< Philemon 1 >
1 Paul, prisoner of Christ Jesus, and Timotheus the brother, to Philemon the beloved and our fellow-workman,
Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2 and to the sister Apphia and to Archippus our fellow-soldier, and to the assembly which [is] in thine house.
na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3 Grace to you and peace from God our Father, and [the] Lord Jesus Christ.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4 I thank my God, always making mention of thee at my prayers,
Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5 hearing of thy love and the faith which thou hast towards the Lord Jesus, and towards all the saints,
maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6 in such sort that thy participation in the faith should become operative in the acknowledgment of every good thing which is in us towards Christ [Jesus].
Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7 For we have great thankfulness and encouragement through thy love, because the bowels of the saints are refreshed by thee, brother.
Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8 Wherefore having much boldness in Christ to enjoin thee what is fitting,
Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9 for love's sake I rather exhort, being such a one as Paul the aged, and now also prisoner of Jesus Christ.
Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10 I exhort thee for my child, whom I have begotten in [my] bonds, Onesimus,
Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11 once unserviceable to thee, but now serviceable to thee and to me:
Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12 whom I have sent back to thee: [but do thou receive] him, that is, my bowels:
Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13 whom I was desirous of keeping with myself, that for thee he might minister to me in the bonds of the glad tidings;
Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14 but I have wished to do nothing without thy mind, that thy good might not be as of necessity but of willingness:
Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15 for perhaps for this reason he has been separated [from thee] for a time, that thou mightest possess him fully for ever; (aiōnios )
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios )
16 not any longer as a bondman, but above a bondman, a beloved brother, specially to me, and how much rather to thee, both in [the] flesh and in [the] Lord?
Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17 If therefore thou holdest me to be a partner [with thee], receive him as me;
Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18 but if he have wronged thee anything or owe anything [to thee], put this to my account.
Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19 I Paul have written [it] with mine own hand; I will repay [it]: that I say not to thee that thou owest even thine own self also to me.
Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20 Yea, brother, I would have profit of thee in [the] Lord: refresh my bowels in Christ.
Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21 Being confident of thine obedience, I have written to thee, knowing that thou wilt do even more than I say.
Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22 But withal prepare me also a lodging; for I hope that I shall be granted to you through your prayers.
Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23 Epaphras salutes thee, my fellow-prisoner in Christ Jesus;
Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24 Mark, Aristarchus, Demas, Luke, my fellow-workmen.
Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25 The grace of our Lord Jesus Christ [be] with your spirit.
Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.