< Mark 10 >
1 And rising up thence he comes into the coasts of Judaea, and the other side of the Jordan. And again crowds come together to him, and, as he was accustomed, again he taught them.
Yesu aliondoka eneo hilo na akaenda katika mkoa wa Uyahudi na eneo la mbele ya Mto Yorodani, na makutano walimfuata tena. Aliwafundisha tena, kama ilivyokuwa kawaida yake kufanya.
2 And Pharisees coming to [him] asked him, Is it lawful for a man to put away [his] wife? (tempting him).
Na Mafarisayo walikuja kumjaribu na wakamuuliza, “Ni halali kwa mwanamume kuachana na mke wake?”
3 But he answering said to them, What did Moses command you?
Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuru nini?”
4 And they said, Moses allowed to write a bill of divorce, and to put away.
Wakasema, “Musa aliruhusu kuandika cheti cha kuachana na kisha kumfukuza mwanamke.”
5 And Jesus answering said to them, In view of your hard-heartedness he wrote this commandment for you;
“Ni kwa sababu ya mioyo yenu migumu ndiyo maana aliwaandikia sheria hii,” Yesu aliwaambia.
6 but from [the] beginning of [the] creation God made them male and female.
“Lakini kutoka mwanzo wa uumbaji, 'Mungu aliwaumba mwanamume na mwanamke.'
7 For this cause a man shall leave his father and mother and shall be united to his wife,
Kwa sababu hii mwanamume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake,
8 and the two shall be one flesh: so that they are no longer two but one flesh.
na hao wawili watakuwa mwili mmoja; Kwa kuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
9 What therefore God has joined together, let not man separate.
Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 And again in the house the disciples asked him concerning this.
Walipokuwa ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza tena kuhusu hili.
11 And he says to them, Whosoever shall put away his wife and shall marry another, commits adultery against her.
Akawaambia, “Yeyote amwachaye mke wake na kumwoa mwanamke mwingine, anafanya uzinzi dhidi yake.
12 And if a woman put away her husband and shall marry another, she commits adultery.
Mwanamke naye akimwacha mme wake na kuolewa na mwanamme mwingine, anafanya uzinzi.”
13 And they brought little children to him that he might touch them. But the disciples rebuked those that brought [them].
Nao walimletea watoto wao wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
14 But Jesus seeing [it], was indignant, and said to them, Suffer the little children to come to me; forbid them not; for of such is the kingdom of God.
Lakini Yesu alipotambua hilo, hakufurahishwa nalo kabisa akawaambia, “Waruhusuni watoto wadogo waje kwangu, na msiwazuie, kwa sababu walio kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
15 Verily I say to you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child, shall in no wise enter into it.
Ukweli nawaambia, yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hakika hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
16 And having taken them in his arms, having laid his hands on them, he blessed them.
Kisha akawachukua watoto mikononi mwake na akawabariki akiwawekea mikono yake juu yao.
17 And as he went forth into the way, a person ran up to [him], and kneeling to him asked him, Good Teacher, what shall I do that I may inherit eternal life? (aiōnios )
Na alipoanza safari yake mtu mmoja alimkimbilia na akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu Mwema, nifanye nini ili niweze kurithi uzima ya milele?” (aiōnios )
18 But Jesus said to him, Why callest thou me good? no one is good but one, [that is] God.
Na Yesu akasema, “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa Mungu peke yake.
19 Thou knowest the commandments: Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Do not defraud, Honour thy father and mother.
Unazijua amri: 'Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, mheshimu baba na mama yako'.”
20 And he answering said to him, Teacher, all these things have I kept from my youth.
Mtu yule akasema, “Mwalimu, haya yote nimeyatii tangu nikiwa kijana.”
21 And Jesus looking upon him loved him, and said to him, One thing lackest thou: go, sell whatever thou hast and give to the poor, and thou shalt have treasure in heaven; and come, follow me, [taking up the cross].
