< Psalms 46 >
1 To the chief Musician. Of the sons of Korah. On Alamoth. A song. God is our refuge and strength, a help in distresses, very readily found.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Therefore will we not fear though the earth be removed, and though the mountains be carried into the heart of the seas;
Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
3 Though the waters thereof roar [and] foam, though the mountains shake with the swelling thereof. (Selah)
Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
4 There is a river the streams whereof make glad the city of God, the sanctuary of the habitations of the Most High.
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 God is in the midst of her; she shall not be moved: God shall help her at the dawn of the morning.
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 The nations raged, the kingdoms were moved; he uttered his voice, the earth melted.
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 Jehovah of hosts is with us; the God of Jacob is our high fortress. (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Come, behold the works of Jehovah, what desolations he hath made in the earth:
Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 He hath made wars to cease unto the end of the earth; he breaketh the bow, and cutteth the spear in sunder; he burneth the chariots in the fire.
Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
10 Be still, and know that I am God: I will be exalted among the nations, I will be exalted in the earth.
“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
11 Jehovah of hosts is with us; the God of Jacob is our high fortress. (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.