< Psalms 113 >
1 Hallelujah! Praise, ye servants of Jehovah, praise the name of Jehovah.
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
2 Blessed be the name of Jehovah, from this time forth and for evermore!
Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun unto the going down of the same, let Jehovah's name be praised.
Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
4 Jehovah is high above all nations, his glory above the heavens.
Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
5 Who is like unto Jehovah our God, who hath placed his dwelling on high;
Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
6 Who humbleth himself to look on the heavens and on the earth?
atazamaye chini angani na duniani?
7 He raiseth up the poor out of the dust; from the dung-hill he lifteth up the needy,
Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
8 To set [him] among nobles, among the nobles of his people.
ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 He maketh the barren woman to keep house, [as] a joyful mother of sons. Hallelujah!
Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!