< Ruth 4 >

1 And Boaz went up to the gate, and sat down there. And behold, he that had the right of redemption, of whom Boaz had spoken, came by. And he said, Thou, such a one, turn aside, sit down here. And he turned aside and sat down.
Ndipo Boazi akaenda kwenye lango la Bethelehemu na kukaa chini. Muda mfupi tu akaja ndugu wa karibu ambaye Boazi alimuongelea. Boazi akamwambia, “Rafiki yangu, njoo hapa na uketi. Kisha mtu huyo akaja na kuketi.
2 And he took ten men of the elders of the city, and said, Sit down here. And they sat down.
Ndipo Boazi akakusanya viongozi kumi wa mji na kusema, “Katini hapa.” Hivyo wakaketi.
3 And he said to him that had the right of redemption: Naomi, who is come back out of the country of Moab, sells the allotment that was our brother Elimelech's.
Boazi alimwambia yule jamaa wa karibu, “Naomi aliyerudi kutoka mji wa Moabu, anauza sehemu ya aridhi ambayo ilikuwa ni miliki ya kaka yetu Elimeleki.
4 And I thought I would apprise thee of it and say, Buy [it] in the presence of the inhabitants, and in the presence of the elders of my people. If thou wilt redeem [it], redeem; but if thou wilt not redeem, tell me, that I may know; for there is none to redeem besides thee; and I am after thee. And he said, I will redeem [it].
Nilifikiria kukujulisha na kukwambia, 'Inunue mbele ya hawa waliokaa hapa, na mbele ya viongozi wa watu wangu.' Ikiwa utapenda kuikomboa, ikomboe. Lakini ikiwa hauhitaji kuikomboa, uniambie, ili nijue, kwa kuwa hakuna mwingine wa kuikomboa isipokuwa wewe, na mimi ni mdogo wako.” Ndipo huyo mtu mwingine akasema, “Nitalikomboa.”
5 And Boaz said, On the day thou buyest the field of the hand of Naomi, thou must buy [it] also of Ruth the Moabitess, the wife of the dead, to raise up the name of the dead upon his inheritance.
Kisha Boazi akasema, “Ile siku utakayonunua shamba kutoka mkononi mwa Naomi, yakupasa pia kumchukua Ruth Mmoabu, mjane wa mtoto wa Elimeleki, ili kuliinua jina la marehemu kama urithi wake.”
6 And he that had the right of redemption said, I cannot redeem [it] for myself, lest I mar mine own inheritance. Redeem thou for thyself what I should redeem, for I cannot redeem [it].
Ndipo yule jamaa wa karibu akasema, “Mimi siwezi kuikomboa ardhi kwa ajili yangu bila kuleta athari kwenye urithi wangu binafsi. Nakupa wewe haki ya kuikomboa kwa ajili yako mwenyewe, kwa kuwa mimi sitoweza.”
7 Now this [was the custom] in former time in Israel concerning redemption and concerning exchange, to confirm the whole matter: a man drew off his sandal, and gave it to his neighbour, and this was the [mode of] attestation in Israel.
Hii ilikuwa ni desturi ya zamani ya Israeli kuhusu ukombozi na kubadilishana mazuri. Kudhibitisha mambo haya yote, mtu huyu alivua kiatu chake na kumpatia jirani yake; hii ilikuwa ni namna ya kufanya makubaliano ya kisheria katika Israeli.
8 And he that had the right of redemption said to Boaz, Buy for thyself; and he drew off his sandal.
Kwa hiyo huyu jamaa wa karibu akamwambia Boazi, “Inunue mwenyewe.” Kisha akavua kiatu chake.
9 And Boaz said to the elders and all the people, Ye are witnesses this day, that I have bought all that was Elimelech's, and all that was Chilion's and Mahlon's, of the hand of Naomi;
Ndipo Boazi akawaambia viongozi na watu wote, “Ninyi ni mashaidi kuwa nimenunua kila kilichokuwa cha Elimeleki na kila kilichokuwa na Kileoni na Mahilon kutoka kwenye mikono ya Naomi.
