< Luke 1 >
1 Forasmuch as many have undertaken to draw up a relation concerning the matters fully believed among us,
Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2 as those who from the beginning were eye-witnesses of and attendants on the Word have delivered them to us,
Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3 it has seemed good to me also, accurately acquainted from the origin with all things, to write to thee with method, most excellent Theophilus,
Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4 that thou mightest know the certainty of those things in which thou hast been instructed.
ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judaea, a certain priest, by name Zacharias, of the course of Abia, and his wife of the daughters of Aaron, and her name Elizabeth.
Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6 And they were both just before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7 And they had no child, because Elizabeth was barren, and they were both advanced in years.
Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it came to pass, as he fulfilled his priestly service before God in the order of his course,
Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9 it fell to him by lot, according to the custom of the priesthood, to enter into the temple of the Lord to burn incense.
Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10 And all the multitude of the people were praying without at the hour of incense.
Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11 And an angel of [the] Lord appeared to him, standing on the right of the altar of incense.
Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12 And Zacharias was troubled, seeing [him], and fear fell upon him.
Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 But the angel said to him, Fear not, Zacharias, because thy supplication has been heard, and thy wife Elizabeth shall bear thee a son, and thou shalt call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14 And he shall be to thee joy and rejoicing, and many shall rejoice at his birth.
Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he shall be great before [the] Lord, and he shall drink no wine nor strong drink; and he shall be filled with [the] Holy Spirit, even from his mother's womb.
Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 And many of the sons of Israel shall he turn to [the] Lord their God.
Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 And he shall go before him in [the] spirit and power of Elias, to turn hearts of fathers to children, and disobedient ones to [the] thoughts of just [men], to make ready for [the] Lord a prepared people.
Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18 And Zacharias said to the angel, How shall I know this, for I am an old man, and my wife advanced in years?
Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
19 And the angel answering, said to him, I am Gabriel, who stand before God, and I have been sent to speak to thee, and to bring these glad tidings to thee;
Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20 and behold, thou shalt be silent and not able to speak, till the day in which these things shall take place, because thou hast not believed my words, the which shall be fulfilled in their time.
Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21 And the people were awaiting Zacharias, and they wondered at his delaying in the temple.
Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22 But when he came out he could not speak to them, and they recognised that he had seen a vision in the temple. And he was making signs to them, and continued dumb.
Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23 And it came to pass, when the days of his service were completed, he departed to his house.
Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24 Now after these days, Elizabeth his wife conceived, and hid herself five months, saying,
Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25 Thus has [the] Lord done to me in [these] days in which he looked upon [me] to take away my reproach among men.
“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
26 But in the sixth month, the angel Gabriel was sent of God to a city of Galilee, of which [the] name [was] Nazareth,
Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27 to a virgin betrothed to a man whose name [was] Joseph, of the house of David; and the virgin's name [was] Mary.
kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28 And the angel came in to her, and said, Hail, [thou] favoured one! the Lord [is] with thee: [blessed art thou amongst women].
Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
29 But she, [seeing] [the angel], was troubled at his word, and reasoned in her mind what this salutation might be.
Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 And the angel said to her, Fear not, Mary, for thou hast found favour with God;
Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 and behold, thou shalt conceive in the womb and bear a son, and thou shalt call his name Jesus.
Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32 He shall be great, and shall be called Son of [the] Highest; and [the] Lord God shall give him the throne of David his father;
Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob for the ages, and of his kingdom there shall not be an end. (aiōn )
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 But Mary said to the angel, How shall this be, since I know not a man?
Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
35 And the angel answering said to her, [The] Holy Spirit shall come upon thee, and power of [the] Highest overshadow thee, wherefore the holy thing also which shall be born shall be called Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36 And behold, Elizabeth, thy kinswoman, she also has conceived a son in her old age, and this is the sixth month to her that was called barren:
Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37 for nothing shall be impossible with God.
Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
38 And Mary said, Behold the bondmaid of [the] Lord; be it to me according to thy word. And the angel departed from her.
Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
39 And Mary, rising up in those days, went into the hill country with haste, to a city of Judah,
Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40 and entered into the house of Zacharias, and saluted Elizabeth.
Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41 And it came to pass, as Elizabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped in her womb; and Elizabeth was filled with [the] Holy Spirit,
Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42 and cried out with a loud voice and said, Blessed [art] thou amongst women, and blessed the fruit of thy womb.
akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43 And whence [is] this to me, that the mother of my Lord should come to me?
Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For behold, as the voice of thy salutation sounded in my ears, the babe leaped with joy in my womb.
Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessed [is] she that has believed, for there shall be a fulfilment of the things spoken to her from [the] Lord.
Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46 And Mary said, My soul magnifies the Lord,
Naye Maria akasema,
47 and my spirit has rejoiced in God my Saviour.
“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48 For he has looked upon the low estate of his bondmaid; for behold, from henceforth all generations shall call me blessed.
Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49 For the Mighty One has done to me great things, and holy [is] his name;
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50 and his mercy [is] to generations and generations to them that fear him.
Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51 He has wrought strength with his arm; he has scattered haughty [ones] in the thought of their heart.
Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 He has put down rulers from thrones, and exalted the lowly.
amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53 He has filled the hungry with good things, and sent away the rich empty.
Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54 He has helped Israel his servant, in order to remember mercy,
Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55 (as he spoke to our fathers, ) to Abraham and to his seed for ever. (aiōn )
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn )
56 And Mary abode with her about three months, and returned to her house.
Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57 But the time was fulfilled for Elizabeth that she should bring forth, and she gave birth to a son.
Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58 And her neighbours and kinsfolk heard that [the] Lord had magnified his mercy with her, and they rejoiced with her.
Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59 And it came to pass on the eighth day they came to circumcise the child, and they called it after the name of his father, Zacharias.
Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60 And his mother answering said, No; but he shall be called John.
Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61 And they said to her, There is no one among thy kinsfolk who is called by this name.
Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62 And they made signs to his father as to what he might wish it to be called.
Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63 And having asked for a writing-table, he wrote saying, John is his name. And they all wondered.
Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64 And his mouth was opened immediately, and his tongue, and he spake, blessing God.
Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came upon all who dwelt round about them; and in the whole hill-country of Judaea all these things were the subject of conversation.
Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66 And all who heard them laid them up in their heart, saying, What then will this child be? And [the] Lord's hand was with him.
Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67 And Zacharias his father was filled with [the] Holy Spirit, and prophesied, saying,
Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68 Blessed be [the] Lord the God of Israel, because he has visited and wrought redemption for his people,
“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69 and raised up a horn of deliverance for us in the house of David his servant;
Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70 as he spoke by [the] mouth of his holy prophets, who have been since the world began; (aiōn )
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn )
71 deliverance from our enemies and out of the hand of all who hate us;
kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 to fulfil mercy with our fathers and remember his holy covenant,
Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73 [the] oath which he swore to Abraham our father,
Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74 to give us, that, saved out of the hand of our enemies, we should serve him without fear
tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75 in piety and righteousness before him all our days.
kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76 And thou, child, shalt be called [the] prophet of [the] Highest; for thou shalt go before the face of [the] Lord to make ready his ways;
Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77 to give knowledge of deliverance to his people by [the] remission of their sins
kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78 on account of [the] bowels of mercy of our God; wherein [the] dayspring from on high has visited us,
Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79 to shine upon them who were sitting in darkness and in [the] shadow of death, to guide our feet into [the] way of peace.
na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80 — And the child grew and was strengthened in spirit; and he was in the deserts until the day of his shewing to Israel.
Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.