< Numbers 25 >
1 And Israel abode in Shittim; and the people began to commit fornication with the daughters of Moab.
Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
2 And they invited the people to the sacrifices of their gods; and the people ate, and bowed down to their gods.
kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
3 And Israel joined himself to Baal-Peor; and the anger of Jehovah was kindled against Israel.
Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
4 And Jehovah said to Moses, Take all the heads of the people, and hang them up to Jehovah before the sun, that the fierce anger of Jehovah may be turned away from Israel.
BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
5 And Moses said to the judges of Israel, Slay every one his men that have joined themselves to Baal-Peor.
Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
6 And behold, a man of the children of Israel came and brought a Midianitish woman to his brethren, in the sight of Moses, and in the sight of the whole assembly of the children of Israel, who were weeping before the entrance of the tent of meeting.
Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
7 And Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, saw it, and rose up from among the assembly, and took a javelin in his hand,
Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
8 and he went after the man of Israel into the tent-chamber, and thrust both of them through, the man of Israel and the woman through her belly. And the plague was stayed from the children of Israel.
Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
9 And those that died in the plague were twenty-four thousand.
Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
10 And Jehovah spoke to Moses, saying,
BWANA akanena na Musa, akasema,
11 Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, hath turned my wrath away from the children of Israel, in that he was jealous with my jealousy among them, so that I consumed not the children of Israel in my jealousy.
“Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
12 Therefore say, Behold, I give unto him my covenant of peace!
Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
13 And he shall have it, and his seed after him, the covenant of an everlasting priesthood; because he was jealous for his God, and made atonement for the children of Israel.
Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
14 And the name of the man of Israel that was slain, who was slain with the Midianitish woman, was Zimri, the son of Salu, the prince of a father's house of the Simeonites.
Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
15 And the name of the Midianitish woman that was slain was Cozbi, the daughter of Zur; he was tribal head of a father's house in Midian.
Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
16 And Jehovah spoke to Moses, saying,
Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
17 Harass the Midianites, and smite them,
“Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
18 for they have harassed you with their wiles, wherewith they have beguiled you in the matter of Peor, and in the matter of Cozbi, the daughter of a prince of Midian, their sister, who was slain on the day of the plague because of the matter of Peor.
kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”