Yesu alimwangalia na kumpenda. Akawambia, “Unapungukiwa kitu kimoja. Unapaswa kuuza vyote ulivyo navyo na uwape masikini, na utakuwa na hazina mbinguni. Ndipo uje unifuate.”
22 But he, sad at the word, went away grieved, for he had large possessions.
Lakini alikata tamaa kwa sababu ya maelezo haya; aliondoka akiwa mwenye huzuni, kwa kuwa alikuwa na mali nyingi.
23 And Jesus looking around says to his disciples, How difficultly shall they that have riches enter into the kingdom of God!
Yesu akatazama pande zote na kuwaambia wanafunzi wake, “Ni jinsi gani ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu!
24 And the disciples were amazed at his words. And Jesus again answering says to them, Children, how difficult it is that those who trust in riches should enter into the kingdom of God!
Wanafunzi walishangazwa kwa maneno haya. Lakini Yesu akawaambia tena, “Watoto, ni jinsi gani ilivyo vigumu kuingia katika ufalme wa Mungu!
25 It is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich man to enter into the kingdom of God.
Ni rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano, kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”
26 And they were exceedingly astonished, saying to one another, And who can be saved?
Walishangazwa sana na wakasemezana, “Hivyo nani ataokoka”
27 But Jesus looking on them says, With men it is impossible, but not with God; for all things are possible with God.
Yesu akawaangalia na kusema, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini sio kwa Mungu. Kwa kuwa katika Mungu yote yanawezekana.”
28 Peter began to say to him, Behold, we have left all things and have followed thee.
“Petro akaanza kuzungumza naye, “Angalia tumeacha vyote na tumekufuata.”
29 Jesus answering said, Verily I say to you, There is no one who has left house, or brethren, or sisters, or father, or mother, [or wife], or children, or lands, for my sake and for the sake of the gospel,
Yesu akasema, “Ukweli nawaambia ninyi, hakuna aliyeacha nyumba, au kaka, au dada, au mama, au baba, au watoto, au ardhi, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 that shall not receive a hundredfold now in this time: houses, and brethren, and sisters, and mothers, and children, and lands, with persecutions, and in the coming age life eternal. (aiōn , aiōnios )
ambaye hatapokea mara mia zaidi ya sasa hapa duniani: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, na ardhi, kwa mateso, na ulimwengu ujao, uzima wa milele. (aiōn , aiōnios )
31 But many first shall be last, and the last first.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 And they were in the way going up to Jerusalem, and Jesus was going on before them; and they were amazed, and were afraid as they followed. And taking the twelve again to [him], he began to tell them what was going to happen to him:
Walipokuwa njiani, kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa amewatangulia mbele yao. Wanafunzi walishangaa, na wale waliokuwa wanafuata nyuma waliogopa. Ndipo Yesu akawatoa pembeni tena wale kumi na wawili na akaanza kuwaambia ambacho kitamtokea hivi karibuni:
33 Behold, we go up to Jerusalem, and the Son of man shall be delivered up to the chief priests and to the scribes, and they shall condemn him to death, and shall deliver him up to the nations:
“Tazama, tunakwenda mpaka Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atafikishwa kwa makuhani wakuu na waandishi. Watamhukumu afe na watamtoa kwa watu wa Mataifa.
34 and they shall mock him, and shall scourge him, and shall spit upon him, and shall kill him; and after three days he shall rise again.
Watamdhihaki, watamtemea mate, watampiga fimbo, na watamwua. Lakini baada ya siku tatu atafufuka.”
35 And there come to him James and John, the sons of Zebedee, saying [to him], Teacher, we would that whatsoever we may ask thee, thou wouldst do it for us.
Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walikuja kwake na kusema, “Mwalimu, tunakuhitaji utufanyie chochote tukuombacho.”
36 And he said to them, What would ye that I should do for you?
Aliwaambia, “Mnataka niwatendee nini?”
