of Nabat, who was yet in Egypt, a fugitive from the face of king Solomon, hearing of his death, returned out of Egypt.
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 And they sent and called him: and Jeroboam came, and all the multitude of Israel, and they spoke to Roboam, saying:
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 Thy father laid a grievous yoke upon us: now therefore do thou take off a little of the grievous service of thy father, and of his most heavy yoke, which he put upon us, and we will serve thee.
“Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 And he said to them: Go till the third day, and come to me again. And when the people was gone,
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 King Roboam took counsel with the old men, that stood before Solomon his father while he yet lived, and he said: What counsel do you give me, that I may answer this people?
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 They said to him: If thou wilt yield to this people today, and condescend to them, and grant their petition, and wilt speak gentle words to them, they will be thy servants always.
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 But he left the counsel of the old men, which they had given him, and consulted with the young men, that had been brought up with him, and stood before him.
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 And he said to them: What counsel do you give me, that I may answer this people, who have said to me: Make the yoke which thy father put upon us lighter?
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 And the young men that had been brought up with him, said: Thus shalt thou speak to this people, who have spoken to thee, saying: Thy father made our yoke heavy, do thou ease us. Thou shalt say to them: My little finger is thicker than the back of my father.
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 And now my father put a, heavy yoke upon you, but I will add to your yoke: my father beat you with whips, but I will beat you with scorpions.
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 So Jeroboam and all the people came to Roboam the third day, as the king had appointed, saying: Come to me again the third day.
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 And the king answered the people roughly, leaving the counsel of the old men, which they had given him,
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 And he spoke to them according to the counsel of the young men, saying: My father made your yoke heavy, but I will add to your yoke: my father beat you with whips, but I will beat you with scorpions.
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 And the king condescended not to the people: for the Lord was turned away from him, to make good his word, which he had spoken in the hand of Ahias the Silonite, to Jeroboam the son of Nabat.
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 Then the people seeing that the king would not hearken to them, answered him, saying: What portion have we in David? or what inheritance in the son of Isai? Go home to thy dwellings, O Israel, now David look to thy own house. So Israel departed to their dwellings.
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 But as for all the children of Israel that dwelt in the cities of Juda, Roboam reigned over them.
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Then king Roboam sent Aduram, who was over the tribute: and all Israel stoned him, and he died. Wherefore king Roboam made haste to get him up into his chariot, and he fled to Jerusalem:
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 And Israel revolted from the house of David, unto this day.
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
20 And it came to pass when all Israel heard that Jeroboam was come again, that they gathered an assembly, and sent and called him, and made him king over all Israel, and there was none that followed the house of David but the tribe of Juda only.
Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
21 And Roboam came to Jerusalem, and gathered together all the house of Juda, and the tribe of Benjamin, a hundred four-score thousand chosen men for war, to fight against the house of Israel and to bring the kingdom again under Roboam the son of Solomon.
Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
22 But the word of the Lord came to Semeias the man of God, saying:
Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
23 Speak to Roboam the son of Solomon, the king of Juda, and to all the house of Juda, and Benjamin, and the rest of the people, saying:
“Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
24 Thus saith the Lord: You shall not go up nor fight against your brethren the children of Israel: let every man return to his house, for this thing is from me. They hearkened to the word of the Lord, and returned from their journey, as the Lord had commanded them.
‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
25 And Jeroboam built Sichem in mount Ephraim, and dwelt there, and going out from thence he built Phanuel.
Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
26 And Jeroboam said in his heart: Now shall the kingdom return to the house of David,
Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
27 If this people go up to offer sacrifices in the house of the Lord at Jerusalem: and the heart of this people will turn to their lord Roboam the king of Juda, and they will kill me, and return to him.
Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
28 And finding out a device he made two golden calves, and said to them: Go ye up no more to Jerusalem: Behold thy gods, O Israel, who brought thee out of the land of Egypt.
Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
29 And he set the one in Bethel, and the other in Dan:
Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
30 And this thing became an occasion of sin: for the people went to adore the calf as far as Dan.
Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
31 And he made temples in the high places, and priests of the lowest of the people, who were not of the sons of Levi.
Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
32 And he appointed a feast in the eighth month, on the fifteenth day of the month, after the manner of the feast that was celebrated in Juda. And going up to the altar, he did in like manner in Bethel, to sacrifice to the calves, which he had made: and he placed in Bethel priests of the high places, which he had made.
Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
33 And he went up to the altar, which he had built in Bethel, on the fifteenth day of the eighth month, which he had devised of his own heart: and he ordained a feast to the children of Israel, and went upon the altar to burn incense.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.

< 1 Kings 12 >