< Philemon 1 >

1 Paul, prisoner of Christ Jesus, and Timotheus the brother, to Philemon the beloved and our fellow-workman,
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
2 and to the sister Apphia and to Archippus our fellow-soldier, and to the assembly which [is] in thine house.
na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
3 Grace to you and peace from God our Father, and [the] Lord Jesus Christ.
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
4 I thank my God, always making mention of thee at my prayers,
Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
5 hearing of thy love and the faith which thou hast towards the Lord Jesus, and towards all the saints,
Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
6 in such sort that thy participation in the faith should become operative in the acknowledgment of every good thing which is in us towards Christ [Jesus].
Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
7 For we have great thankfulness and encouragement through thy love, because the bowels of the saints are refreshed by thee, brother.
Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
8 Wherefore having much boldness in Christ to enjoin thee what is fitting,
Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
9 for love's sake I rather exhort, being such a one as Paul the aged, and now also prisoner of Jesus Christ.
lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
10 I exhort thee for my child, whom I have begotten in [my] bonds, Onesimus,
Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
11 once unserviceable to thee, but now serviceable to thee and to me:
Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
12 whom I have sent back to thee: [but do thou receive] him, that is, my bowels:
Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
13 whom I was desirous of keeping with myself, that for thee he might minister to me in the bonds of the glad tidings;
Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
14 but I have wished to do nothing without thy mind, that thy good might not be as of necessity but of willingness:
Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
15 for perhaps for this reason he has been separated [from thee] for a time, that thou mightest possess him fully for ever; (aiōnios g166)
Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
16 not any longer as a bondman, but above a bondman, a beloved brother, specially to me, and how much rather to thee, both in [the] flesh and in [the] Lord?
Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
17 If therefore thou holdest me to be a partner [with thee], receive him as me;
Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
18 but if he have wronged thee anything or owe anything [to thee], put this to my account.
Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
19 I Paul have written [it] with mine own hand; I will repay [it]: that I say not to thee that thou owest even thine own self also to me.
Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
20 Yea, brother, I would have profit of thee in [the] Lord: refresh my bowels in Christ.
Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
21 Being confident of thine obedience, I have written to thee, knowing that thou wilt do even more than I say.
Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
22 But withal prepare me also a lodging; for I hope that I shall be granted to you through your prayers.
Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
23 Epaphras salutes thee, my fellow-prisoner in Christ Jesus;
Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
24 Mark, Aristarchus, Demas, Luke, my fellow-workmen.
na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
25 The grace of our Lord Jesus Christ [be] with your spirit.
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.

< Philemon 1 >