< Obadiah 1 >
1 The vision of Obadiah. Thus saith the Lord Jehovah concerning Edom: We have heard a report from Jehovah, and an ambassador is sent among the nations. Arise ye, and let us rise up against her in battle.
Maono ya Obadia. Bwana MUNGU asema hivi juu ya Edomu Tumesikia habari kutoka kwa Bwana, na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema, Inukeni! Tuinuke dhidi yake kwa vita!”
2 Behold, I have made thee small among the nations; thou art greatly despised.
Tazama, nitawafanya wadogo kati ya mataifa, mutadharauliwa sana.
3 The pride of thy heart hath deceived thee, thou that dwellest in the clefts of the rock, whose habitation is high; — he that saith in his heart, Who shall bring me down to the ground?
Kiburi cha moyo wako kimekudanganya wewe, wewe ambaye unishi katika makaburi ya miamba, katika nyumba yako ya juu; asemaye moyoni mwako, 'Ni nani atakayenishusha mimi chini?'
4 Though thou exalt thyself as the eagle, and though thou set thy nest among the stars, thence will I bring thee down, saith Jehovah.
Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko, asema Yahweh.
5 If thieves had come to thee, if robbers by night, (how art thou cut off!) would they not have stolen [till] they had had enough? If grape-gatherers had come to thee, would they not have left some gleanings?
Kama wezi walikuja kwako, ikiwa wanyang'anyi wangekujilia usiku (jinsi ungekatilwa mbali!), Wasingeweza kuiba vya kuwatosha? Ikiwa wakusanya zabibu wangekujilia, wasingeacha mavuno?
6 How is Esau searched! his hidden things sought out!
Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje!
7 All the men of thy confederacy have pushed thee to the border; the men that were at peace with thee have deceived thee, they have prevailed against thee; [they that eat] thy bread have laid a snare under thee. There is no understanding in him.
Watu wote wa ushirikiano wako watakupeleka katika njiani ya hadi mpakani. Watu waliokuwa na amani pamoja nawe wamekudanganya, na kukushinda. Wale wanaokula mkate wako wameweka mtego chini yako. Hakuna uelewa ndani yake.
8 Shall I not in that day, saith Jehovah, destroy the wise men out of Edom, and understanding out of the mount of Esau?
Je! Sikuweza siku hiyo, asema Bwana, kuwaangamiza watu wenye hekima kutoka Edomu na kuelewa kutoka mlima wa Esau?
9 And thy mighty men, O Teman, shall be dismayed, to the end that every one may be cut off from the mount of Esau by slaughter.
Mashujaa wako watafadhaika, Temani, ili kila mtu akatiliwe mbali kutoka mlima wa Esau kwa kuuawa.
10 Because of violence against thy brother Jacob, shame shall cover thee, and thou shalt be cut off for ever.
Kwa sababu ya ukatili uliofanywa kwa ndugu yako Yakobo, utafunikwa na aibu, nawe utakatiliwa mbali milele.
11 In the day that thou stoodest on the other side, in the day that strangers carried away captive his substance, and foreigners entered into his gates, and cast lots upon Jerusalem, even thou wast as one of them.
Siku ile ulikuwa umesimama, siku wageni walichukua mali zake, na waliokuwa wageni katika malango yake, na kupiga kura kwa Yerusalemu, wewe ulikuwa kama mmoja wao.
12 But thou shouldest not have looked on the day of thy brother in the day of his disaster; neither shouldest thou have rejoiced over the children of Judah in the day of their destruction; nor have opened wide thy mouth in the day of distress.
Lakini usifurahi siku ya ndugu yako, siku ya msiba wake, wala usifurahi juu ya watu wa Yuda siku ya uharibifu wao; msijisifu siku ya dhiki yao.
13 Thou shouldest not have entered into the gate of my people in the day of their calamity, nor have looked, even thou, on their affliction in the day of their calamity, neither shouldest thou have laid [hands] on their substance in the day of their calamity;
Usiingie mlango wa watu wangu siku ya msiba wao; usifurahi juu ya taabu yao siku ya msiba wao, wala msipotee utajiri wao siku ya uharibifu wao.
14 and thou shouldest not have stood on the crossway, to cut off those of his that did escape, nor have delivered up those remaining of him in the day of distress.
Usisimama kwenye njia panda, ili kuwakatilia mbali wakimbizi wake na usiwatoe waathirika wake katika siku ya dhiki.
15 For the day of Jehovah is near upon all the nations: as thou hast done, it shall be done unto thee: thy recompence shall return upon thine own head.
Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote. Kama ulivyofanya, itafanyika kwako; matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako mwenyewe.
16 For as ye have drunk upon my holy mountain, so shall all the nations drink continually; yea, they shall drink, and shall swallow down, and they shall be as though they had not been.
Kwa vile mlivyokunywa katika mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote yatakavyo kunywa daima. Watakunywa na kumeza na itakuwa kana kwamba hawakuwepo kabisa.
17 But upon mount Zion shall there be deliverance, and it shall be holy; and the house of Jacob shall possess their possessions.
Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale waliookoka na watakuwa watakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki miliki zao.
18 And the house of Jacob shall be a fire, and the house of Joseph a flame, and the house of Esau for stubble; and they shall kindle in them and devour them; and there shall not be any remaining of the house of Esau: for Jehovah hath spoken [it].
Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu ni mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaunguza, na kuwateketeza. Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau, kwa kuwa Bwana amesema.
19 And [they of] the south shall possess the mount of Esau; and they of the lowland the Philistines; yea, they shall possess the field of Ephraim and the field of Samaria; and Benjamin [shall possess] Gilead;
Wote kutoka Negebu watamiliki mlima wa Esau na wale wa Shepela watamiliki nchi ya Wafilisti. Wao wataimiliki nchi ya Efraimu na nchi ya Samaria; na Benyamini atamiliki Gileadi.
20 and the captives of this host of the children of Israel [shall possess] what belonged to the Canaanites, unto Zarephath; and the captives of Jerusalem, who [were] in Sepharad, shall possess the cities of the south.
Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli watamiliki ardhi ya Kanaani mpaka Sarepta. Wahamiaji wa Yerusalemu, waliopo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
21 And saviours shall come up on mount Zion, to judge the mount of Esau; and the kingdom shall be Jehovah's.
Waokoaji watakwenda hadi juu ya Mlima Sayuni kutawala nchi ya vilima ya Esau, na ufalme utakuwa wa Bwana.