< Psalms 106 >

1 Hallelujah! Give ye thanks unto Jehovah; for he is good; for his loving-kindness [endureth] for ever.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Who can utter the mighty acts of Jehovah? [who] can shew forth all his praise?
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Blessed are they that keep justice, [and] he that doeth righteousness at all times.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Remember me, O Jehovah, with [thy] favour toward thy people; visit me with thy salvation:
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 That I may see the prosperity of thy chosen ones, that I may rejoice in the joy of thy nation, that I may glory with thine inheritance.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 We have sinned with our fathers, we have committed iniquity, we have done wickedly.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Our fathers in Egypt considered not thy wondrous works; they remembered not the multitude of thy loving-kindnesses; but they rebelled at the sea, at the Red Sea.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Yet he saved them for his name's sake, that he might make known his might.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 And he rebuked the Red Sea, and it dried up; and he led them through the deeps as through a wilderness.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 And he saved them from the hand of him that hated [them], and redeemed them from the hand of the enemy.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 And the waters covered their oppressors: there was not one of them left.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Then believed they his words; they sang his praise.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 They soon forgot his works; they waited not for his counsel:
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 And they lusted exceedingly in the wilderness, and tempted God in the desert.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 Then he gave them their request, but sent leanness into their soul.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 And they envied Moses in the camp, [and] Aaron, the saint of Jehovah.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 The earth opened and swallowed up Dathan, and covered the company of Abiram;
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 And fire was kindled in their company; a flame burned up the wicked.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 They made a calf in Horeb, and did homage to a molten image;
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 And they changed their glory into the similitude of an ox that eateth grass.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 They forgot God their Saviour, who had done great things in Egypt,
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 Wondrous works in the land of Ham, terrible things by the Red Sea.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 And he said that he would destroy them, had not Moses, his chosen, stood before him in the breach, to turn away his fury, lest he should destroy [them].
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 And they despised the pleasant land; they believed not his word,
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 But murmured in their tents: they hearkened not unto the voice of Jehovah.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 And he lifted up his hand to them, that he would make them fall in the wilderness;
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 And that he would make their seed fall among the nations, and disperse them through the countries.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 And they joined themselves unto Baal-Peor, and ate the sacrifices of the dead;
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 And they provoked [him] to anger with their doings; and a plague broke out among them.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 Then stood up Phinehas and executed judgment, and the plague was stayed;
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 And that was reckoned unto him for righteousness, from generation to generation, for evermore.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 And they moved him to wrath at the waters of Meribah, and it went ill with Moses on their account;
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 For they provoked his spirit, so that he spoke unadvisedly with his lips.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 They did not destroy the peoples, as Jehovah commanded them;
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 But they mingled with the nations, and learned their works;
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 And they served their idols; and they were a snare unto them:
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 And they sacrificed their sons and their daughters unto demons,
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 And shed innocent blood, the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed unto the idols of Canaan; and the land was polluted with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 And they were defiled with their works, and went a-whoring in their doings.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 Then was the anger of Jehovah kindled against his people, and he abhorred his inheritance;
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 And he gave them into the hand of the nations; and they that hated them ruled over them:
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 And their enemies oppressed them, and they were brought into subjection under their hand.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Often did he deliver them; but as for them they provoked [him] by their counsel, and they were brought low by their iniquity.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 But he regarded their distress, when he heard their cry;
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 And he remembered for them his covenant, and repented according to the multitude of his loving-kindnesses;
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 And he caused them to find compassion of all those that had carried them captives.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Save us, Jehovah our God, and gather us from among the nations, to give thanks unto thy holy name, [and] to triumph in thy praise.
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Blessed be Jehovah the God of Israel, from eternity and to eternity! And let all the people say, Amen! Hallelujah!
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Psalms 106 >