< Psalms 114 >
1 When Israel went out of Egypt, the house of Jacob from a people of strange language,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Judah was his sanctuary, Israel his dominion.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 The sea saw it and fled, the Jordan turned back;
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 The mountains skipped like rams, the hills like lambs.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 What ailed thee, thou sea, that thou fleddest? thou Jordan, that thou turnedst back?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 Ye mountains, that ye skipped like rams? ye hills, like lambs?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Tremble, thou earth, at the presence of the Lord, at the presence of the God of Jacob,
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 Who turned the rock into a pool of water, the flint into a fountain of waters.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.