< Nehemiah 8 >

1 all the people gathered together as one man to the open place that was before the water-gate; and they spoke to Ezra the scribe to bring the book of the law of Moses, which Jehovah had commanded Israel.
watu wote wakakusanyika kama mtu mmoja kwenye uwanja mbele ya Lango la Maji. Wakamwambia Ezra mwandishi alete Kitabu cha Sheria ya Mose, ambacho Bwana aliamuru kwa ajili ya Israeli.
2 And Ezra the priest brought the law before the congregation, both of men and women, and all that could hear with understanding, on the first day of the seventh month.
Basi katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba, kuhani Ezra akaleta Sheria mbele ya kusanyiko, ambamo walikuwamo wanaume, wanawake na watu wote walioweza kufahamu.
3 And he read in it before the open place that was before the water-gate from the morning until midday, in presence of the men and the women, and those that could understand. And the ears of all the people were [attentive] to the book of the law.
Akaisoma kwa sauti kubwa tangu mapambazuko mpaka adhuhuri, akiwa ameuelekea uwanja uliokuwa mbele ya Lango la Maji mbele ya wanaume, wanawake na wengine ambao waliweza kufahamu. Watu wote wakasikiliza kwa makini kile Kitabu cha Sheria.
4 And Ezra the scribe stood upon a high stage of wood, which they had made for the purpose. And beside him stood Mattithiah, and Shema, and Anaiah, and Urijah, and Hilkijah, and Maaseiah on his right hand; and on his left hand, Pedaiah, and Mishael, and Malchijah, and Hashum, and Hashbaddana, Zechariah, Meshullam.
Mwandishi Ezra alikuwa amesimama juu ya jukwaa la miti lililojengwa kwa kusudi hilo. Karibu naye upande wa kuume alisimama Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya. Upande wake wa kushoto walikuwepo Pedaya, Mishaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu.
5 And Ezra opened the book in the sight of all the people, for he was above all the people; and when he opened it, all the people stood up.
Ezra akakifungua kile kitabu. Watu wote waliweza kumwona kwa sababu alikuwa amesimama juu zaidi, naye alipokifungua watu wote wakasimama.
6 And Ezra blessed Jehovah, the great God; and all the people answered, Amen, Amen! with lifting up of their hands; and they bowed their heads, and worshipped Jehovah with their faces to the ground.
Ezra akamsifu Bwana, Mungu mkuu, nao watu wote wakainua mikono yao na kuitikia, “Amen! Amen!” Kisha wakasujudu na kumwabudu Bwana hali nyuso zao zikigusa ardhi.
7 And Jeshua, and Bani, and Sherebiah, Jamin, Akkub, Shabbethai, Hodijah, Maaseiah, Kelita, Azariah, Jozabad, Hanan, Pelaiah, and the Levites, caused the people to understand the law; and the people [stood] in their place.
Watu wakiwa wamesimama pale, Walawi wafuatao waliwafunza ile Sheria: Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya.
8 And they read in the law of God distinctly out of the book, and gave the sense, and caused [them] to understand the reading.
Walisoma kutoka kile Kitabu cha Sheria ya Mungu, wakiifafanua na kuwapa maelezo ili watu waweze kufahamu kile kilichokuwa kikisomwa.
9 And Nehemiah, that is, the Tirshatha, and Ezra the priest the scribe, and the Levites that explained to the people, said to all the people, This day is holy to Jehovah your God: mourn not, nor weep. For all the people wept when they heard the words of the law.
Ndipo Nehemia aliyekuwa mtawala, Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia wote, “Siku hii ni takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msiomboleze wala msilie.” Kwa kuwa watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya ile Sheria.
10 And he said to them, Go your way, eat the fat, and drink the sweet, and send portions to them for whom nothing is prepared; for the day is holy to our Lord; and be not grieved, for the joy of Jehovah is your strength.
Nehemia akasema, “Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Bwana. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”
11 And the Levites quieted all the people, saying, Be still! for the day is holy; neither be grieved.
Walawi wakawatuliza watu wote wakisema, “Kuweni watulivu, kwa kuwa hii ni siku takatifu. Msihuzunike.”
12 And all the people went their way, to eat and to drink, and to send portions, and to make great rejoicing. For they had understood the words that were declared to them.
Kisha watu wote wakaondoka kwenda kula na kunywa, na kupeana sehemu ya chakula, na wakaadhimisha kwa furaha kubwa, kwa sababu sasa walifahamu maneno yale waliyokuwa wameelezwa.
13 And on the second day were gathered together the chief fathers of all the people, the priests, and the Levites, to Ezra the scribe, even to gain wisdom as to the words of the law.
Katika siku ya pili ya mwezi, wakuu wa mbari zote, pamoja na makuhani na Walawi, walikusanyika wakimzunguka Ezra mwandishi ili wapate kusikiliza kwa makini maneno ya Sheria.
14 And they found written in the law which Jehovah had commanded through Moses, that the children of Israel should dwell in booths in the feast of the seventh month,
Wakakuta imeandikwa katika ile Sheria, ambayo Bwana aliiamuru kupitia kwa Mose, kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba,
15 and that they should publish and proclaim through all their cities, and at Jerusalem, saying, Go forth to the mount, and fetch olive-branches, and wild olive-branches, and myrtle-branches, and palm-branches, and branches of thick trees, to make booths, as it is written.
na kwamba walipaswa kutangaza neno hili na kulieneza katika miji yao na katika Yerusalemu wakisema: “Enendeni katika nchi ya mlima na kuleta matawi kutoka miti ya mizeituni, mizeituni mwitu, mihadasi, mitende na miti ya kivuli, ili kutengeneza vibanda,” kama ilivyoandikwa.
16 And the people went forth and brought [them], and made themselves booths, everyone upon the roof of his house, and in their courts, and in the courts of the house of God, and in the open space of the water-gate, and in the open space of the gate of Ephraim.
Basi watu wakaenda na kuleta matawi, nao wakajijengea vibanda juu ya paa za nyumba zao, katika nyua zao, katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja karibu na Lango la Maji na uwanja wa Lango la Efraimu.
17 And all the congregation of them that had come back from the captivity made booths, and dwelt in the booths. For since the days of Jeshua the son of Nun until that day had not the children of Israel done so. And there was very great gladness.
Jamii yote ya watu waliorudi kutoka utumwani wakajenga vibanda na kuishi ndani yake. Tangu wakati wa Yoshua mwana wa Nuni mpaka siku ile, Waisraeli hawakuwahi kuiadhimisha namna hii. Furaha yao ilikuwa kubwa sana.
18 Also day by day, from the first day to the last day, he read in the book of the law of God. And they observed the feast seven days; and on the eighth day was a solemn assembly, according to the ordinance.
Siku baada ya siku, kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho, Ezra alisoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakaiadhimisha sikukuu ile kwa siku saba, nayo siku ya nane, kufuatana na maagizo, kulikuwa na kusanyiko maalum.

< Nehemiah 8 >