< Proverbs 21 >
1 The king's heart in the hand of Jehovah is [as] brooks of water: he turneth it whithersoever he will.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Every way of a man is right in his own eyes; but Jehovah weigheth the hearts.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 To exercise justice and judgment is more acceptable to Jehovah than sacrifice.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 Lofty eyes, and a proud heart, the lamp of the wicked, is sin.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 The thoughts of the diligent [tend] only to plenteousness; but of every one that is hasty, only to want.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 The getting of treasures by a lying tongue is a fleeting breath of them that seek death.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 The devastation of the wicked sweepeth them away, because they refuse to do what is right.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 Very crooked is the way of a guilty man; but as for the pure, his work is upright.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 It is better to dwell in a corner of the housetop, than with a contentious woman, and a house in common.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 The soul of the wicked desireth evil: his neighbour findeth no favour in his eyes.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 When the scorner is punished, the simple becometh wise; and when the wise is instructed, he receiveth knowledge.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 One that is righteous wisely considereth the house of the wicked: he overthroweth the wicked to [their] ruin.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 Whoso stoppeth his ears at the cry of the poor, he also himself shall cry, and shall not be heard.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 A gift in secret pacifieth anger; and a present in the bosom, vehement fury.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 It is joy to a righteous [man] to do what is right; but it is ruin for the workers of iniquity.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 The man that wandereth out of the way of wisdom shall abide in the congregation of the dead.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 He that loveth mirth shall be a poor man; he that loveth wine and oil shall not be rich.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 The wicked is a ransom for the righteous, and a treacherous [man] in the stead of the upright.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 It is better to dwell in a desert land. than with a contentious and irritable woman.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 There is costly store and oil in the dwelling of a wise [man]; but a foolish man swalloweth it up.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 He that followeth after righteousness and mercy findeth life, righteousness, and honour.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 A wise [man] scaleth the city of the mighty, and casteth down the strength of the confidence thereof.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 Whoso keepeth his mouth and his tongue keepeth his soul from troubles.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 Proud, arrogant, scorner is his name who dealeth in proud wrath.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 The desire of the sluggard killeth him; for his hands refuse to work:
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 He coveteth greedily all the day long; but the righteous giveth and spareth not.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 The sacrifice of the wicked is abomination: how much more when they bring it with a wicked purpose!
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 A lying witness shall perish; and a man that heareth shall speak constantly.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 A wicked man hardeneth his face; but as for the upright, he establisheth his way.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 There is no wisdom, nor understanding, nor counsel against Jehovah.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 The horse is prepared for the day of battle; but safety is of Jehovah.
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.