< Psalms 64 >

1 To the chief Musician. A Psalm of David. Hear, O God, my voice in my plaint; preserve my life from fear of the enemy:
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
2 Hide me from the secret counsel of evil-doers, from the tumultuous crowd of the workers of iniquity,
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
3 Who have sharpened their tongue like a sword, [and] have aimed their arrow, a bitter word;
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
4 That they may shoot in secret at the perfect: suddenly do they shoot at him, and fear not.
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
5 They encourage themselves in an evil matter, they concert to hide snares; they say, Who will see them?
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
6 They devise iniquities: We have it ready, the plan is diligently sought out. And each one's inward [thought] and heart is deep.
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
7 But God will shoot an arrow at them: suddenly are they wounded;
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
8 By their own tongue they are made to fall over one another: all that see them shall flee away.
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
9 And all men shall fear, and shall declare God's doing; and they shall wisely consider his work.
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
10 The righteous shall rejoice in Jehovah, and trust in him; and all the upright in heart shall glory.
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.

< Psalms 64 >