10 moreover Ruth the Moabitess, the wife of Mahlon, have I purchased to be my wife, to raise up the name of the dead upon his inheritance, that the name of the dead be not cut off from among his brethren and from the gate of his place: ye are witnesses this day.
Zaidi ya hayo kumhusu Ruth Mmoabu, mke wa Mahlon: nimempa kibali cha kuwa mke wangu, ili kuendeleza jina na urithi wa marehumu, ili kwamba jina lake lisipotee kati ya ndugu zake na lango la watu wake. Ninyi ni mashahidi leo.”
11 And all the people that were in the gate and the elders said, [We are] witnesses. Jehovah make the woman that cometh into thy house like Rachel and like Leah, which two did build the house of Israel; and acquire power in Ephratah, and make thyself a name in Bethlehem;
Watu wote na viongozi waliokuwa katika lango, walisema, “Tu mashahidi. Yahweh amfanye mwanamke huyu ambaye amekuja nyumbani kwako kama Raheli na Leya, ambao wawili hawa wameijenga nyumba ya Israeli. Na ubarikiwe katika Efrata na kuwa mashuhuri katika Bethelehem.
12 and let thy house become like the house of Pherez, whom Tamar bore to Judah, of the seed which Jehovah shall give thee of this young woman.
Na nyumba yako kama nyumba ya Peres, ambaye Tamari alimzalia yuda, kupitia uzao ambao Yahweh atakupatia pamoja na msichana huyu.”
13 And Boaz took Ruth, and she became his wife; and he went in unto her, and Jehovah gave her conception, and she bore a son.
Hivyo Boazi alimchukua Ruth, na akawa mke wake. Boazi alilala naye, na Yahweh alimruhusu kupata mimba, na alizaa mtoto wa kiume.
14 And the women said to Naomi, Blessed be Jehovah who hath not left thee this day without one that has the right of redemption, and may his name be famous in Israel!
Wanamke huyu akamwambia Naomi, “Yahweh abarikiwe, ambaye hajakuacha bila ndugu wa karibu, yaani mtoto huyu. Jina lake na liwe maarufu katika Israeli.
15 And he shall be to thee a restorer of thy life, and a nourisher of thine old age; for thy daughter-in-law who loves thee, who is better to thee than seven sons, has borne him.
Na awe kwako mrutubishaji wa maisha na mwenye ruzuku uzeeni mwako, kwa kuwa mtoto wako mkwe, ambaye anakupenda, ambaye ni bora kwako kuliko watoto wa kiume saba, amemzaa.
16 And Naomi took the child, and laid it in her bosom, and became nurse to it.
Kisha naomi akamchukua mtoto, akamlaza kifuani pake, na kumhudumia.
17 And the women [her] neighbours gave it a name, saying, There is a son born to Naomi. And they called his name Obed. He is the father of Jesse, the father of David.
Na majirani wa yule mwanamke, wakampa jina, wakisema, “Mtoto amezaliwa kwa Naomi.” Wakawita Obedi. Ambaye alikuja kuwa baba yake na Jese, ambaye alikuja kuwa baba yake na Daudi.
18 Now these are the generations of Pherez. Pherez begot Hezron,
Hiki kilikuwa ni kizazi cha Peresi: Peres alimzaa Hezroni,
19 and Hezron begot Ram, and Ram begot Amminadab,
Hezroni akamzaa Ram, Ram akamzaa Aminadabu,
20 and Amminadab begot Nahshon, and Nahshon begot Salmon,
Aminadabu akamzaa Nashon, Nashon akamzaa Salmon,
21 and Salmon begot Boaz, and Boaz begot Obed,
Salmon akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obed,
22 and Obed begot Jesse, and Jesse begot David.
Obedi akamzaa Jese, na Jese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >