< Luke 22 >

1 Now the feast of unleavened bread, which [is] called the passover, drew nigh,
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2 and the chief priests and the scribes sought how they might kill him; for they feared the people.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3 And Satan entered into Judas, who was surnamed Iscariote, being of the number of the twelve.
Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4 And he went away and spoke with the chief priests and captains as to how he should deliver him up to them.
Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5 And they were rejoiced, and agreed to give him money.
Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6 And he came to an agreement to do it, and sought an opportunity to deliver him up to them away from the crowd.
Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7 And the day of unleavened bread came, in which the passover was to be killed.
Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8 And he sent Peter and John, saying, Go and prepare the passover for us, that we may eat [it].
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
9 But they said to him, Where wilt thou that we prepare [it]?
Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
10 And he said to them, Behold, as ye enter into the city a man will meet you, carrying an earthen pitcher of water; follow him into the house where he goes in;
Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11 and ye shall say to the master of the house, The Teacher says to thee, Where is the guest-chamber where I may eat the passover with my disciples?
Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12 And he will shew you a large upper room furnished: there make ready.
Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
13 And having gone they found it as he had said to them; and they prepared the passover.
Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14 And when the hour was come, he placed himself at table, and the [twelve] apostles with him.
Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15 And he said to them, With desire I have desired to eat this passover with you before I suffer.
Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16 For I say unto you, that I will not eat any more at all of it until it be fulfilled in the kingdom of God.
Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
17 And having received a cup, when he had given thanks he said, Take this and divide it among yourselves.
Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18 For I say unto you, that I will not drink at all of the fruit of the vine until the kingdom of God come.
Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
19 And having taken a loaf, when he had given thanks, he broke [it], and gave [it] to them, saying, This is my body which is given for you: this do in remembrance of me.
Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
20 In like manner also the cup, after having supped, saying, This cup [is] the new covenant in my blood, which is poured out for you.
Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21 Moreover, behold, the hand of him that delivers me up [is] with me on the table;
“Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22 and the Son of man indeed goes as it is determined, but woe unto that man by whom he is delivered up.
Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
23 And they began to question together among themselves who then it could be of them who was about to do this.
Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24 And there was also a strife among them which of them should be held to be [the] greatest.
Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25 And he said to them, The kings of the nations rule over them, and they that exercise authority over them are called benefactors.
Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26 But ye [shall] not [be] thus; but let the greater among you be as the younger, and the leader as he that serves.
Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27 For which [is] greater, he that is at table or he that serves? [Is] not he that is at table? But I am in the midst of you as the one that serves.
Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28 But ye are they who have persevered with me in my temptations.
“Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29 And I appoint unto you, as my Father has appointed unto me, a kingdom,
na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30 that ye may eat and drink at my table in my kingdom, and sit on thrones judging the twelve tribes of Israel.
Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 And the Lord said, Simon, Simon, behold, Satan has demanded to have you, to sift [you] as wheat;
“Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32 but I have besought for thee that thy faith fail not; and thou, when once thou hast been restored, confirm thy brethren.
Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
33 And he said to him, Lord, with thee I am ready to go both to prison and to death.
Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
34 And he said, I tell thee, Peter, [the] cock shall not crow to-day before that thou shalt thrice deny that thou knowest me.
Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
35 And he said to them, When I sent you without purse and scrip and sandals, did ye lack anything? And they said, Nothing.
Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
36 He said therefore to them, But now he that has a purse let him take [it], in like manner also a scrip, and he that has none let him sell his garment and buy a sword;
Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37 for I say unto you, that this that is written must yet be accomplished in me, And he was reckoned with [the] lawless: for also the things concerning me have an end.
Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
38 And they said, Lord, behold here are two swords. And he said to them, It is enough.
Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
39 And going forth he went according to his custom to the mount of Olives, and the disciples also followed him.
Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40 And when he was at the place he said to them, Pray that ye enter not into temptation.
Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
41 And he was withdrawn from them about a stone's throw, and having knelt down he prayed,
Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42 saying, Father, if thou wilt remove this cup from me: — but then, not my will, but thine be done.
“Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
43 And an angel appeared to him from heaven strengthening him.
Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44 And being in conflict he prayed more intently. And his sweat became as great drops of blood, falling down upon the earth.
Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45 And rising up from his prayer, coming to the disciples, he found them sleeping from grief.
Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46 And he said to them, Why sleep ye? rise up and pray that ye enter not into temptation.
Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47 As he was yet speaking, behold, a crowd, and he that was called Judas, one of the twelve, went on before them, and drew near to Jesus to kiss him.
Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48 And Jesus said to him, Judas, deliverest thou up the Son of man with a kiss?
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49 And they who were around him, seeing what was going to follow, said [to him], Lord, shall we smite with [the] sword?
Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
50 And a certain one from among them smote the bondman of the high priest and took off his right ear.
Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51 And Jesus answering said, Suffer thus far; and having touched his ear, he healed him.
Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52 And Jesus said to the chief priests and captains of the temple and elders, who were come against him, Have ye come out as against a robber with swords and sticks?
Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53 When I was day by day with you in the temple ye did not stretch out your hands against me; but this is your hour and the power of darkness.
Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
54 And having laid hold on him, they led him [away], and they led [him] into the house of the high priest. And Peter followed afar off.
Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55 And they having lit a fire in the midst of the court and sat down together, Peter sat among them.
Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56 And a certain maid, having seen him sitting by the light, and having fixed her eyes upon him, said, And this [man] was with him.
Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
57 But he denied [him], saying, Woman, I do not know him.
Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
58 And after a short time another seeing him said, And thou art of them. But Peter said, Man, I am not.
Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
59 And after the lapse of about one hour another stoutly maintained it, saying, In truth this [man] also was with him, for also he is a Galilaean.
Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
60 And Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he was yet speaking, [the] cock crew.
Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61 And the Lord, turning round, looked at Peter; and Peter remembered the word of the Lord, how he said to him, Before [the] cock crow thou shalt deny me thrice.
Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
62 And Peter, going forth without, wept bitterly.
Hapo akatoka nje, akalia sana.
63 And the men who held him mocked him, beating [him];
Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64 and covering him up, asked him saying, Prophesy, who is it that struck thee?
Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
65 And they said many other injurious things to him.
Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66 And when it was day, the elderhood of the people, both [the] chief priests and scribes, were gathered together, and led him into their council, saying,
Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67 If thou art the Christ, tell us. And he said to them, If I tell you, ye will not at all believe;
Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68 and if I should ask [you], ye would not answer me at all, nor let me go;
na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69 but henceforth shall the Son of man be sitting on the right hand of the power of God.
Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
70 And they all said, Thou then art the Son of God? And he said to them, Ye say that I am.
Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
71 And they said, What need have we any more of witness, for we have heard ourselves out of his mouth?
Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”

< Luke 22 >