< Psalms 19 >

1 To the chief Musician. A Psalm of David. The heavens declare the glory of God; and the expanse sheweth the work of his hands.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 Day unto day uttereth speech, and night unto night sheweth knowledge.
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3 There is no speech and there are no words, yet their voice is heard.
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
4 Their line is gone out through all the earth, and their language to the extremity of the world. In them hath he set a tent for the sun,
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 And he is as a bridegroom going forth from his chamber; he rejoiceth as a strong man to run the race.
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
6 His going forth is from the end of the heavens, and his circuit unto the ends of it; and there is nothing hid from the heat thereof.
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
7 The law of Jehovah is perfect, restoring the soul; the testimony of Jehovah is sure, making wise the simple;
Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
8 The precepts of Jehovah are right, rejoicing the heart; the commandment of Jehovah is pure, enlightening the eyes;
Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
9 The fear of Jehovah is clean, enduring for ever; the judgments of Jehovah are truth, they are righteous altogether:
Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
10 They are more precious than gold, yea, than much fine gold; and sweeter than honey and the dropping of the honeycomb.
Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
11 Moreover, by them is thy servant enlightened; in keeping them there is great reward.
Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
12 Who understandeth [his] errors? Purify me from secret [faults].
Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
13 Keep back thy servant also from presumptuous [sins]; let them not have dominion over me: then shall I be perfect, and I shall be innocent from great transgression.
Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
14 Let the words of my mouth and the meditation of my heart be acceptable in thy sight, O Jehovah, my rock, and my redeemer.
Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

< Psalms 19 >