< Psalms 22 >
1 To the chief Musician. Upon Aijeleth-Shahar. A Psalm of David. My God, my God, why hast thou forsaken me? [why art thou] far from my salvation, from the words of my groaning?
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
2 My God, I cry by day, and thou answerest not; and by night, and there is no rest for me:
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
3 And thou art holy, thou that dwellest amid the praises of Israel.
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
4 Our fathers confided in thee: they confided, and thou didst deliver them.
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
5 They cried unto thee, and were delivered; they confided in thee, and were not confounded.
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
6 But I am a worm, and no man; a reproach of men, and the despised of the people.
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
7 All they that see me laugh me to scorn; they shoot out the lip, they shake the head, [saying: ]
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
8 Commit it to Jehovah — let him rescue him; let him deliver him, because he delighteth in him!
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
9 But thou art he that took me out of the womb; thou didst make me trust, upon my mother's breasts.
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
10 I was cast upon thee from the womb; thou art my God from my mother's belly.
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
11 Be not far from me, for trouble is near; for there is none to help.
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
12 Many bulls have encompassed me; Bashan's strong ones have beset me round.
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
13 They gape upon me with their mouth, [as] a ravening and a roaring lion.
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
14 I am poured out like water, and all my bones are out of joint: my heart is become like wax; it is melted in the midst of my bowels.
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
15 My strength is dried up like a potsherd, and my tongue cleaveth to my palate; and thou hast laid me in the dust of death.
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16 For dogs have encompassed me; an assembly of evil-doers have surrounded me: they pierced my hands and my feet.
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 I may count all my bones. They look, they stare upon me;
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18 They part my garments among them, and cast lots upon my vesture.
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19 But thou, Jehovah, be not far [from me]; O my strength, haste thee to help me.
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20 Deliver my soul from the sword; my only one from the power of the dog;
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
21 Save me from the lion's mouth. Yea, from the horns of the buffaloes hast thou answered me.
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
22 I will declare thy name unto my brethren, in the midst of the congregation will I praise thee.
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
23 Ye that fear Jehovah, praise him; all ye the seed of Jacob, glorify him; and revere him, all ye the seed of Israel.
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
24 For he hath not despised nor abhorred the affliction of the afflicted; neither hath he hid his face from him: but when he cried unto him, he heard.
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
25 My praise is from thee, in the great congregation; I will pay my vows before them that fear him.
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
26 The meek shall eat and be satisfied; they shall praise Jehovah that seek him: your heart shall live for ever.
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
27 All the ends of the earth shall remember and turn unto Jehovah, and all the families of the nations shall worship before thee:
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
28 For the kingdom is Jehovah's, and he ruleth among the nations.
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
29 All the fat ones of the earth shall eat and worship; all they that go down to the dust shall bow before him, and he that cannot keep alive his own soul.
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
30 A seed shall serve him; it shall be accounted to the Lord for a generation.
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
31 They shall come, and shall declare his righteousness unto a people that shall be born, that he hath done [it].
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!