< Psalms 36 >
1 To the chief Musician. [A Psalm] of the servant of Jehovah; of David. The transgression of the wicked uttereth within my heart, There is no fear of God before his eyes.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 For he flattereth himself in his own eyes, [even] when his iniquity is found to be hateful.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 The words of his mouth are wickedness and deceit: he hath left off to be wise, to do good.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 He deviseth wickedness up on his bed; he setteth himself in a way that is not good: he abhorreth not evil.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 Jehovah, thy loving-kindness is in the heavens, and thy faithfulness [reacheth] unto the clouds.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Thy righteousness is like the high mountains; thy judgments are a great deep: thou, Jehovah, preservest man and beast.
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 How precious is thy loving-kindness, O God! So the sons of men take refuge under the shadow of thy wings.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 They shall be abundantly satisfied with the fatness of thy house; and thou wilt make them drink of the river of thy pleasures.
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 For with thee is the fountain of life: in thy light shall we see light.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Continue thy loving-kindness unto them that know thee, and thy righteousness to the upright in heart;
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 Let not the foot of pride come against me, and let not the hand of the wicked drive me away.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 There are the workers of iniquity fallen: they are cast down, and are not able to rise.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!