37 And they said to him, Give to us that we may sit, one on thy right hand, and one on thy left hand, in thy glory.
Wakasema, “Turuhusu tukae nawe katika utukufu wako, mmoja katika mkono wako wa kuume na mwingine mkono wako wa kushoto.”
38 And Jesus said to them, Ye do not know what ye ask. Are ye able to drink the cup which I drink, or be baptised with the baptism that I am baptised with?
Lakini Yesu aliwajibu, “Hamjui mnachoomba. Mnaweza kukinywea kikombe ambacho nitakiywea au kustahimili ubatizo ambao nitabatizwa?”
39 And they said to him, We are able. And Jesus said to them, The cup that I drink ye will drink and with the baptism that I am baptised with ye will be baptised,
Wakamwambia, “Tunaweza” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokinywea, mtakinywea. Na ubatizo ambao kwao nimebatizwa, mtaustahimili.
40 but to sit on my right hand or on my left is not mine to give, but for those for whom it is prepared.
Lakini atakayekaa mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto sio mimi wa kutoa, lakini ni kwa wale ambao kwao imekwisha andaliwa.”
41 And the ten having heard [of it], began to be indignant about James and John.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 But Jesus having called them to [him], says to them, Ye know that those who are esteemed to rule over the nations exercise lordship over them; and their great men exercise authority over them;
Yesu akawaita kwake na kusema, “Mnajua kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala, na watu wao mashuhuri huwaonyesha mamlaka juu yao.”
43 but it is not thus among you; but whosoever would be great among you, shall be your minister;
Lakini haipaswi kuwa hivi kati yenu. Yeyote atakaye kuwa mkubwa kati yenu lazima awatumikie,
44 and whosoever would be first of you shall be bondman of all.
na yeyote atakaye kuwa wa kwanza kati yenu ni lazima awe mtumwa wa wote.
45 For also the Son of man did not come to be ministered to, but to minister, and give his life a ransom for many.
Kwa kuwa Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa bali kutumika, na kuyatoa maisha yake kuwa fidia kwa wengi.”
46 And they come to Jericho, and as he was going out from Jericho, and his disciples and a large crowd, the son of Timaeus, Bartimaeus, the blind [man], sat by the wayside begging.
Wakaja Yeriko. Alipokuwa akiondoka Yeriko na wanafunzi wake na kundi kubwa, mwana wa Timayo, Batimayo, kipofu mwombaji, alikaa kando ya barabara.
47 And having heard that it was Jesus the Nazaraean, he began to cry out and to say, O Son of David, Jesus, have mercy on me.
Aliposikia kuwa ni Yesu Mnazareti, alianza kupiga kelele na kusema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 And many rebuked him, that he might be silent; but he cried so much the more, Son of David, have mercy on me.
Wengi walimkemea yule kipofu, wakimwambia anyamaze. Lakini alilia kwa sauti zaidi, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 And Jesus, standing still, desired him to be called. And they call the blind [man], saying to him, Be of good courage, rise up, he calls thee.
Yesu alisimama na kuamuru aitwe. Walimwita yule kipofu, wakisema, “Kuwa shujaa! Inuka! Yesu anakuita.”
50 And, throwing away his garment, he started up and came to Jesus.
Akalitupa pembeni koti lake, akakimbia zaidi, na kuja kwa Yesu.
51 And Jesus answering says to him, What wilt thou that I shall do to thee? And the blind [man] said to him, Rabboni, that I may see.
Yesu akamjibu na kusema, “Unataka nikufanyie nini?” Yule mwanaume kipofu akamjibu, “Mwalimu, ninataka kuona.”
52 And Jesus said to him, Go, thy faith has healed thee. And he saw immediately, and followed him in the way.
Yesu akamwambia, “Nenda. Imani yako imekuponya.” Hapo hapo macho yake yakaona; na akamfuata Yesu barabarani.