< Psalms 46 >
1 To the chief Musician. Of the sons of Korah. On Alamoth. A song. God is our refuge and strength, a help in distresses, very readily found.
Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
2 Therefore will we not fear though the earth be removed, and though the mountains be carried into the heart of the seas;
Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
3 Though the waters thereof roar [and] foam, though the mountains shake with the swelling thereof. (Selah)
hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
4 There is a river the streams whereof make glad the city of God, the sanctuary of the habitations of the Most High.
Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
5 God is in the midst of her; she shall not be moved: God shall help her at the dawn of the morning.
Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
6 The nations raged, the kingdoms were moved; he uttered his voice, the earth melted.
Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
7 Jehovah of hosts is with us; the God of Jacob is our high fortress. (Selah)
Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
8 Come, behold the works of Jehovah, what desolations he hath made in the earth:
Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
9 He hath made wars to cease unto the end of the earth; he breaketh the bow, and cutteth the spear in sunder; he burneth the chariots in the fire.
Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
10 Be still, and know that I am God: I will be exalted among the nations, I will be exalted in the earth.
Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
11 Jehovah of hosts is with us; the God of Jacob is our high fortress. (Selah)
Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah