< 1 Chronicles 15 >

1 He made also houses for himself in the city of David: and built a place for the ark of God, and pitched a tabernacle for it.
Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
2 Then David said: No one ought to carry the ark of God, but the Levites, whom the Lord hath chosen to carry it, and to minister unto himself for ever.
Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
3 And he gathered all Israel together into Jerusalem, that the ark of God might be brought into its place, which he had prepared for it.
Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
4 And the sons of Aaron also, and the Levites.
Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
5 Of the children of Caath, Uriel was the chief, and his brethren a hundred and twenty.
Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
6 Of the sons of Merari, Asaia the chief, and his brethren two hundred and twenty.
Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
7 Of the sons of Gersom, Joel the chief, and his brethren a hundred and thirty.
Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
8 Of the sons of Elisaphan, Semeias the chief: and his brethren two hundred.
Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
9 Of the sons of Hebron, Eliel the chief: and his brethren eighty.
Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
10 Of the sons of Oziel, Aminadab the chief: and his brethren a hundred and twelve.
Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
11 And David called Sadoc, and Abiathar the priests, and the Levites, Uriel, Asaia, Joel, Semeia, Eliel, and Aminadab:
Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
12 And he said to them: You that are the heads of the Levitical families, be sanctified with your brethren, and brine the ark of the Lord the God of Israel to the place, which is prepared for it:
Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
13 Lest as the Lord at first struck us, because you were not present, the same should now also come to pass, by our doing some thing against the law.
Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
14 So the priests and the Levites were sanctified, to carry the ark of the Lord the God of Israel.
Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
15 And the sons of Levi took the ark of God as Moses had commanded, according to the word of the Lord, upon their shoulders, with the staves.
Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
16 And David spoke to the chiefs of the Levites, to appoint some of their brethren to be singers with musical instruments, to wit, on psalteries, and harps, and cymbals, that the joyful noise might resound on high.
Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
17 And they appointed Levites, Hemam the son of Joel, and of his brethren Asaph the son of Barachias: and of the sons of Merari, their brethren: Ethan the son of Casaia.
Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
18 And with them their brethren: in the second rank, Zacharias, and Ben, and Jaziel, and Semiramoth, and Jahiel, and Ani, and Eliab, and Banaias, and Maasias, and Mathathias, and Eliphalu, and Macenias, and Obededom, and Jehiel, the porters.
hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
19 Now the singers, Heman, Asaph, and Ethan, sounded with cymbals of brass.
Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
20 And Zacharias, and Oziel, and Semiramoth, and Jehiel, and Ani, and Eliab, and Maasias, and Banaias, sung mysteries upon psalteries.
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
21 And Mathathias, and Eliphalu, and Macenias and Obededom, and Jehiel and Ozaziu, sung a song of victory for the octave upon harps.
na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
22 And Chonenias chief of the Levites, presided over the prophecy, to give out the tunes: for he was very skillful.
Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
23 And Barachias, and Elcana, were doorkeepers of the ark.
Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
24 And Sebenias, and Josaphat, and Nathanael, and Amasai, and Zacharias, and Banaias, and Eliezer the priests, sounded with trumpets, before the ark of God: and Obededom and Jehias were porters of the ark.
Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
25 So David and all the ancients of Israel, and the captains over thousands, went to bring the ark of the covenant of the Lord out of the house of Obededom with joy.
Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
26 And when God had helped the Levites who carried the ark of the covenant of the Lord, they offered in sacrifice seven oxen, and seven rams.
Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
27 And David was clothed with a robe of fine linen, and all the Levites that carried the ark, and the singing men, and Chonenias the ruler of the prophecy among the singers: and David also had on him an ephod of linen.
Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
28 And all Israel brought the ark of the covenant of the Lord with joyful shouting, and sounding with the sound of the comet, and with trumpets, and cymbals, and psalteries, and harps.
Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
29 And when the ark of the covenant of the Lord was come to the city of David, Michol the daughter of Saul looking out at a window, saw king David dancing and playing, and she despised him in her heart.
Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

< 1 Chronicles 15 >