< Proverbs 9 >
1 Wisdom hath built her house, she hath hewn out her seven pillars;
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 she hath slaughtered her cattle, she hath mingled her wine, she hath also prepared her table;
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 she hath sent forth her maidens: she crieth upon the summits of the high places of the city,
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 Whoso is simple, let him turn in hither. To him that is void of understanding, she saith,
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 Come, eat ye of my bread, and drink of the wine that I have mingled.
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Forsake follies and live, and go in the way of intelligence.
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 He that instructeth a scorner getteth to himself shame; and he that reproveth a wicked [man] [getteth] to himself a blot.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 Reprove not a scorner, lest he hate thee; reprove a wise [man], and he will love thee.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Impart to a wise [man], and he will become yet wiser; teach a righteous [man], and he will increase learning.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 The fear of Jehovah is the beginning of wisdom; and the knowledge of the Holy is intelligence.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 For by me thy days shall be multiplied, and years of life shall be added to thee.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 If thou art wise, thou shalt be wise for thyself; and if thou scornest, thou alone shalt bear it.
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 The foolish woman is clamorous; she is stupid, and knoweth nothing.
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 And she sitteth at the entry of her house, on a seat in the high places of the city,
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 to call passers-by who go right on their ways:
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 Whoso is simple, let him turn in hither. And to him that is void of understanding she saith,
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 Stolen waters are sweet, and the bread of secrecy is pleasant.
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 But he knoweth not that the dead are there; [that] her guests are in the depths of Sheol. (Sheol )
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol )