< Matthew 17 >
1 And after six days Jesus takes with [him] Peter, and James, and John his brother, and brings them up into a high mountain apart.
Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu.
2 And he was transfigured before them. And his face shone as the sun, and his garments became white as the light;
Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3 and lo, Moses and Elias appeared to them talking with him.
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
4 And Peter answering said to Jesus, Lord, it is good we should be here. If thou wilt, let us make here three tabernacles: for thee one, and for Moses one, and one for Elias.
Hapo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.”
5 While he was still speaking, behold, a bright cloud overshadowed them, and lo, a voice out of the cloud, saying, This is my beloved Son, in whom I have found my delight: hear him.
Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni.”
6 And the disciples hearing [it] fell upon their faces, and were greatly terrified.
Wanafunzi waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
7 And Jesus coming to [them] touched them, and said, Rise up, and be not terrified.
Yesu akawaendea, akawagusa, akasema, “Simameni, msiogope!”
8 And lifting up their eyes, they saw no one but Jesus alone.
Walipoinua macho yao hawakumwona mtu, ila Yesu peke yake.
9 And as they descended from the mountain, Jesus charged them, saying, Tell the vision to no one, until the Son of man be risen up from among [the] dead.
Basi, walipokuwa wanashuka mlimani, Yesu akawaonya: “Msimwambie mtu mambo mliyoyaona mpaka Mwana wa Mtu atakapofufuliwa kutoka wafu.”
10 And [his] disciples demanded of him saying, Why then say the scribes that Elias must first have come?
Kisha wanafunzi wakamwuliza, “Mbona walimu wa Sheria wanasema ati ni lazima kwanza Eliya aje?”
11 And he answering said to them, Elias indeed comes first and will restore all things.
Yesu akawajibu, “Kweli, Eliya atakuja kutayarisha mambo yote.
12 But I say unto you that Elias has already come, and they have not known him, but have done unto him whatever they would. Thus also the Son of man is about to suffer from them.
Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja nao hawakumtambua, bali walimtendea jinsi walivyotaka. Mwana wa Mtu atateswa vivyo hivyo mikononi mwao.”
13 Then the disciples understood that he spoke to them of John the baptist.
Hapo hao wanafunzi wakafahamu kwamba alikuwa akiwaambia juu ya Yohane mbatizaji.
14 And when they came to the crowd, a man came to him, falling on his knees before him, and saying,
Walipojiunga tena na ule umati wa watu, mtu mmoja alimwendea Yesu, akampigia magoti,
15 Lord, have mercy on my son, for he is lunatic, and suffers sorely; for often he falls into the fire and often into the water.
akasema, “Mheshimiwa, mwonee huruma mwanangu kwa kuwa ana kifafa, tena anateseka sana; mara nyingi yeye huanguka motoni na majini.
16 And I brought him to thy disciples, and they were not able to heal him.
Nilimleta kwa wanafunzi wako lakini hawakuweza kumponya.”
17 And Jesus answering said, O unbelieving and perverted generation, how long shall I be with you? how long shall I bear with you? Bring him here to me.
Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia ninyi mpaka lini? Mleteni hapa huyo mtoto.”
18 And Jesus rebuked him, and the demon went out from him, and the boy was healed from that hour.
Basi, Yesu akamkemea huyo pepo, naye akamtoka, na yule mtoto akapona wakati huohuo.
19 Then the disciples, coming to Jesus apart, said [to him], Why were not we able to cast him out?
Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha, wakamwuliza, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo?”
20 And he says to them, Because of your unbelief; for verily I say unto you, If ye have faith as a grain of mustard [seed], ye shall say to this mountain, Be transported hence there, and it shall transport itself; and nothing shall be impossible to you.
Yesu akawajibu, “Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, hata iwe ndogo kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: Toka hapa uende pale, nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu.”
21 But this kind does not go out but by prayer and fasting.
“Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga.”
22 And while they abode in Galilee, Jesus said to them, The Son of man is about to be delivered up into [the] hands of men,
Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, “Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.
23 and they shall kill him; and the third day he shall be raised up. And they were greatly grieved.
Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa.” Wanafunzi wakahuzunika mno.
24 And when they came to Capernaum, those who received the didrachmas came to Peter and said, Does your teacher not pay the didrachmas?
Walipofika Kafarnaumu watu wenye kukusanya fedha ya zaka ya Hekalu walimwendea Petro, wakamwuliza, “Je, mwalimu wenu hulipa fedha ya zaka?”
25 He says, Yes. And when he came into the house, Jesus anticipated him, saying, What dost thou think, Simon? the kings of the earth, from whom do they receive custom or tribute? from their own sons or from strangers?
Petro akajibu, “Naam, hulipa.” Basi, Petro alipoingia ndani ya nyumba, kabla hata hajasema neno, Yesu akamwuliza, “Simoni, wewe unaonaje? Wafalme wa dunia hukusanya ushuru au kodi kutoka kwa kina nani? Kutoka kwa wananchi ama kutoka kwa wageni?”
26 Peter says to him, From strangers. Jesus said to him, Then are the sons free.
Petro akajibu, “Kutoka kwa wageni.” Yesu akamwambia, “Haya basi, wananchi hawahusiki.
27 But that we may not be an offence to them, go to the sea and cast a hook, and take the first fish that comes up, and when thou hast opened its mouth thou wilt find a stater; take that and give it to them for me and thee.
Lakini kusudi tusiwakwaze, nenda ziwani ukatupe ndoana; chukua samaki wa kwanza atakayenaswa, fungua kinywa chake, na ndani utakuta fedha taslimu ya zaka. Ichukue ukawape kwa ajili yangu na kwa ajili yako.”