< Psalms 81 >

1 To the chief Musician. Upon the Gittith. [A Psalm] of Asaph. Sing ye joyously unto God our strength, shout aloud unto the God of Jacob;
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Raise a song, and sound the tambour, the pleasant harp with the lute.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Blow the trumpet at the new moon, at the set time, on our feast day:
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 For this is a statute for Israel, an ordinance of the God of Jacob;
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 He ordained it in Joseph [for] a testimony, when he went forth over the land of Egypt, [where] I heard a language that I knew not.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 I removed his shoulder from the burden; his hands were freed from the basket.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 Thou calledst in trouble, and I delivered thee; I answered thee in the secret place of thunder; I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Hear, my people, and I will testify unto thee; O Israel, if thou wouldest hearken unto me!
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 There shall no strange god be in thee, neither shalt thou worship any foreign god.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 I am Jehovah thy God, that brought thee up out of the land of Egypt: open thy mouth wide, and I will fill it.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 But my people hearkened not to my voice, and Israel would none of me.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 So I gave them up unto their own hearts' stubbornness: they walked after their own counsels.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 Oh that my people had hearkened unto me, that Israel had walked in my ways!
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 I would soon have subdued their enemies, and turned my hand against their adversaries.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 The haters of Jehovah would have come cringing unto him; but their time would have been for ever.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 And he would have fed them with the finest of wheat; yea, with honey out of the rock would I have satisfied thee.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Psalms 81 >