< 1 Chronicles 27 >

1 Now the children of Israel according to their number, the heads of families, captains of thousands and of hundreds, and officers, that served the king according to their companies, who came in and went out every month in the year, under every chief were four and twenty thousand.
Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
2 Over the first company the first month Jesboam, the son of Zabdiel was chief, and under him were four and twenty thousand.
Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
3 Of the sons of Phares, the chief of all the captains in the host in the first month.
Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 The company of the second month was under Dudia, an Ahohite, and after him was another named Macelloth, who commanded a part of the army of four and twenty thousand.
Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
5 And the captain of the third company for the third month, was Banaias the son of Joiada the priest: and in his division were four and twenty thousand.
Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
6 This is that Banaias the most valiant among the thirty, and above the thirty. And Amizabad his son commanded his company.
Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
7 The fourth, for the fourth month, was Asahel the brother of Joab, and Zabadias his son after him: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
8 The fifth captain for the fifth month, was Samaoth a Jezerite: and his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
9 The sixth, for the sixth month, was Hira the son of Acces a Thecuite: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
10 The seventh, for the seventh month, was Helles a Phallonite of the sons of Ephraim: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
11 The eighth, for the eighth month, was Sobochai a Husathite of the race of Zarahi: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
12 The ninth, for the ninth month, was Abiezer an Anathothite of the sons of Jemini, and in His company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
13 The tenth, for the tenth month, was Marai, who was a Netophathite of the race of Zarai: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
14 The eleventh, for the eleventh month, was Banaias, a Pharathonite of the sons of Ephraim: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
15 The twelfth, for the twelfth month, was Holdai a Netophathite, of the race of Gothoniel: and in his company were four and twenty thousand.
Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
16 Now the chiefs over the tribes of Israel were these: over the Rubenites, Eliezer the son of Zechri was ruler: over the Simeonites, Saphatias the son of Maacha:
Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
17 Over the Levites, Hasabias the son of Camuel: over the Aaronites, Sadoc:
Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
18 Over Juda, Eliu the brother of David: over Issachar, Amri the son of Michael:
Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
19 Over the Zabulonites, Jesmaias the son of Adias: over the Nephtalites, Jerimoth the son of Ozriel:
Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
20 Over the sons of Ephraim, Osee the: son of Ozaziu: over the half tribe of Manasses, Joel the son of Phadaia:
Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
21 And over the half tribe of Manasses: in Galaad, Jaddo the son of Zacharias: and over Benjamin, Jasiel the son of Abner.
Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
22 And over Dan, Ezrihel the son of Jeroham: these were the princes of the children of Israel.
Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
23 But David would not number them from twenty years old and under: because the Lord had said that he would multiply Israel like the stars of heaven.
Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
24 Joab the son of Sarvia began to number, but he finished not: because upon this there fell wrath upon Israel: and therefore the number of them that were numbered, was not registered in the chronicles of king David.
Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
25 And over the king’s treasures was Azmoth the son of Adiel: and over those stores which were in the cities, and is the villages, and in the castles, was Jonathan the son of Ozias.
Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
26 And over the tillage, and the husbandmen, who tilled the ground, was Ezri the son of Chelub:
Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
27 And over the dressers of the vineyards, was Semeias a Romathite: and over the wine cellars, Zabdias an Aphonite.
Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
28 And over the oliveyards and the fig groves, which were in the plains, was Balanam a Gederite: and over the oil cellars, Joas.
Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
29 And over the herds that fed in Saron, was Setrai a Saronite: and over the. oxen in the valleys, Saphat the son of Adli:
Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
30 And over the camels, Ubil an Ishmahelite: and over the asses, Jadias a Meronathite:
Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
31 And over the sheep Jazia an Agarene. All these were the rulers of the substance of king David.
Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
32 And Jonathan David’s uncle, a counsellor, a wise and learned man: he and Jahiel the son of Hachamoni were with the king’s sons.
Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
33 And Achitophel was the king’s counsellor, and Chusai the Arachite, the king’s friend.
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
34 And after Achitophel was Joiada the son of Banaias, and Abiathar. And the general of the king’s army was Joab.
Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.

< 1 Chronicles 27 >